Akaanza Kutetemeka Alipomuona

Nadhani alikuwa ana hamu ya Kuwaonesha wengine kuwa naye ana mchumba ambaye wanapeana mapenzi ya aina yote na alishawahadithia upoje so jamaa wanakufahamu kuwa u mhongaji wa hali ya juu...

Kwa hili la kusafiri umbali wote huo yapata km 500 hivi nakupa hongera
 
duh, kazi ipo
punda atakufa ila tutafika tu.
 
Amewambia wewe ndo kaka yake mkubwa, yan ndo wa kwanza nyumbani 'kwenu'! so akawaonesha makea 'yenu' si ulisema kwao wanajiweza,so ndo aliwaonesha 'uzungu' wa hom 'kwenu':lol:
hahahahaha... maneno yko yanaukweli ndani yke.
 
ukiona alama za miguu?uje watu wamesha kanyaga.....lol

Kaka unatisha,si mshabiki sana wa jukwaa hili ila kati mara chache ninazopita post zako huwa zinanipa raha sana..lol,hii nimeipenda,habari ndio hiyo.
 
Hehehehe kwasababu yanaonekana kirahisi. Akiwa na nyumba watu wasiomfahamu hawawezi kujua anayo mpaka awaambie, wakati gari hata machinga naona "dah, yule mshkaji anatembelea tairi aisee." Wabongo kwa sifa hawawezekani!!
sometimes wanasema ashakum si matusi "mshikaji siku hizi anatembelea mata..ko!
 
Sungura, sasa kama humuamini mpenzi wako, nani unataka amuamini....Love is an act of faith.

You must always keep your faith till the end.

Mimi naona kutetemeka kuna sababu nyingi, inawezekana ile ndo mara ya kwanza anakutana na watu wanao mjua na yuko na mwanaume.

Point ingine kama angekuwa hakupendi, angekuja kukushika pale mbele zao time mnaondoka tena kiuno!!

Yule mimi naona anakupenda usisikie maneno ya watu....Wale vijana inawezekana kaenda wambia kuwa huyu ndo future husband wangu ili wasiende mchafulia jina lake...wanawake wengine wanaona mbali dogo.

Wacha shaka shaka, type kama yako ndo mnaishia kukaa maisha yenu bila wanawake wa maana, kwa wasi wasi wenu na ma wivu.
 
ushaliwa wewe.. ''mara mia kuwa na mahusiano na changudoa kuliko mwanafunzi wa chuo anayeishi hostel''
 
ushaliwa wewe.. ''mara mia kuwa na mahusiano na changudoa kuliko mwanafunzi wa chuo anayeishi hostel''

hii nayo mpya tena yaani changu lililokata tamaa na maisha linatafuta watu wa kufa nao ndie awe mpenzi wako kuliko mwanachuo anayeishi hostel oi! kwa hiyo kama wewe umekuwa na mpenzi wako anahitaji kuendelea na masoma hautakubali hilo jambo sio au utataka ahamie day wakati na wewe unaishi Kilimanjaro na chuo kipo Dar!

Kama huna ushauri bora kunyamaza...
Mchizi anaomba Ushauri na sio kukatisha tamaa wengi humu tunasoma jf
 
unakuta mtu kiwanja hana,lakini ana magari mawili ya mkopo..
watu bana lol

Kuna rafiki yangu aliwahi niambia kwa kuniuliza swali "Uliwahi kusikia watu wanamuita baba mwneye gari? Mara nyingi wasema baba mwenye nyumba".
Dada zetu wawe waangalifu na hayo magari watakosa wachumba bure!!!
 
Alikuwa anawamix ila kwa vile yale ma classmate yake matoz au mabishoo ameamua kuwa na wewe ndo maana kakushika kiuno wakati mnaondoka.Machezeaji yanakubaligi kuwa hata kwenye folen elimradi yampate so alienda kumuambia hivi"SI NILIKUAMBIA wakati unanitokea kuwa NINABOI FRND WNG NDO YULE So usilete usumbufu tulia zamu yako tukirudi chuo"
 
Mimi sijaona shida; huyo dada si mzorfu kihivyo ndio maana alitetemeka sijui.

Utani vyuoni na makazini upo kwa sana tu, na kwavile ni mpole ndio maana alishindwa kuihandle hiyo situation.

Unafikiri angeweza kukushika kiunoni kama alikuwa na mtu pale; naamini huwa wanamtania ndio maana akawaoneshea kuwa naye ana mtu.

Nakuonea huruma sana; safari ya mapenzi ni ngumu sana, ukianza kuonesha mistrust kwa kutafuta vijimakosa hamtafika mbali na utajuta pale utakapopata mwanamke kichomi anaweza kuwafool na kuwapanga kama mafiga na huyo mchumba wako uliyemuanza mwenyewe akiolewa na mtu mwingine!

Hakuna kitu kibaya kama kumdoubt mwenzio. Wanasema if u look for mistakes, u will surely find them, kwani kitu kidogo utakimagnify na kukikuza!
 
Kuna rafiki yangu aliwahi niambia kwa kuniuliza swali "Uliwahi kusikia watu wanamuita baba mwneye gari? Mara nyingi wasema baba mwenye nyumba".
Dada zetu wawe waangalifu na hayo magari watakosa wachumba bure!!!

Jamani nyumba ni basic need; na almost everyone has it (iwe ya kupanga, mkopo au kujenga) lkn gari ni kitu kinachorahisisha shughuli. Pia huwezi kuwa umejenga kila mkoa (wanaohama hama), lkn gari waweza move nalo; na mwisho Gari ni cheap kuliko nyumba!

Sasa kwa wadada nyumba yako itamsaidia nini; lkn gari lampeleka salon, kazini, shopping etc.
 
Reactions: SMU
Ila mim nikawa na maswal mengi
1.kwanin akose comfednce alipowaona wale jamaa?
2.kwanin aliporudi alinishika kiuno na sio kawaida yake?
wanajamii hebu nisaidieni

wewe chukua ngoma yako kiujumla achana na fikra hizo kama zipo utaziona huko mbeleni...........
 
Dah, pole mwana. Ila kwa mambo ambayo nimewahi kuyaona tangu niwe na ailiki timamu naweza kwambia POLE, hapo umeliwa.
Wale jamaa anamahusiano nao, na hapo aliwadanganya kuwa wewe ni kaka yake. Watu kama hao they are so techinical, hapo utakuta ana namba nyingine za cm anazotumia tofauti na unazofahamu wewe, so unaweza kaa na cm yake unayoifahamu wewe cku nzima na ucone kitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…