Akiwa Uganda, Tundu Lissu akosoa vikali viongozi wa Afrika kwa kujilikimbizia madaraka. Amtaja Museveni na Mwalimu Nyerere

Akiwa Uganda, Tundu Lissu akosoa vikali viongozi wa Afrika kwa kujilikimbizia madaraka. Amtaja Museveni na Mwalimu Nyerere

Mbinile

Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
46
Reaction score
106
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu amewakosoa vikali wanasiasa na viongozi wa Afrika kwa tabia yao ya kung'ang'ania madaraka kwa maslahi binafsi.Akizungumza katika kikao cha kujadili masuala ya demokrasia barani Afrika katika Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda, Lissu ameainisha mbinu mbalimbali zinazotumiwa na viongozi wa Afrika kuendeleza udhibiti wa kisiasa kwa kisingizio cha kulinda katiba.

Kulingana na kituo cha habarwi cha DW, Lissu ameeleza kuwa viongozi wengi wa Afrika wanaanza kwa kuhamasisha uzalendo na kuungwa mkono na wananchi, lakini wanapopata madaraka, hujenga mifumo inayodhoofisha demokrasia. Amesema mfano halisi ni serikali ya Uganda ambayo imehusisha jeshi katika siasa za nchi, hali inayohatarisha misingi ya utawala wa kidemokrasia.

Katika hotuba yake, Lissu amesema kuwa Mwalimu Julius Nyerere alitoa mchango mkubwa katika uongozi wa Afrika, lakini baadhi ya viongozi waliiga mifumo yake ya udhibiti wa taasisi za kisiasa, kijamii, na kiuchumi kwa manufaa yao binafsi.

"Kuhusika kwa majeshi katika siasa za taifa ni hatari sana, na Mwalimu Nyerere aliwafunza viongozi wengi wa Afrika namna ya kutumia majeshi katika kudhibiti upinzani. Itakuwa vigumu kuondoa hali hiyo," amesema Lissu.

"Wakati mwingine kiongozi anafahamu kile ambacho raia hawawezi kukubaliana nacho, lakini baadaye kinakuwa na manufaa kwa taifa," amesema Dk. Ruhweza.Lissu amewataka viongozi wa Afrika kuiga mfano wa Nyerere wa kuheshimu ukomo wa madaraka na kuachia nafasi baada ya kuhudumu kwa mihula miwili, badala ya kung'ang'ania madaraka.

"Angalau wajifunze yale mazuri ya Nyerere, hasa ya kuachia madaraka kwa hiari na kuheshimu utawala wa awamu mbili,"
amesema Lissu.

Pia amesisitiza kuwa wanasiasa na wanasheria wanapaswa kushirikiana katika kuhakikisha kunakuwepo na utawala wa kidemokrasia, haki za binadamu, na kulinda katiba za nchi zao.


lissu.jpeg


Source: Jambo TV
 
Enyi Wapiga Kura wa CHADEMA tuleteeni TAL kwa kuwa ndio mtu SAHIHI wa kuleta MATOKEO CHANYA ya kutuokoa Watanzania zidi ya UDIKTETA.

Mkimrejesha mtatufanya wengi turejeshe nia ya kupiga kura 2025. Ni mtu sahihi wa kutetea wanyonge wa Afrika zidi ya MADIKTETA kama KAGAME na MUSEVENI kupitia vikao vya EAC, SADC na Umoja wa Afrika (AU).
 
M7 kashasema hawezi kuwaachia madaraka watu wajinga wajinga, Uganda nzima hajaona mrithi wake bado.
Hii ndiyo Africa.
 
Habari wanajanvi? Nilisema humu ni TAL ndio mwenye uwezo wa kuwaambia ukweli M7 na Kagame karika Surmit za AU, EAC, na SADC waache kuumiza raia. Sio dada yangu mwenye macho mazuri kazi kuwakaribisha pale Johari Hotel. Tazama hapo chini amempiga spana M7 nyumbani kwake.


View: https://x.com/Jambotv_/status/1897896338978943310?t=87hqeGzQ8EScgH9X3pCRqQ&s=19



Ukiwa mkweli sana, mnyoofu, mpinga DHULUMA, rushwa, Ufisadi au ukiwa mpenda Haki Sana, basi tambua ya kwamba kwako Afrika siyo mahali salama pa kuishi.
 
Habari wanajanvi? Nilisema humu ni TAL ndio mwenye uwezo wa kuwaambia ukweli M7 na Kagame karika Surmit za AU, EAC, na SADC waache kuumiza raia. Sio dada yangu mwenye macho mazuri kazi kuwakaribisha pale Johari Hotel. Tazama hapo chini amempiga spana M7 nyumbani kwake.


View: https://x.com/Jambotv_/status/1897896338978943310?t=87hqeGzQ8EScgH9X3pCRqQ&s=19

Kwa akili Yako unadhani style ya Lissu alivyomuongelea Museven inawezekana kutumiwa na Kiongozi wa Taifa (Raisi) na isiwe na impact?
 
Kwa akili Yako unadhani style ya Lissu alivyomuongelea Museven inawezekana kutumiwa na Kiongozi wa Taifa (Raisi) na isiwe na ict?
Nyerere amefanya sana hizi mambo. Hata PK anapigaga sana.
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu amewakosoa vikali wanasiasa na viongozi wa Afrika kwa tabia yao ya kung'ang'ania madaraka kwa maslahi binafsi.Akizungumza katika kikao cha kujadili masuala ya demokrasia barani Afrika katika Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda, Lissu ameainisha mbinu mbalimbali zinazotumiwa na viongozi wa Afrika kuendeleza udhibiti wa kisiasa kwa kisingizio cha kulinda katiba.

Kulingana na kituo cha habarwi cha DW, Lissu ameeleza kuwa viongozi wengi wa Afrika wanaanza kwa kuhamasisha uzalendo na kuungwa mkono na wananchi, lakini wanapopata madaraka, hujenga mifumo inayodhoofisha demokrasia. Amesema mfano halisi ni serikali ya Uganda ambayo imehusisha jeshi katika siasa za nchi, hali inayohatarisha misingi ya utawala wa kidemokrasia.

Katika hotuba yake, Lissu amesema kuwa Mwalimu Julius Nyerere alitoa mchango mkubwa katika uongozi wa Afrika, lakini baadhi ya viongozi waliiga mifumo yake ya udhibiti wa taasisi za kisiasa, kijamii, na kiuchumi kwa manufaa yao binafsi.

"Kuhusika kwa majeshi katika siasa za taifa ni hatari sana, na Mwalimu Nyerere aliwafunza viongozi wengi wa Afrika namna ya kutumia majeshi katika kudhibiti upinzani. Itakuwa vigumu kuondoa hali hiyo," amesema Lissu.

"Wakati mwingine kiongozi anafahamu kile ambacho raia hawawezi kukubaliana nacho, lakini baadaye kinakuwa na manufaa kwa taifa," amesema Dk. Ruhweza.Lissu amewataka viongozi wa Afrika kuiga mfano wa Nyerere wa kuheshimu ukomo wa madaraka na kuachia nafasi baada ya kuhudumu kwa mihula miwili, badala ya kung'ang'ania madaraka.

"Angalau wajifunze yale mazuri ya Nyerere, hasa ya kuachia madaraka kwa hiari na kuheshimu utawala wa awamu mbili,"
amesema Lissu.

Pia amesisitiza kuwa wanasiasa na wanasheria wanapaswa kushirikiana katika kuhakikisha kunakuwepo na utawala wa kidemokrasia, haki za binadamu, na kulinda katiba za nchi zao.


View attachment 3262510

Source: Jambo TV
bora amemtaja M7 akiwa nyumbani kwake,mwamba ni jasiri sana
 
Back
Top Bottom