Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
AL JAMIATUL ISLAMIYYA FI TANGANYIKA (UMOJA WA WAISLAM WA TANGANYIKA) 1930s
Picha hiyo hapo chini inawaonyesha Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) wakiwa wamesimama mbele ya ofisi yao Mtaa wa Stanely na New Street (sasa Max Mbwana na Lumumba Avenue).
Wanasema picha inazugumza maneno elfu moja.
Wanasema jicho lako haliwezi kusahau kile jicho la camera iliona.
Siku chache zilizopita niliweka hapa picha ya jengo la shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika lililotaifishwa na serikali baada ya kuvunjwa EAMWS na kuundwa BAKWATA.
Waislam wameomba warudishiwe shule yao kwa kuwa waliijenga kama wakfu wamekataliwa.
Jengo hili ni mbele ya hapo ilipopigwa picha hii.
Katika picha hiyo ya Al Jamiatul Islamiyya kuna watu ambao wana historia za kusisimua sana.
Bahati mbaya sana hayakuweza kupatikana majina yote ya waliokuwa kwenye picha ila wachache hasa kwa kuwa picha ni ya zamani sana na si rahisi kutambua sura.
Lakini hapo hawawezi kukosa kuwepo Mzee bin Sudi na Ali Jumbe Kiro.
Al Jamiatul Islamiyya takriban wote ukimtoa Liwali Ahmed Saleh walikuwa wanachama wa African Association kisha TAA jina lilipobadilika mwaka wa 1948.
Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika yote ilijiunga na TANU pale chama kilipoasisiwa 1954 na Mweka Hazina wake Iddi Faizi Mafungo ndiye alikuwa pia Mweka Hazina wa TANU.
Hii ndiyo sababu ya hafla ya kumuaga Julius Nyerere safari ya kwanza UNO mwaka wa 1955 ilifanyika katika majengo ya shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Tuanze na Maalim Mohamed Matar:
Mwisho walio nyuma kushoto wa kwanza kapiga kilemba na kanzu ni Maalim Matar.
Nani Maalim Matar?
Maalim Matar alikuwa mwalimu wa kusomesha Qur'an na ndiyo aliyowasomesha wazee wetu wengi Qur'an hapo shuleni.
Mwanafunzi wake aliyekuja kuwa mtu maarufu sana ni Abdulwahid Sykes.
Maalim Matar alipata kuwekwa kizuizini mara mbili na kufungwa Ukonga, Dar es Salaam na Kiinua Miguu, Zanzibar kwa maonevu tu kwani hakupata katika maisha yake kujihuisisha na siasa.
Kassim Hanga aliporudi Tanzania akitokea Uingereza kwa Oscar Kambona na baada ya kuonywa akiwa London kuwa asirejee Tanzania na kukaidi na pia akaonywa bado akiwa Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam kuwa wala asithubutu kuingia mjini bali asubiri hapo hapo uwanja wa ndege arejee London na ndege hiyo hiyo iliyomleta na pia kukaidi, Ali Nabwa na huyo muonyaji wa Uwanja wa Ndege walimpeleka Hanga nyumbani kwa Maalim Matar akaombewe dua.
Maalim Matar watu wakimuheshimu sana kwa ucha Mungu wake na akiitadikiwa kuwa ni walii.
Kleist Sykes.
Yeye na Mzee bin Sudi ni waasisi wa African Association 1929 kisha Al Jamiatul Islamiyya 1933 wakiwa President na Secretary.
Ali Mwinyi Tambwe.
Ali Mwinyi Tambwe alikuja kuwa katibu wa Al Jamiatul Islamiyya.
Ali Mwinyi Tambwe nilipofanya mahijianonae wakati wa kutafiti kitabu cha Abdul Sykes alinambia kuwa yeye ni mkubwa sana kwa Abdul na Ally Sykes na akiwaona wakija kusali Maghrib Msikiti wa Kitumbini na baba yao kawashika mikono.
Ally Mwinyi Tambwe anasema yeye alikuwa mkubwa na akii zake kamili.
Ally Mwinyi katika picha amekaa bega kwa bega na Kleist Sykes.
Picha hii ni ushahidi wa kauli yake.
Kwenye picha hiyo Abdul ni mtoto mdogo labda miaka 10 hivi.
Ally Mwinyi akiwa na Abdul Sykes alishiriki katika mazungumzo ya kumtia Julius Nyerere katika uongozi wa juu wa TAA kwenye kikao kilichofanyika Nansio, Ukerewe nyumbani kwa Hamza Mwapachu mwaka wa 1953.
Kleist Sykes na mwanae Abdulwahid.
Hakika hawa hawahitaji kuelezwa kamwe.
Kleist Sykes kaacha mswada wa kitabu cha maisha yake na kutoka mswada huu ndiyo tumejifunza historia ya African Association na Al Jamiatul Islamiyya.
Abdul Sykes yeye maisha yake na ndiyo historia ya TANU yameandikwa na mwandishi.
Kitabu hiki ndicho kilichofunua mengi katika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kuunganisha historia ya African Association na TAA 1929 - 1954 na historia ya TANU 1954 - 1961 uhuru ulipopatikana.
Mstari wa mbele katika picha wa tano kutoka kushoto ni Kleist Sykes akifuatiwa na Ali Mwinyi Tambwe kisha Liwali Ahmed Saleh.
Mstari wa katikati wa tatu kutoka kushoto ni mtoto Abdulwahid Kleist Sykes.
Ally Mwinyi alihusika sana katika harakati za kupindua serkali ya Mohamed Shamte Zanzibar mwaka wa 1964 na yeye ndiye aliyesaidia kuweka kambi maarufu ya Kipumbwi, Tanga iliyokuwa inawavusha Wamakonde kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura kuingia Zanzibar mwaka wa 1961 kuipigia kura ASP na mwaka wa 1964 kushiriki katika mapinduzi.
PICHA: Maalim Matar, Mzee bin Sudi, Msafara wa TANU Zanzibar wakati wa kupigania uhuru Ali Mwinyi Tambwe (Ali Haluwa) wa kwanza kulia, jengo la Al Jamiatul Islamiyya na picha ya viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya 1930s.
Picha hiyo hapo chini inawaonyesha Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) wakiwa wamesimama mbele ya ofisi yao Mtaa wa Stanely na New Street (sasa Max Mbwana na Lumumba Avenue).
Wanasema picha inazugumza maneno elfu moja.
Wanasema jicho lako haliwezi kusahau kile jicho la camera iliona.
Siku chache zilizopita niliweka hapa picha ya jengo la shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika lililotaifishwa na serikali baada ya kuvunjwa EAMWS na kuundwa BAKWATA.
Waislam wameomba warudishiwe shule yao kwa kuwa waliijenga kama wakfu wamekataliwa.
Jengo hili ni mbele ya hapo ilipopigwa picha hii.
Katika picha hiyo ya Al Jamiatul Islamiyya kuna watu ambao wana historia za kusisimua sana.
Bahati mbaya sana hayakuweza kupatikana majina yote ya waliokuwa kwenye picha ila wachache hasa kwa kuwa picha ni ya zamani sana na si rahisi kutambua sura.
Lakini hapo hawawezi kukosa kuwepo Mzee bin Sudi na Ali Jumbe Kiro.
Al Jamiatul Islamiyya takriban wote ukimtoa Liwali Ahmed Saleh walikuwa wanachama wa African Association kisha TAA jina lilipobadilika mwaka wa 1948.
Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika yote ilijiunga na TANU pale chama kilipoasisiwa 1954 na Mweka Hazina wake Iddi Faizi Mafungo ndiye alikuwa pia Mweka Hazina wa TANU.
Hii ndiyo sababu ya hafla ya kumuaga Julius Nyerere safari ya kwanza UNO mwaka wa 1955 ilifanyika katika majengo ya shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Tuanze na Maalim Mohamed Matar:
Mwisho walio nyuma kushoto wa kwanza kapiga kilemba na kanzu ni Maalim Matar.
Nani Maalim Matar?
Maalim Matar alikuwa mwalimu wa kusomesha Qur'an na ndiyo aliyowasomesha wazee wetu wengi Qur'an hapo shuleni.
Mwanafunzi wake aliyekuja kuwa mtu maarufu sana ni Abdulwahid Sykes.
Maalim Matar alipata kuwekwa kizuizini mara mbili na kufungwa Ukonga, Dar es Salaam na Kiinua Miguu, Zanzibar kwa maonevu tu kwani hakupata katika maisha yake kujihuisisha na siasa.
Kassim Hanga aliporudi Tanzania akitokea Uingereza kwa Oscar Kambona na baada ya kuonywa akiwa London kuwa asirejee Tanzania na kukaidi na pia akaonywa bado akiwa Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam kuwa wala asithubutu kuingia mjini bali asubiri hapo hapo uwanja wa ndege arejee London na ndege hiyo hiyo iliyomleta na pia kukaidi, Ali Nabwa na huyo muonyaji wa Uwanja wa Ndege walimpeleka Hanga nyumbani kwa Maalim Matar akaombewe dua.
Maalim Matar watu wakimuheshimu sana kwa ucha Mungu wake na akiitadikiwa kuwa ni walii.
Kleist Sykes.
Yeye na Mzee bin Sudi ni waasisi wa African Association 1929 kisha Al Jamiatul Islamiyya 1933 wakiwa President na Secretary.
Ali Mwinyi Tambwe.
Ali Mwinyi Tambwe alikuja kuwa katibu wa Al Jamiatul Islamiyya.
Ali Mwinyi Tambwe nilipofanya mahijianonae wakati wa kutafiti kitabu cha Abdul Sykes alinambia kuwa yeye ni mkubwa sana kwa Abdul na Ally Sykes na akiwaona wakija kusali Maghrib Msikiti wa Kitumbini na baba yao kawashika mikono.
Ally Mwinyi Tambwe anasema yeye alikuwa mkubwa na akii zake kamili.
Ally Mwinyi katika picha amekaa bega kwa bega na Kleist Sykes.
Picha hii ni ushahidi wa kauli yake.
Kwenye picha hiyo Abdul ni mtoto mdogo labda miaka 10 hivi.
Ally Mwinyi akiwa na Abdul Sykes alishiriki katika mazungumzo ya kumtia Julius Nyerere katika uongozi wa juu wa TAA kwenye kikao kilichofanyika Nansio, Ukerewe nyumbani kwa Hamza Mwapachu mwaka wa 1953.
Kleist Sykes na mwanae Abdulwahid.
Hakika hawa hawahitaji kuelezwa kamwe.
Kleist Sykes kaacha mswada wa kitabu cha maisha yake na kutoka mswada huu ndiyo tumejifunza historia ya African Association na Al Jamiatul Islamiyya.
Abdul Sykes yeye maisha yake na ndiyo historia ya TANU yameandikwa na mwandishi.
Kitabu hiki ndicho kilichofunua mengi katika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kuunganisha historia ya African Association na TAA 1929 - 1954 na historia ya TANU 1954 - 1961 uhuru ulipopatikana.
Mstari wa mbele katika picha wa tano kutoka kushoto ni Kleist Sykes akifuatiwa na Ali Mwinyi Tambwe kisha Liwali Ahmed Saleh.
Mstari wa katikati wa tatu kutoka kushoto ni mtoto Abdulwahid Kleist Sykes.
Ally Mwinyi alihusika sana katika harakati za kupindua serkali ya Mohamed Shamte Zanzibar mwaka wa 1964 na yeye ndiye aliyesaidia kuweka kambi maarufu ya Kipumbwi, Tanga iliyokuwa inawavusha Wamakonde kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura kuingia Zanzibar mwaka wa 1961 kuipigia kura ASP na mwaka wa 1964 kushiriki katika mapinduzi.
PICHA: Maalim Matar, Mzee bin Sudi, Msafara wa TANU Zanzibar wakati wa kupigania uhuru Ali Mwinyi Tambwe (Ali Haluwa) wa kwanza kulia, jengo la Al Jamiatul Islamiyya na picha ya viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya 1930s.