Akiamka usingizini, anachoka kusimama

Wa Mjengoni

JF-Expert Member
Joined
May 4, 2010
Posts
480
Reaction score
128
Wakuu wana wa JF na wenye taaluma ya afya, Salaam!

Nina mwanangu wa kiume wa miaka sita na anasoma shule ambayo humfanya tumwamshe kila siku ya shule saa 11:45 asubuhi.

Akiamka na kusimama kwenye sinki ili kupiga mswaki huwa analalamika miguu inachoka na hudai apige mswaki amekaa.

Swali langu je, huu huwa ni usingizi tu au ugonjwa fulani unajengeka?

Hali hii hutokea asubuhi tu anapotoka usingizini.
 
i think ni usingizi tu huo unamsumbua. jaribu kuwa ..Awe analala mapema zaidi. Na chumba chake kiwe kinapitisha oxygen ya kutosha.(madirisha yenye hewa).Pia kitanda chake kisiwe kinabonyea kupitiliza(kisiwe na magodoro mawili yaliyobebana). kisha ucheki maendeleo
 
Fuata ushauri hapo juu
Halafu hakikisha anakunywa maji mengi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…