Akili kubwa rais Uhuru aalikwa tena kwenye kikao cha wachache duniani G7

Akili kubwa rais Uhuru aalikwa tena kwenye kikao cha wachache duniani G7

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Kwa mara ya pili, rais Uhuru amealikwa kwenye kikao cha G7 ambacho ni mkusanyiko wa mataifa machache yenye ushawishi mkubwa duniani, na kualikwa humo uhutubie na kueleza lazima uwe umekaguliwa uwezo wako, michango yako na ushawishi wako kwenye ukanda unaotokea.
Ikumbukwe Kenya mwaka jana ilikua mwenyeji wa wageni 18,000 waliotokea kwenye mataifa 170 duniani ambao walikuja kuhudhuria kikao cha kwanza kuwahi kutokea duniani cha kujadili uchumi wa bahari, maziwa, mito na maeneo yote yenye maji (blue economy).

Huo hapo ni mfano mmoja tu wa jinsi gani Kenya chini ya uongozi wa rais Uhuru, imechukua nafasi ya kuiongoza Afrika kwenye kila hali, na zaidi ya yote Kenya leo hii ndio inaongoza kiuchumi, kijeshi, kielimu ukanda wote huu, imeipiku hata Ethiopia, yaani kote hadi hata Afrika ya kati.

Ni fahari kwa rais wetu kualikwa kwenye vikao kama hivi, maana kwa wanaoelewa siasa za kimataifa na diplomasia wanajua ni jinsi gani taifa hufaidi linapopigiwa debe kihivi, na humo kama ilivyo kawaida yake rais, atakua na vikao vya faraghani pembeni na kila rais wa hayo mataifa ambayo ndio huongoza dunia na kuelekeza sera.

Hii hapa video anavyotema yai kuhusu sera za kutambua mchango wa wanawake kwenye uongozi....hamna cha zezeze
 
we mkikiyu, kwanza tupe faida za kiuchumi ambazo kenya imefaidika baada ya uhuru kenyatta kuhudhurua G7 summit ya 2018.
 
Kwa mara ya pili, rais Uhuru amealikwa kwenye kikao cha G7 ambacho ni mkusanyiko wa mataifa machache yenye ushawishi mkubwa duniani, na kualikwa humo uhutubie na kueleza lazima uwe umekaguliwa uwezo wako, michango yako na ushawishi wako kwenye ukanda unaotokea.
Ikumbukwe Kenya mwaka jana ilikua mwenyeji wa wageni 18,000 waliotokea kwenye mataifa 170 duniani ambao walikuja kuhudhuria kikao cha kwanza kuwahi kutokea duniani cha kujadili uchumi wa bahari, maziwa, mito na maeneo yote yenye maji (blue economy).

Huo hapo ni mfano mmoja tu wa jinsi gani Kenya chini ya uongozi wa rais Uhuru, imechukua nafasi ya kuiongoza Afrika kwenye kila hali, na zaidi ya yote Kenya leo hii ndio inaongoza kiuchumi, kijeshi, kielimu ukanda wote huu, imeipiku hata Ethiopia, yaani kote hadi hata Afrika ya kati.

Ni fahari kwa rais wetu kualikwa kwenye vikao kama hivi, maana kwa wanaoelewa siasa za kimataifa na diplomasia wanajua ni jinsi gani taifa hufaidi linapopigiwa debe kihivi, na humo kama ilivyo kawaida yake rais, atakua na vikao vya faraghani pembeni na kila rais wa hayo mataifa ambayo ndio huongoza dunia na kuelekeza sera.

Hii hapa video anavyotema yai kuhusu sera za kutambua mchango wa wanawake kwenye uongozi....hamna cha zezeze
Sisi hayo yote tulishayafanya na kikwete awamu iliyopita nyie mnafanya sasa mbona mmechelewa Sana?

Sent from my Desire12 using JamiiForums mobile app
 
Ni jambo zuri kwa Uhuru na Wakenya kupata recognition hiyo. Ila you also need to take into consideration kwamba hawa jamaa huwa na matakwa yao ambayo wanahitaji kuyatimiza kupitia Uhuru, msibweteke kwamba mnapendwa sana.
Historia ni shahidi kuna wakati fulani M7 aliwahi kuwa mtoto mzuri kwa Viranja hao wa dunia
Ni urafiki wa mashaka
 
we mkikiyu, kwanza tupe faida za kiuchumi ambazo kenya imefaidika baada ya uhuru kenyatta kuhudhurua G7 summit ya 2018.

Ahaaa haaa haaa
Nashangaa mleta uzi anashangilia kualikwa kwenye g7 utafikiri ni jambo so special. Utadhani uhuru ni wa kwanza kualikwa.
Sasa ninachoshangaa ni KWAMBA NAFASI ya Kenya kwenye ukanda huu na Afrika kwa ujumla HAMNA mtu ambaye anaweza tabanaisha kianuwai. Ni nchi ambayo mataifa ya magharibi yaniona kama ni jimbo lao la ughaibuni (over seas province) ambalo halina mafungamano yenye ushawishi kwa majirani wanalolizunguka. Binafsi naona Kenya inafanywa kama summer house for westerners. Ambayo wanakuja kujiburudisha au mapumziko baada ya kuwa na kipindi kirefu cha kazi. Nasema hivyo kwa sababu sijaona hata siku moja resolution ikapitishwa Kenya ili kusudi ienezwe Afrika Mashariki au Afrika yote. Wengi wanajua, Kenya haiwezi kutumika kwa ushawishi wa bara la Afrika. Maana kila nchi Afrika inaichukulia Kenya kwa tahadhari kubwa SANA kwa sifa zake. Rejea kilichompata mfalme wa UARABUNI.
 
Ni jambo zuri kwa Uhuru na Wakenya kupata recognition hiyo. Ila you also need to take into consideration kwamba hawa jamaa huwa na matakwa yao ambayo wanahitaji kuyatimiza kupitia Uhuru, msibweteke kwamba mnapendwa sana.
Historia ni shahidi kuna wakati fulani M7 aliwahi kuwa mtoto mzuri kwa Viranja hao wa dunia
Ni urafiki wa mashaka

Haya mambo hatujaanza kuyafanya leo, na huwa hatufanyi chochote bila malengo, ndio maana nikasema inahitaji mtu mwenye uelewa wa masuala ya kimataifa na diplomasia kufahamu umuhimu ya yote haya.
 
Back
Top Bottom