Akutwa amejinyonga baada ya dili lake kutiki

Akutwa amejinyonga baada ya dili lake kutiki

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Mwili wa mtu mmoja mwenye umri unaokadiriwa kuwa na umri wa miaka 35-40 umekutwa ukiwa unaning'nia juu ya mti, akiwa amefariki kwa kujinyonga.

Kijana huyo mtanashati alitambuliwa na majirani kuwa amejinyonga mapema Leo alfajiri na alikutwa mfukoni na karatasi iliyokuwa na ujumbe uliondikwa kwa lugha ya Kiaramanic ربي اغفر لي inasomwa rabiy aghfir li.

Mtu huyo ametambuliwa kwa jina يهوذا الإسخريوطي inasomwa Yhwdha Al'iiskhryutiu.

Mtu huyo alionekana Jana asubuhi kwa wazee wa mji akiwa na Mipango nao, Kisha baada ya hapo akaonekana kwenye maduka ya masonara akiwa na vipande vingi sana vya madini ya silver, inakadiriwa vipande hivyo vilikuwa na uzito usiopungua kilo moja kwa kila kimoja na vilikuwa thelani.

Mungu ailaze roho ya marehemu peponi.
Kutokana na msiba huu mzito, TUNAOMBOLEZA mpaka jumanne.

BURIANI YUDA ISKARIOTI, BILA WEWE DUNIA ISINGEKOMBOLEWA.

TUTAKUKUMBUKA DAIMA
 
Umenikumbusha nikiwa bado dogolasi early 1990's lilifanyika igizo la Pasaka moja matata Kanisani nikiwa na Bi mdash, nilikuwa naogopa hata baada ya kurudi home,hasa baada ya Yuda kujirestishainipisi.........ilifanyika ktk Kanisa moja la Moravian pale Mbeya
 
Umenikumbusha nikiwa bado dogolasi early 1990's lilifanyika igizo la Pasaka moja matata Kanisani nikiwa na Bi mdash, nilikuwa naogopa hata baada ya kurudi home,hasa baada ya Yuda kujirestishainipisi.........ilifanyika ktk Kanisa moja la Moravian pale Mbeya
Mbeya mjini jirani na Loleza? Mimi ndiye niliyeigiza kama Yuda, enzi hizo Mchungaji akiitwa Hitson Mwamlima.
 
Back
Top Bottom