Akiwa msibani, Kamishna wa TRA aahidi kushirikiana na Polisi katika kukamata wakwepa kodi kuanzia sasa

Akiwa msibani, Kamishna wa TRA aahidi kushirikiana na Polisi katika kukamata wakwepa kodi kuanzia sasa

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Sakata la yule Afisa wa TRA aliyefariki limeendelea kuchukua sura mpya.

===================

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Mwenda, ametangaza kuwa oparesheni zote za kitengo cha Fast cha kudhibiti wakwepa kodi zitafanywa kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kuanzia sasa.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya tukio la kusikitisha la kuuawa kwa dereva wa TRA, Amani Kamguna Simbayao, aliyeshambuliwa na wananchi wakati wa utekelezaji wa majukumu yake katika eneo la Tegeta Nyuki, Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu, Bw. Mwenda amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuwakamata washukiwa wa tukio hilo na amesisitiza kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Amefafanua kuwa gari lililokuwa likifuatiliwa na marehemu na wenzake liliingizwa nchini kwa njia za magendo bila kulipa kodi, na kodi hiyo ingeweza kuchangia maendeleo ya taifa.

"Ningependa mjue kwamba kazi wanayofanya watumishi wa TRA ni kwa niaba ya Watanzania wote. Marehemu Amani alijitahidi kuhakikisha kodi inakusanywa ili kuboresha maisha ya wananchi. Hatustahili kuona wafanyakazi wa TRA wakifanyiwa matendo kama haya. Wanastahili heshima kwa kazi yao kubwa," amesema Bw. Mwenda.

Bw. Mwenda aliendelea kusema kuwa TRA itaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kodi na mamlaka ya watumishi wake katika kutekeleza majukumu yao.

TRA .png


"Kwetu sisi, Marehemu ni shujaa wa taifa. Alifariki akiwa kazini, akilinda mali ya serikali kwa uadilifu na uzalendo mkubwa. Hatutamsahau kwa mchango wake mkubwa," amesema Bw. Mwenda.

Akizungumzia familia ya marehemu, Bw. Mwenda ameahidi msaada wa kiuchumi na kijamii.

Source: Jambo TV
 
Serikali inafuatilia gari lenye makosa ya kikodi, kwanini msimfuate mpaka anapopaki mtu mkaipiga pin gari mkaita tow truck (breakdown) mkaivuta gari mpaka ofisini kwenu mwenye gari ataamua mwenyewe kujakumaliza msala wake au gari muipige mnada, kuliko kumsimamisha mtu barabarani na kumtaka ashuke tena wakati giza limeshaingia huko ni kutafutia watu lawama.
 
CCM inaharibia sana taasisi nyingine hapa nchini. Saizi hata Hawa maafisa mikopo wa Taasisi zote za fedha zenye kutoa mikopo wawe makini. Unaenda kudai defaulter huko unapigiwa kelele wewe ni mtejaji......kwisha habari Yako....
 
Ni wajibu wa vyombo vya umma kushughulikia kila aina ya uhalifu na jinai. Ila hakuna kitu kizuri kinachofanyika bila kufuata sheria na taratibu. Pamoja na nia njema, kama sheria za taratibu hazifuatwi, tutegemee matatizo mengi kutokea kwa pande zote.
Nampongeza Mkubwa wa TRA kutambua kwamba kukamata wahalifu sio kazi yao kisheria. Ndio maana tuna jeshi la polisi. Jeshi la polisi lina vitendea kazi na maarifa ya kushughulika na uhalifu na jinai.
 
Wakuu,

Sakata la yule Afisa wa TRA aliyefariki limeendelea kuchukua sura mpya.

===================

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Mwenda, ametangaza kuwa oparesheni zote za kitengo cha Fast cha kudhibiti wakwepa kodi zitafanywa kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kuanzia sasa.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya tukio la kusikitisha la kuuawa kwa dereva wa TRA, Amani Kamguna Simbayao, aliyeshambuliwa na wananchi wakati wa utekelezaji wa majukumu yake katika eneo la Tegeta Nyuki, Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu, Bw. Mwenda amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuwakamata washukiwa wa tukio hilo na amesisitiza kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Amefafanua kuwa gari lililokuwa likifuatiliwa na marehemu na wenzake liliingizwa nchini kwa njia za magendo bila kulipa kodi, na kodi hiyo ingeweza kuchangia maendeleo ya taifa.

"Ningependa mjue kwamba kazi wanayofanya watumishi wa TRA ni kwa niaba ya Watanzania wote. Marehemu Amani alijitahidi kuhakikisha kodi inakusanywa ili kuboresha maisha ya wananchi. Hatustahili kuona wafanyakazi wa TRA wakifanyiwa matendo kama haya. Wanastahili heshima kwa kazi yao kubwa," amesema Bw. Mwenda.

Bw. Mwenda aliendelea kusema kuwa TRA itaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kodi na mamlaka ya watumishi wake katika kutekeleza majukumu yao.

View attachment 3172985

"Kwetu sisi, Marehemu ni shujaa wa taifa. Alifariki akiwa kazini, akilinda mali ya serikali kwa uadilifu na uzalendo mkubwa. Hatutamsahau kwa mchango wake mkubwa," amesema Bw. Mwenda.

Akizungumzia familia ya marehemu, Bw. Mwenda ameahidi msaada wa kiuchumi na kijamii.

Source: Jambo TV
Na raia nao watawala vichwa tu watelaji
 
Back
Top Bottom