Akiwa na kiporo tuzo za channel O, Diamond atajwa kuwania tuzo kubwa za MTV Europe

heaven on desert

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2013
Posts
1,025
Reaction score
393
Tuzo kubwa za MTV EUROPE zimewadia na Mtanzania Diamond platnumz ameteuliwa, kuwania kipengele cha mwanmziki bora wa Afrika/,kama utakumbuka za mwanzo zilikuwa ni tuzo za Mtv kwa aAfrika pekee.

Kuteuliwa huko kumekuja wakati tayari yupo nominated kwenye Tuzo zingine mbili za kimatifa,
#IRAWMA za nchini MAREKANI NA CHANNEL O ZA Africa kusini akiwa nominated kwenye category 4.

MTV EUROPE anapambana na Davido,Goldfish wa afrika kusini na Toofan wa Togo
Mungu Mbaliki diamond,Bariki Bongo fleva na Tanzania.

kwa kiwangu cha hali ya juu,diamond ameonesha nini maana ya artist to work hard, Tanzania tumekuwa tukibeza mafanikio ambayo hatujayazoea, tulizoea kuwa watu wa kuachwa mbali kwa muda mrefu,si katika soka,ngumi,riadha na michezo mingine mingi.

Tunatawaliwa na siasa katika kila jambo linalohitaji ufundi, wanaojitokeza kubeza mafanikio ya Diamond ni wale ambao hawalitakii mema taifa katika sanaa kwa ujumla, wakimaanisha wao furaha yao ni kuona hatutambuliki na tunashangilia mataifa mengine katika mafanikio yao.

Haiingii akilini msanii wa Tanzania anafanya vizuri Mtanzania ageuke kikwazo.

Nilikuwa naota kila wakati kuja kuona na sisi (Tanzania)tunaheshimika na kutambuliwa pindi wanapokaa chini kupanga nomination.





Davido (Nigeria)









Goldfish (South Africa)








Diamond (Tanzania)









Toofan (Togo)







 
namkubali sana diamond ila kwa kipindi hiki kuna msemo "penye davido diamond hakai" kiufupi davido haachi tuzo yoyote mwaka huu kazifyeka zote from b.e.t mpaka mtv africa yani ni shida kama davido amepangwa ila.nafurai hata mafikozolo wamewatupilia pemben wamemweka kijana wetu
 
Hongera zake ina maana nyimbo ya Mwana daresalama hawajaisikia huko jamaniii nimeamini palipo Daimond, Aly k hagusiii duuu

Ali k moto mwingine.......Diamond kampigwa mtama wa nguvu.We subiri balaa lake
 
point yako hasa ni nini mkuu?

kwa nini Diamond anatumia blog mnashindwa nini kutumia website??

Alafu jifunze Pr mkuu utakiwi kulalamika,unatakiwa kuelezea mafanikio yake na vitu positive kama hivi then penye kuitaji ufafanuzi unaoitajika unaelezea,penye kuitaji uhamasishaji unafanya then unajikataa. usishindane na washabiki hautokaa uwashinde .

Diamond anaonekana nje kwa sasa sababu wabongo wanamsapot sana toka day one, na sio kila anaetoa negative comment anamchukia wengine wanatania, wengine wanamkubali ila hawataki kukubali matokeo kuwa wanamkubali na wapo wasiompenda kweli ambao uwezi kuwashawishi kwa namna yoyote wana ile roho warugulu wanaita kazopata ni kuendelea kuwashawishi kwa nominations kama hizi.

All in all my point is jaribu kuwa more professional.
 
Yan people muslazmishe kupandisha aly k kupitia nasib,yan ndo mnampoteza kiba wawatu kabsaa. Video yenyewe anangoja ela ya fiesta. Mwambieni aanze taratibu kwan akimfatiliza mond ataangukia pua. Mwenzie ana hela mingi na anajua kufanya,tena kwa juhudi.
 
sio kila kitu lazima ujibu, bosi wako anaongea vizuri kuliko wewe, ushauri wangu baki na kupiga picha tu PR waachie wengine

HOD ni mgumu kushaurika ,watu jamvini wanajitahidi sana kumuelekeza lakini dogo mgumu.Watu wameshamwambia kwamba ukileta habari ilete bila kuweka hisia zako na pili awe analeta vitu ambavyo amehakiki kwa hili pili amejitahidi kwa la kwanza ndio tatizo kwake.
 
Hongera sana diamond. Unafanya kazi nzuri,utafika mbali.
 
Hongera zake ina maana nyimbo ya Mwana daresalama hawajaisikia huko jamaniii nimeamini palipo Daimond, Aly k hagusiii duuu

Mwanadaresalama ni wimbo mzuri lakini sio style ya nyimbo ambayo watu wengi wa nje wako familiar with au wanaweza kuwa intrigue with. Zitarun Bongo tu. Mfano hata style za akina jux haziwezi kuitambulisha tz nje tena ughaibuni unless zibadilike. Ni bongo na labda EA kdg.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…