Mudawote
JF-Expert Member
- Jul 10, 2013
- 10,771
- 14,129
GTs,
Hakika ukiyasikia ya miaka hii ya utumishi wa umma na kustaafu utashangaa hivi kwanini watu wanang’ang’ania ofisini baada ya muda wa utumishi kuisha?
Kuna mtumishi mmoja hapa Dar alistaafu kwenye taasisi moja ya umma, akaongezewa mkataba kwa mfululizo miaka miwili, mwaka wa tatu wakamkatalia, ila yeye akalazimishq dereva awe ana mfuata, baadaye dereva akazuiwa na ofisi basi njemba akawa anajiendesha mwenyewe na akajiwekea kiti ofisini. Aliendelea na huo mtindo mpaka akafariki mwezi wa nne mwaka huu baada ya mapumziko ya Pasaka.
Hii inamaanisha nini??
Ninavyoona hakuna mtanzania mwenye cheo anataka kuachia cheo chake:
1. hili linaanzia kwa wanasiasa, hakuna mbunge yupo tayari kustaafu
2. Hakuna mkurugenzi wa shirika lolote la umma yupo tayari kustaafu, yaani atafanya lolote huko aongezewe muda hata miaka miwili
3. Hakuna mkuu wa mkoa, RAS, au yeyote kwenye hizo kada anataka kustaafu, yupo tayari kufanya lolote abaki kwenye nafasi au aongezewe muda
Hivyo namuunga mkono Mh. Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti wa hiyo NGO yake maana ni utamaduni wa walionacho kutaka kuendelea na vyeo, yaani bora auwe mtu kuliko kuachia cheo.
Hakika ukiyasikia ya miaka hii ya utumishi wa umma na kustaafu utashangaa hivi kwanini watu wanang’ang’ania ofisini baada ya muda wa utumishi kuisha?
Kuna mtumishi mmoja hapa Dar alistaafu kwenye taasisi moja ya umma, akaongezewa mkataba kwa mfululizo miaka miwili, mwaka wa tatu wakamkatalia, ila yeye akalazimishq dereva awe ana mfuata, baadaye dereva akazuiwa na ofisi basi njemba akawa anajiendesha mwenyewe na akajiwekea kiti ofisini. Aliendelea na huo mtindo mpaka akafariki mwezi wa nne mwaka huu baada ya mapumziko ya Pasaka.
Hii inamaanisha nini??
Ninavyoona hakuna mtanzania mwenye cheo anataka kuachia cheo chake:
1. hili linaanzia kwa wanasiasa, hakuna mbunge yupo tayari kustaafu
2. Hakuna mkurugenzi wa shirika lolote la umma yupo tayari kustaafu, yaani atafanya lolote huko aongezewe muda hata miaka miwili
3. Hakuna mkuu wa mkoa, RAS, au yeyote kwenye hizo kada anataka kustaafu, yupo tayari kufanya lolote abaki kwenye nafasi au aongezewe muda
Hivyo namuunga mkono Mh. Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti wa hiyo NGO yake maana ni utamaduni wa walionacho kutaka kuendelea na vyeo, yaani bora auwe mtu kuliko kuachia cheo.