Akiba ya damu Tanzania iliyopo ni chupa 375,000, uhitaji ni chupa 550,000 hadi 600,000

Akiba ya damu Tanzania iliyopo ni chupa 375,000, uhitaji ni chupa 550,000 hadi 600,000

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
4dcd3118-17ad-4177-b400-e728f6b1abc0.jpg


Jamii imeshauriwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kuchangia damu kwa lengo la kusaidia jamii yenye uhitaji kwa kuwa kuna upungufu wa damu maeneo mengi yenye uhitaji.

Imeelezwa kuwa uhitaji wa damu uliopo Nchini ni kati ya chupa laki tano na nusu mpaka sita huku akiba iliyopo ni chupa laki tatu na sabini na tano, hii ikiwa ni takwimu zilizofanywa mwaka 2021.

Hayo yamesemwa na wakati wa uchangiaji wa damu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Damu inayofanyika kila mwaka Juni 14.

Afisa Mhamasishaji Jamii Damu Salama Kanda Mashariki, Mariam Juma amesema ni muhimu kwa jamii kujitoa katika kuchangia damu kwani uhitaji bado ni mkubwa.

"Jamii inahitaji kujitolea damu maana wahitaji ni wengi na huwezi jua leo kwa mwenzio kesho kwako," anasema Mariam.

Amewataka wananchi kutokuamini dhana potofu kwamba ukitoa damu ndio chanzo cha kulazimika kutoa damu mara kwa mara.
e75324e3-3431-43d3-815f-06779b3f7023.jpg
"Assembly Insurance imejitolea katika kuhamasisha siku hiyo basi liwe jambo endelevu katika taasisi au makampuni mengine kufanya uhamasishaji wa kuchangia mfuko wa damu salama," alisema Mariam.

Naye Meneja Mkuu wa Assembly Insurance, Tabia Masoud amesema wao wameamua kujitoa kufanya kazi hiyo Juni 17 kutokana na kuona umuhimu wa kuchangia damu inayohitajika.

Alisema wao ni taasisi ya Bima wanazunguka na kuona kwamba uhitaji wa damu na hata kwa wateja wao ni mkubwa hivyo wametumia siku ya leo katika kuchangia damu.
 
Toaaaa weee, haya siku wewe unahitaji
Ndio utajua hujui,
Tutoe kwa huruma tu usisubiri shukrani
 
Kwa matunda yapi wanayokula wananchi mpaka wapate damu ya kutoa?

Watu wamejaa stress za ugumu wa maisha mpk damu zinakaukia mwilini bila chembe ya huruma bado mnataka kuwatoa damu...mmewanyonya kodi haijatosha sasa inafuata kodi ya damu
 
Kuna ujinga na changamoto nyingi saaana tunakutana nazo tukitaka damu wakati tulichangia na kadi tunazo....

Wanaweka pesa mbele kuliko huduma, ni muda sasa na wao waanze kununua damu kwetu
 
Si wachukue kwa lazima kwa wafungwa.
kuna uzi mmoja nilisoma humu kama sikosei walisema kwa wenzetu (mashariki ya mbali) mashoga hawaruhusiwi kuchangia damu (sikufuatilia zaidi kwenye vyanzo vya ziada) hivyo tukija kwenye suala la magerezani hivyo vitendo ni kama dawa ,kwa hiyo kama kuna uhalisia basi na hii pia haitakuwa suluhisho
 
Jamii imeshauriwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kuchangia damu kwa lengo la kusaidia jamii yenye uhitaji kwa kuwa kuna upungufu wa damu maeneo mengi yenye uhitaji.

Imeelezwa kuwa uhitaji wa damu uliopo Nchini ni kati ya chupa laki tano na nusu mpaka sita huku akiba iliyopo ni chupa laki tatu na sabini na tano, hii ikiwa ni takwimu zilizofanywa mwaka 2021.

Hayo yamesemwa na wakati wa uchangiaji wa damu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Damu inayofanyika kila mwaka Juni 14.

Afisa Mhamasishaji Jamii Damu Salama Kanda Mashariki, Mariam Juma amesema ni muhimu kwa jamii kujitoa katika kuchangia damu kwani uhitaji bado ni mkubwa.

"Jamii inahitaji kujitolea damu maana wahitaji ni wengi na huwezi jua leo kwa mwenzio kesho kwako," anasema Mariam.

Amewataka wananchi kutokuamini dhana potofu kwamba ukitoa damu ndio chanzo cha kulazimika kutoa damu mara kwa mara.
"Assembly Insurance imejitolea katika kuhamasisha siku hiyo basi liwe jambo endelevu katika taasisi au makampuni mengine kufanya uhamasishaji wa kuchangia mfuko wa damu salama," alisema Mariam.

Naye Meneja Mkuu wa Assembly Insurance, Tabia Masoud amesema wao wameamua kujitoa kufanya kazi hiyo Juni 17 kutokana na kuona umuhimu wa kuchangia damu inayohitajika.

Alisema wao ni taasisi ya Bima wanazunguka na kuona kwamba uhitaji wa damu na hata kwa wateja wao ni mkubwa hivyo wametumia siku ya leo katika kuchangia damu.
Kwa niliyoyaona kwenye vitengo vya damu salama, siwezi kuchangia damu mimi, damu zinauzwa kama nyanya
 
Back
Top Bottom