uvugizi
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 1,278
- 956
TAFAKURI …. AKILI SI YA KUHIFADHI WAZO, BALI YA KUBUNI WAZO.
Unatoka kazini ukiwa na mambo mengi kichwani . Ghafla unakumbuka unatakiwa kupitia kitu muhimu nyumbani . lakini unasema nikifika tu nyumbani nitamtuma mtoto akanunue .
Lakini unapofika nyumbani unakumbana na vitu vingine tena vingi . Aidha kuna taarifa na majukumu ambayo yanakutoa katika mstari . Hadi kesho au baada ya muda Fulani ndipo unaanza kukumbuka tena . Sababu kubwa ni kutopangilia ipasavyo . HUNA UTARATIBU NA RATIBA YA MAMBO YAKO . Wewe unataka kukumbuka kila kitu . Jambo hili si la kawaida na haliwezekani . kumbuka vitu kwa vipaumbele vyake na utaratibu uliouweka .
Kazi ya akili yako ni kufikiri , kufanya maaumuzi na kutatua matatizo . hauendi zaidi ya hapo na si kuhifadhi tu . Akili imetengenezwa kuleta ubunifu . ndiyo maana albert Einstein alikuwa hafahamu namba yake ya simu . Alipoulizwa yeye alisema , mimi ninayo katika phonebook , ni swala la kungalia na kupiga . Kwani akili yangu ni ya kubuni na si kuhifadhi . Mind is not for storing idea ,but is for creating ideas.
Tunaishi katika dunia ambayo vitu vingi sana vinaingilia maisha yetu na mipango Yetu . Kuna matumizi ya simu , tv , nk . Hata tunafika mahli tunakosa control ya maisha yetu wenyewe .
Hapa ndipo unapopata sheria ya Bwana david allen,( GTD ) Getting things done . Huu ni utaratibu wa mawazo namna ya kupangilia mawazo yako ili upate uzalishaji chanya katika mradi wako . Fanyia kazi jambo kwa mujibu wa uwezekano wake , na kama ulivyopanga . Akili yako ni kwa ajili ya kukamatia mawazo( to capture a thougth) , si kuyashikilia( not To hold them). Akimaanisha ukishikilia mambo lazima yakuponyoke .
Kama akili yako ikiwa inapanga mambo kwa mpangilio sawia utapata matokeo chanya . Akili yako inakusaidia kuweka record na utaratibu wa majukumu , kipi kianze na kipi kifuate . SI KUHIFADHI TU .
Katika utaratibu huu wa GTD Kuna hatua tano za kufanya mambo yatokee .
. 1 - Capture 2 - Clarify 3 - Organize 4 - Reflect 5 - Engage
Kitu cha kwanza ni kukamata kwanza jambo lolote aidha inaweza kuwa ni taarifa . Unatakiwa kukamata na si kuingiza tu katika akili yako bali kukusanya kwa ajili ya hatua ya pili . taarifa zozote zinazotoka kwa watu zinaweza kuwa ni wazo la kuzaa shughuli kwako . ZIKAMATE KWANZA ( CAPTURE THEM) . Hapa ndiyo wengi tunakamatwa , kwani kukamata tunakamata . Tunafanyia nini , ndiyo kazi ilipo.
Baada ya hatua hiyo unatakiwa uanze sasa kujiuliza je inawezekana ( is it actionable ) . Jibu katika taarifa yote hiyo itakuwa YES or NO . hapa kuna mchujo . Hata jibu likiwa ni ndiyo ,lazima uangalie itachukua muda gani kutenda . Kama itakuwa ni hapana , lazima utenge na kuliweka kwa angalizo la ziada , unaliacha kwa muda au kulitupa kabisa . Utafanya hivi kwa kila hatua za taarifa ulizo nazo .
Baada ya kuchakata ni wakati wa kupangilia . Hapa tunapata mpangilio katika jambo husika , muda na maudhui yake . Vitu vya aina moja lazima uviunganishe pamoja , usivitenge . vile vinavyohitaji muda maalum navyo lazima viungane pamoja . kuna vingine aidha vinahitaji aidha kufanywa na mtu mwingine hapa ndiyo mahali pa kuamua .
Swala kubwa hapa ni namna ya kuchukua zile hatua , kipi kianze na kipi kisianze . Mimi natumia one note kwa computer na keep note kwa simu . Inanisaidia sana principle hii .sina takataka kichwani na mlundikano wa majukumu kichwani .
Baada ya hapo , fanya rejea ya vile ulivyopanga . kama ulikuwa unajua kuna sehemu hukufanya sawa ni wakati sasa wa kurudia , unaweza kufanya kila baada ya muda Fulani . Kama una mipango mikubwa jiwekee utaratibu wa kurejea mambo yako kila baada ya mwezi .
Baada ya hapo unaenda kufanya .kama taarifa unazo nyingi inabidi na akili inatakiwa kuwa katika hali ya UKUU . Yaani akili kubwa tatizo kubwa akili ndogo akili ndogo katika kutatua . kwa kufanya hivyo kila kitu kitakuwa kimekaa mahali pake na hakuna cha kukuponyoka tena , na hutakuwa mtu wa kupoteza muda . Mambo mengi yatapata kufanyika .
Watu wengi hapo wanapanga , Lakini kwa mkusanyiko wa taarifa nyingi kichwani . wanajikuta kwa kuwa hawaweki mtiririko huu wanakwama . Wanahudhuria semina nyingi na hakuna matokeo .
Biblia inasema .Mithali 21:5 ,.’’’ Mawazo ya wenye bidii huelekea utajiri tu ; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji .’’’’’( ESV BIBLE) . The plans of the diligent lead surely to abundance, but everyone who is hasty comes only to poverty.
TAFAAKRI NAMI
Unatoka kazini ukiwa na mambo mengi kichwani . Ghafla unakumbuka unatakiwa kupitia kitu muhimu nyumbani . lakini unasema nikifika tu nyumbani nitamtuma mtoto akanunue .
Lakini unapofika nyumbani unakumbana na vitu vingine tena vingi . Aidha kuna taarifa na majukumu ambayo yanakutoa katika mstari . Hadi kesho au baada ya muda Fulani ndipo unaanza kukumbuka tena . Sababu kubwa ni kutopangilia ipasavyo . HUNA UTARATIBU NA RATIBA YA MAMBO YAKO . Wewe unataka kukumbuka kila kitu . Jambo hili si la kawaida na haliwezekani . kumbuka vitu kwa vipaumbele vyake na utaratibu uliouweka .
Kazi ya akili yako ni kufikiri , kufanya maaumuzi na kutatua matatizo . hauendi zaidi ya hapo na si kuhifadhi tu . Akili imetengenezwa kuleta ubunifu . ndiyo maana albert Einstein alikuwa hafahamu namba yake ya simu . Alipoulizwa yeye alisema , mimi ninayo katika phonebook , ni swala la kungalia na kupiga . Kwani akili yangu ni ya kubuni na si kuhifadhi . Mind is not for storing idea ,but is for creating ideas.
Tunaishi katika dunia ambayo vitu vingi sana vinaingilia maisha yetu na mipango Yetu . Kuna matumizi ya simu , tv , nk . Hata tunafika mahli tunakosa control ya maisha yetu wenyewe .
Hapa ndipo unapopata sheria ya Bwana david allen,( GTD ) Getting things done . Huu ni utaratibu wa mawazo namna ya kupangilia mawazo yako ili upate uzalishaji chanya katika mradi wako . Fanyia kazi jambo kwa mujibu wa uwezekano wake , na kama ulivyopanga . Akili yako ni kwa ajili ya kukamatia mawazo( to capture a thougth) , si kuyashikilia( not To hold them). Akimaanisha ukishikilia mambo lazima yakuponyoke .
Kama akili yako ikiwa inapanga mambo kwa mpangilio sawia utapata matokeo chanya . Akili yako inakusaidia kuweka record na utaratibu wa majukumu , kipi kianze na kipi kifuate . SI KUHIFADHI TU .
Katika utaratibu huu wa GTD Kuna hatua tano za kufanya mambo yatokee .
. 1 - Capture 2 - Clarify 3 - Organize 4 - Reflect 5 - Engage
Kitu cha kwanza ni kukamata kwanza jambo lolote aidha inaweza kuwa ni taarifa . Unatakiwa kukamata na si kuingiza tu katika akili yako bali kukusanya kwa ajili ya hatua ya pili . taarifa zozote zinazotoka kwa watu zinaweza kuwa ni wazo la kuzaa shughuli kwako . ZIKAMATE KWANZA ( CAPTURE THEM) . Hapa ndiyo wengi tunakamatwa , kwani kukamata tunakamata . Tunafanyia nini , ndiyo kazi ilipo.
Baada ya hatua hiyo unatakiwa uanze sasa kujiuliza je inawezekana ( is it actionable ) . Jibu katika taarifa yote hiyo itakuwa YES or NO . hapa kuna mchujo . Hata jibu likiwa ni ndiyo ,lazima uangalie itachukua muda gani kutenda . Kama itakuwa ni hapana , lazima utenge na kuliweka kwa angalizo la ziada , unaliacha kwa muda au kulitupa kabisa . Utafanya hivi kwa kila hatua za taarifa ulizo nazo .
Baada ya kuchakata ni wakati wa kupangilia . Hapa tunapata mpangilio katika jambo husika , muda na maudhui yake . Vitu vya aina moja lazima uviunganishe pamoja , usivitenge . vile vinavyohitaji muda maalum navyo lazima viungane pamoja . kuna vingine aidha vinahitaji aidha kufanywa na mtu mwingine hapa ndiyo mahali pa kuamua .
Swala kubwa hapa ni namna ya kuchukua zile hatua , kipi kianze na kipi kisianze . Mimi natumia one note kwa computer na keep note kwa simu . Inanisaidia sana principle hii .sina takataka kichwani na mlundikano wa majukumu kichwani .
Baada ya hapo , fanya rejea ya vile ulivyopanga . kama ulikuwa unajua kuna sehemu hukufanya sawa ni wakati sasa wa kurudia , unaweza kufanya kila baada ya muda Fulani . Kama una mipango mikubwa jiwekee utaratibu wa kurejea mambo yako kila baada ya mwezi .
Baada ya hapo unaenda kufanya .kama taarifa unazo nyingi inabidi na akili inatakiwa kuwa katika hali ya UKUU . Yaani akili kubwa tatizo kubwa akili ndogo akili ndogo katika kutatua . kwa kufanya hivyo kila kitu kitakuwa kimekaa mahali pake na hakuna cha kukuponyoka tena , na hutakuwa mtu wa kupoteza muda . Mambo mengi yatapata kufanyika .
Watu wengi hapo wanapanga , Lakini kwa mkusanyiko wa taarifa nyingi kichwani . wanajikuta kwa kuwa hawaweki mtiririko huu wanakwama . Wanahudhuria semina nyingi na hakuna matokeo .
Biblia inasema .Mithali 21:5 ,.’’’ Mawazo ya wenye bidii huelekea utajiri tu ; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji .’’’’’( ESV BIBLE) . The plans of the diligent lead surely to abundance, but everyone who is hasty comes only to poverty.
TAFAAKRI NAMI