Akina Mzee Ndolanga na familia ya mpira

Akina Mzee Ndolanga na familia ya mpira

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Tulimuondoa Muhidini Ndolanga na Rage kwenye mpira kwakuwa mambo ya mpira yalikuwa hayaendi vizuri nchini. Tulidhani sababu ni kwasababu akina Ndolanga na wenzake hawatoki kwenye familia ya mpira wa miguu hivyo hawajui kuongoza mpira. Hivyo watanzania tukaaminishwa kuwa tukiwaweka viongozi waliowahi kuucheza au kuuongoza mpira mambo yetu ya soka yatakwenda vizuri na makombe tutapata.

Tangu waondoke akina Ndolanga na wenzake na kuwakaribisha "football family" hali yetu imebaki ileile au heri ya akina Ndolanga. Akina Mzee Tenga, Malinzi na sasa Karia mambo yetu ni yaleyale tu ya kichwa cha mwenda wazimu.

Kuna haja ya kuwaomba radhi akina Ndolanga na Rage kwanza kwa kejeli tulizowapa kabla ya kutafuta chanzo halisi cha kuboronga kwetu kwenye mpira.
 
Muhidin Ahmad Ndolanga alikuwa Kiongzo Mzuri sana Tatizo Mfumo wa Dola ulikuwa haumtaki

Waziri wa Michezo wakati huo Juma Othman Kapuya alikuwa anamhujumu sana

Mwenyekt wa BMT wakati huo X Afande Said Hamad Elmaamry nae alikuwa hamtaki
 
Muhidin Ahmad Ndolanga alikuwa Kiongzo Mzuri sana Tatizo Mfumo wa Dola ulikuwa haumtaki

Waziri wa Michezo wakati huo Juma Othman Kapuya alikuwa anamhujumu sana

Mwenyekt wa BMT wakati huo X Afande Said Hamad Elmaamry nae alikuwa hamtaki
Tulidhani Tenga atakuwa mwarubaini wa mpira, ona sasa Karia!!! alama 1 tu CECAFA challenge.
 
Ndolanga na mwenzie Aden Rage ndio waasisi wa sheria no 18 ya FIFA timu ya nyumbani lazima ishinde sheria hii ndiyo iliyoangusha mpira wetu
 
Ndolanga na mwenzie Aden Rage ndio waasisi wa sheria no 18 ya FIFA timu ya nyumbani lazima ishinde sheria hii ndiyo iliyoangusha mpira wetu
 
Tulimuondoa Muhidini Ndolanga na Rage kwenye mpira kwakuwa mambo ya mpira yalikuwa hayaendi vizuri nchini. Tulidhani sababu ni kwasababu akina Ndolanga na wenzake hawatoki kwenye familia ya mpira wa miguu hivyo hawajui kuongoza mpira. Hivyo watanzania tukaaminishwa kuwa tukiwaweka viongozi waliowahi kuucheza au kuuongoza mpira mambo yetu ya soka yatakwenda vizuri na makombe tutapata.

Tangu waondoke akina Ndolanga na wenzake na kuwakaribisha "football family" hali yetu imebaki ileile au heri ya akina Ndolanga. Akina Mzee Tenga, Malinzi na sasa Karia mambo yetu ni yaleyale tu ya kichwa cha mwenda wazimu.

Kuna haja ya kuwaomba radhi akina Ndolanga na Rage kwanza kwa kejeli tulizowapa kabla ya kutafuta chanzo halisi cha kuboronga kwetu kwenye mpira.

Labda useme Ndolanga, kama kweli hayo ndiyo yalikuwa mawazo yaani mlimchukulia Rage siyo mtu wa mpira wakati historia yake kimpira haina tofauti na Tenga, ndiyo chanzo cha makosa.

Kwa maneno mengine hatuwezi kuepuka mtizamo wa kiujumla. TFF ni chama. Kinachojenga uwezo wa wachezaji ni mfumo wa maendeleo wa mchezo ambayo kwa tz naona vyanzo vitatu: shule, mtaani, vilabu vya soka. Tofauti ya mchango wa hizo vyanzo na mazingira wezeshi ya serikali(kupitia baraza la michezo) na TFF nayo yana mchango.

Tuwe wakweli katika vyanzo vya wachezaji vyote na wawezeshaji hao hapo juu tatizo liko wapi? Lazima tafiti za maana na za kisayansi zifanyike na majibu yafanyiwe kazi, vinginevyo tutabaki tunalia kumuomba Raisi Mstaafu Mwinyi afute usemi wa kichwa cha mwendawazimu.
 
Labda useme Ndolanga, kama kweli hayo ndiyo yalikuwa mawazo yaani mlimchukulia Rage siyo mtu wa mpira wakati historia yake kimpira haina tofauti na Tenga, ndiyo chanzo cha makosa.

Kwa maneno mengine hatuwezi kuepuka mtizamo wa kiujumla. TFF ni chama. Kinachojenga uwezo wa wachezaji ni mfumo wa maendeleo wa mchezo ambayo kwa tz naona vyanzo vitatu: shule, mtaani, vilabu vya soka. Tofauti ya mchango wa hizo vyanzo na mazingira wezeshi ya serikali(kupitia baraza la michezo) na TFF nayo yana mchango.

Tuwe wakweli katika vyanzo vya wachezaji vyote na wawezeshaji hao hapo juu tatizo liko wapi? Lazima tafiti za maana na za kisayansi zifanyike na majibu yafanyiwe kazi, vinginevyo tutabaki tunalia kumuomba Raisi Mstaafu Mwinyi afute usemi wa kichwa cha mwendawazimu.
Hapo umenena, lakini kuna kasumba ya kisakatonge ya wakati wa uchaguzi TFF ukifika eti watu waliowahi kucheza au kuo goza mpira ndio wachaguliwe TFF na kusahau kuwa uongozi ni zaidi ya kucheza mpira utotoni.
 
Back
Top Bottom