Ajikata uume wake na kuutupa. Akipona jeraha lake atafikishwa Mahakamani kujibu shtaka linalomkabili

Ajikata uume wake na kuutupa. Akipona jeraha lake atafikishwa Mahakamani kujibu shtaka linalomkabili

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Screenshot 2023-05-07 154944.png

Mwanaume mmoja ajulikaye kwa jina la Marco Samweli mwenye umri wa miaka 32 mkulima na mkazi wa Kijiji cha Kibitilo kata ya Ilula wilayani Kwimba mkoani Mwanza amejikata uume wake na kisha kuutupa kwa kutumia kisu kwa madai kuwa amechoka kuumwa ugonjwa uliokuwa unamsumbua.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa amesema tukio hilo limetokea may 5 mwaka huu majira ya saa saba usiku mara baada ya mwanaume huyo kutoka hospitali kwa maradhi yanayomsumbua ambapo inadaiwa aliugua kwa zaidi ya miaka mitano.

Aidha kamanda Mutafungwa amesema kwa sasa mgonjwa huyo anatibiwa katika hospitali ya rufaa ya kanda Bugando akiwa chini ya ulinzi wa jeshi hilo kutokana na kitendo alichofanya cha kujijeruhi na pindi atakapopona jeraha lake atafikishwa mahakamani kujibu shtaka linalomkabili.

Manara TV
 
Kafanya kwa hiari yake mwenyewe .... Huenda kinachomsumbua kinasababishwa na urinaji wa asali kwa kutumia kiungo hicho
 
Askari anaemlinda mgonjwa huyo ataongezewa posho ama mshahara utapanda?

Anyway, hizo ndo kazi za Askari wetu, kulinda wagonjwa hadi wapone.
 
Ni wa kumhurumia huyo mtu, atakuwa ana matatizo makubwa sana nahisi, si jambo la kawaida mtu kujikata kiungo chake bila ganzi. Ni sawa tu na wanaojaribu kujiua, lazima kuna mengi ya kuumiza yamemtokea.
 
Back
Top Bottom