Ajira za ualimu: serikali ije na majibu ya kueleweka juu ya walimu wangapi wa shahada 'degree' iliowaajiri

Ajira za ualimu: serikali ije na majibu ya kueleweka juu ya walimu wangapi wa shahada 'degree' iliowaajiri

msovero

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2019
Posts
863
Reaction score
1,534
Miongoni mwa mambo yanayotakiwa kutupiwa jicho ni ubaguzi uliopo kwenye utoaji wa ajira kwa kada mbali mbali ikiwemo ualimu

Serikali ya awamu ya tano chini ya utawala wa hayati Magufuli imekuwa ikitoa ajira za ualimu kwa upendeleo na ubaguzi bila kuzingatia usawa na elimu za waombaji

Tumeshuhudia kwa miaka mitano mfululizo walimu wenye elimu ya shahada 'degree' wakibaguliwa wazi wazi kwenye mchakato wa ajira. Si walimu wa sanaa wala wa sayansi wote kwa ujumla wao wamesomeshwa namba vyakutosha huku kipaumbele cha ajira wakipewa walimu wa cheti na stashahada pekee

Kwakuwa utawala umebadilika, chini ya Rais wa awamu ya sita mama yetu Samia Suluhu Hassan tunaamini serikali yake itaenda kufanya mabadiliko makubwa kwenye utoaji na upangaji wa ajira ili walimu wote bila kujari elimu zao waajiriwe kwa uwiano sawa bila ubaguzi wowote wa kielimu.

Hali hii imekuwa ikiwakatisha tamaa vijana wengi wenye elimu ya shahada kuomba ajira kwa sababu hata wanapoomba wanakuwa hawana matumaini ya kupata kwani kuna imani imejengeka kwamba serikali haiwaajiri ili kubana matumizi ya bajeti hususani kwenye upande wa mishahara.

Sasa basi ili kuondoa dhana hii Tunaiomba serikali itakapotangaza ajira 6000 za ualimu hivi karibuni ije na majibu ya kueleweka juu ya walimu wangapi wa shahada 'degree' iliyowaajiri ili kusudi kama idadi itakuwa ni ndogo basi vijana wajue namna ya kujipanga kufanya mambo mengine kuliko kupotezewa muda wao kuomba ajira ambazo hawaajiriki..!

KAZI IENDELEE....
 
Awamu ya Sita ndo kwanza umeanza kuajiri nakushauri tulia kwanza tuone mwenendo ndo utakuja na hoja yako sasa ni mapema mno
 
Awamu ya Sita ndo kwanza umeanza kuajiri nakushauri tulia kwanza tuone mwenendo ndo utakuja na hoja yako sasa ni mapema mno
ile kauli yake ya kusema yeye na mwendazake ni kitu kimoja nayo inatafakarisha mkuu huenda amejipanga kufuata nyayo zile zile kwahiyo lazima tutoe alert mapema
 
Kwenye ajira mwendazake alivuruga,hivyo hata Samia nae itabidi aende polepole
 
Kwenye ajira mwendazake alivuruga,hivyo hata Samia nae itabidi aende polepole
Ni kweli mwendazake kaacha tatizo kubwa kwenye ajira ambalo hata Rais Samia hatoweza kulimudu lakini kwa ajira kidogo hizi anazozitoa tunaomba asiendelee na ubaguzi wa kutoajiri walimu wenye shahada bali ajira zitolewe kwa uwiano sawa kulingana na nafasi zilizopo pamoja na mahitaji
 
Kwenye ajira mwendazake alivuruga,hivyo hata Samia nae itabidi aende polepole
Hata Kikwete alianza kuajiri Kwa timing. Aliajiri Sana miaka ya 2010 2012 na 2014. Hii ni miaka Kikwete aliajiri zaidi lakini tukumbuke hata Kikwete angeemdelea kuepo Madarakani asingeweza kuendelea kuajiri idadi kubwa ya watu kama unavyofikria. Kwamba graduates wote waajiriwe na serikali
 
Back
Top Bottom