Akili kubwa inahitajika pia ili kucheza soccer kikamilifu

Akili kubwa inahitajika pia ili kucheza soccer kikamilifu

Umkonto

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2018
Posts
2,652
Reaction score
4,593
Mtazamo wangu baada ya kuwatazama Barcelona dhidi ya Madrid, nimegundua kwamba, pamoja na kufanya mazoezi ili mchezaji aweze kucheza soccer kikamilifu na kung'ara anatakiwa pia awe na akili kubwa.

Akili kubwa itamfanya mchezaji kufuata maelekezo ya kocha akiwa kwenye mechi na pia itamuwezesha kutafsiri matukio kwa haraka mfano kupiga chenga, kutoa pasi nk. Hapa ndipo utasiki kocha anasema hawa wachezaji wanafundishika, lakini wale hawafundishiki.

Kwa mfano, Barcelona ina wachezaji vijana wenye akili kubwa ndiyo maana waliweza kuwa-win wachezaji wa Madrid.

Mfano mwingine, wale mabeki wa Barcelona walifanikiwa kucheza offside triki na wachezaji wa Madrid wakaotea zaidi ya mara tano. Hii ni akili kubwa kwamba wanakuwa wapo mchezoni muda wote na kufuata maelekezo ya kocha. Kungekuwa na akili ndogo kwenye ile beki ya Barcelona lazima mmojawapo angechomesha.

Mchezaji mwenye akili ndogo anashindwa kutafsiri matukio kwa haraka akiwa uwanjani. Sehemu ya kutoa pasi ili mwingine afunge, hafanyi hivyo bali analazimisha afunge yeye na anakosa.

Hivyo, tujitahidi kuwajengea watoto mazingira ya kuwa na akili kubwa kwa sababu hata katika vipaji akili kubwa inahitajika pia mfano katika soccer, utunzi wa muziki nk.

Akili kubwa ya mtoto itaanza kujengwa tangu siku ya kutungwa mimba ambapo mama mjamzito anatakiwa afuate ushauri wa daktari katika masuala ya lishe. Pia. mtoto akizaliwa anatakiwa apewe lishe bora
 
Mtazamo wangu baada ya kuwatazama Barcelona dhidi ya Madrid, nimegundua kwamba, pamoja na kufanya mazoezi ili mchezaji aweze kucheza soccer kikamilifu na kung'ara anatakiwa pia awe na akili kubwa.

Akili kubwa itamfanya mchezaji kufuata maelekezo ya kocha akiwa kwenye mechi na pia itamuwezesha kutafsiri matukio kwa haraka mfano kupiga chenga, kutoa pasi nk. Hapa ndipo utasiki kocha anasema hawa wachezaji wanafundishika, lakini wale hawafundishiki.

Kwa mfano, Barcelona ina wachezaji vijana wenye akili kubwa ndiyo maana waliweza kuwa-win wachezaji wa Madrid.

Mfano mwingine, wale mabeki wa Barcelona walifanikiwa kucheza offside triki na wachezaji wa Madrid wakaotea zaidi ya mara tano. Hii ni akili kubwa kwamba wanakuwa wapo mchezoni muda wote na kufuata maelekezo ya kocha. Kungekuwa na akili ndogo kwenye ile beki ya Barcelona lazima mmojawapo angechomesha.

Mchezaji mwenye akili ndogo anashindwa kutafsiri matukio kwa haraka akiwa uwanjani. Sehemu ya kutoa pasi ili mwingine afunge, hafanyi hivyo bali analazimisha afunge yeye na anakosa.

Hivyo, tujitahidi kuwajengea watoto mazingira ya kuwa na akili kubwa kwa sababu hata katika vipaji akili kubwa inahitajika pia mfano katika soccer, utunzi wa muziki nk.

Akili kubwa ya mtoto itaanza kujengwa tangu siku ya kutungwa mimba ambapo mama mjamzito anatakiwa afuate ushauri wa daktari katika masuala ya lishe. Pia. mtoto akizaliwa anatakiwa apewe lishe bora
Unaisema Mikia FC kijanja.
 
KwAnza nikupongeze !huwa unatazama mpila kwenye jicho la mwewe ni watu wachache sana wanafanyA kama wewe wengi wanaendekeza Ushabiki wa timu ili swala ndo linatutesa kwenye timu ya Taifa tuna kundi la wachezaji ambao kichwani hamna kitu angalia tukio la goli ambalo tulifungwa na Congo mchezaji ameupoteza mpila anamkimbiza mchezaji hadi anatoa pasi hivi kwA nini asifanye tecnic faulo ili mjipange unagundua hatuko sawa kichwani kuna haja kuangalia wachezaji jinsi wAnavyotafsiri matukio uwanjani ndo iwe kigezo cha kuitwa timu ya Taifa.
 
Back
Top Bottom