Ndugu yangu klorokwini, ndege ulojipatia,
Usimtupe shimoni, ndege asije kulia,
Ahsante kwa shukurani, sisi ni ndugu sawia,
Ila usije sahau, zuri kula na nduguyo.
Ndege huyo maridadi, kama ulivomsifu,
Asipigwe na baridi, wala kung'atwa siafu,
Kumtuna huna budi, Asije kupata ufu,
Msiba wake mkubwa, kufiwa na ndege wako.
Kaa naye kwa makini, haja kumtimizia,
Asijeshinda bandani, njaa kumuumizia,
Chakula alie ndani, siyo chini kumwekea,
Ndege akinona nona, ndo utamu utapata.
Hii ndo JF bwana!
...........ya kuto kula kibua!!!Umeonae....twaweza pata sababu hapa....
Umeonae....twaweza pata sababu hapa....
Babu uko vizuri aseee.....
Ndugu yangu klorokwini, ndege ulojipatia,
Usimtupe shimoni, ndege asije kulia,
Ahsante kwa shukurani, sisi ni ndugu sawia,
Ila usije sahau, zuri kula na nduguyo.
Ndege huyo maridadi, kama ulivomsifu,
Asipigwe na baridi, wala kung'atwa siafu,
Kumtuna huna budi, Asije kupata ufu,
Msiba wake mkubwa, kufiwa na ndege wako.
Kaa naye kwa makini, haja kumtimizia,
Asijeshinda bandani, njaa kumuumizia,
Chakula alie ndani, siyo chini kumwekea,
Ndege akinona nona, ndo utamu utapata.
Nilikuwa ninawaza, kalamu nisiishike,
Nikae kwenye baraza, moja mbili nisishike,
Maguluma kanikwaza, ngoja mic niishike
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Ndio hapa mnambie, kwa nini wampakata?
Tena nidadavulie, ni raha gani wapata?
Ili nami nikimbie, nimsake huyo bata,
Nawauliza malenga, bata anapakatwaje?
Hommie wangu 'Sipirini, hata nawe Klorokwini,
Mwanakijiji Amani, Magulumangu mwiteni,
Aje hapa barazani, aujibu mtihani,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
'Mesikia nimeona, bata yake kuharisha,
Wala sio kunong'ona, hilo usije kubisha
Kumpakata mi naona, hilo jambo la kutisha,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Domo lake lachokoa, vinyesi na konokono,
Alacho ndio atoa, kwani nimpe mkono?
Usije kunizodoa, haya yangu ni maono,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Na Kaizer K. Kaizer (Sauti ya watu)
kuna zawadi yako hapa.
yote nimeyakubali, mistari imetulia
lakini kuna mahali, naomba kukubishia
naomba niwe katili, udugu ulogusia
ndege si wa wawili, hilo wazi nakwambia
kizuri ule na nduguyo, msemo hauko sawia
kheri niitwe mchoyo, kuliko ndege kushea
ndege huyu si kimeo, kila mti kurukia
ana kijumba cha mbao, fensi nimemtilia.
tena natangaza wazi, msije mkaribia
nitatia mtu kitanzi , ndege kimsogelea
hatari ya ovadozi ,klorokwini mwaijua
ndege wangu si ulanzi, kila mtu kujinywea.
hehehe hapa hamna kizuri kula na nduguyo wala babuyo. tutashare sredi za JF tu lakini haka kandege hamna kabisa yaani. tafteni bata la magulumangu mkashee.
Klorokwini, AmaniGK, Magulumangu, Asprin......et al....I will BE BACK....U r hilarious
Halafu Mwanakijiji ako wapi?
hahahahahahaaaaaa
Kizuri wakatalia
Tena wanipotezea,
Hutaki tena kushea,
Hata kama namezea.
Ndege hutaki kushea,
Manati nilikupea,
Ndege ukamuwindia,
Kisha ukamchukua.
Nduguyo wanikimbia,
Kisa ndege kanogea,
Yani wanipotezea,
Kisa ndege kakolea?
Hebu badili nia,
Undugu vema kushea,
Mapatano kolezea
Kisha sote twalea.
kuna vingi vya kushea
visokuwa na hatia
ndege wapo mia mia
aspirin bana tulia
ndege wangu kimchukua
aweza akakimbia
akajenga mazowea
na kwako akahamia
ndege si wa muamana
hawana hawa dhamana
tam tam akiona
atatoroka mchana
mjadala hapa hapana
lete vyengine vina
kwa ndege kuazimana
suala hili hakuna
ndege wangu sio bundi
kuruka ruka hapendi
ndege huyu si wa lindi
na kwengineko haendi.
Haikuwa yangu nia,
Ndege kumng'ang'ania,
Nakutaka kuridhia,
Kamwe sitambugia.
Hakika nitamtunza,
hataliwa na mafunza,
Na mengi atajifunza
Hatayapata mauza.
Kwako akisharejea,
Uzoefu kapatia,
Wewe unajimegea,
Kwa raha pia madaha
Ndugu yangu klorokwini
Mimi nduguyo asprini,
Tuko pamoja kundini,
Undugu mpaka damuni.
Wa kijiji kakimbia,
Na ndege anayelia,
Tumbo limemvimbia
Kibudu amejilia.
Kurudi aogopea,
watu watamchekea,
bundi alijipatia,
Ndege alimdhania.
Mwanakijiji uko wapi ?
Akilia sana, karibu kutunguliwa...!
Ha ha ha lol wewe bwanaaspirin ameshajibu hapo juu lol , dah! aspirin bana