Matojo Cosatta
JF-Expert Member
- Jul 28, 2017
- 234
- 390
ALAMA INAYOKUBALIKA WAKATI WA KUPIGA KURA NA KUHESABU KURA.
Kwa mujibu wa Aya ya 3.4 ya Maelekezo kwa Wasimamizi wa Vituo vya Kupiga Kura, 2020, alama zinazokubalika katika kupiga kura ni hizi ambazo zimeelezwa hapa kama ifutavyo;
(1) Alama inayokubalika katika chumba kilichopo wazi kwenye karatasi ya kura ni alama ya vema (√).
(2) Alama nyingine zinazokubalika ni pamoja na alama ekisi yaani “X” ilimradi tu iwe katika chumba kilicho wazi.
(3) Hatahiyo, iwapo mpiga kura atashindwa kuweka kuweka alama ya vema (√) au alama ekisi (x) kama inavyotakiwa basi alama yoyote inayoonesha wazi kwamba mpiga kura alitarajia kumchagua mgombea yupi nayo itakuwa alama halali kisheria na itakubaliwa.
⛔ N.B: Kama mpiga kura atashindwa kuweka alama katika chumba kilicho wazi na badala yake akaweka alama hiyo kwenye jina la mgombea au chama chake cha siasa au nembo ya chama chake cha siasa, alama hiyo nayo itakubalika kuwa ni kura halali kisheria.
Zingatia: "Maelekezo ya Uchaguzi" (Election Directives) ni Sheria Ndogo Ndogo ambazo zimetungwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi chini ya mashartti ya Kifungu cha 126 cha Sheria ya Uchaguzi wa Taifa, Sura ya 343.
By Matojo M. Cosatta
(the Legal Fitnaologist of Election Law and JF Senior Member).
Kwa mujibu wa Aya ya 3.4 ya Maelekezo kwa Wasimamizi wa Vituo vya Kupiga Kura, 2020, alama zinazokubalika katika kupiga kura ni hizi ambazo zimeelezwa hapa kama ifutavyo;
(1) Alama inayokubalika katika chumba kilichopo wazi kwenye karatasi ya kura ni alama ya vema (√).
(2) Alama nyingine zinazokubalika ni pamoja na alama ekisi yaani “X” ilimradi tu iwe katika chumba kilicho wazi.
(3) Hatahiyo, iwapo mpiga kura atashindwa kuweka kuweka alama ya vema (√) au alama ekisi (x) kama inavyotakiwa basi alama yoyote inayoonesha wazi kwamba mpiga kura alitarajia kumchagua mgombea yupi nayo itakuwa alama halali kisheria na itakubaliwa.
⛔ N.B: Kama mpiga kura atashindwa kuweka alama katika chumba kilicho wazi na badala yake akaweka alama hiyo kwenye jina la mgombea au chama chake cha siasa au nembo ya chama chake cha siasa, alama hiyo nayo itakubalika kuwa ni kura halali kisheria.
Zingatia: "Maelekezo ya Uchaguzi" (Election Directives) ni Sheria Ndogo Ndogo ambazo zimetungwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi chini ya mashartti ya Kifungu cha 126 cha Sheria ya Uchaguzi wa Taifa, Sura ya 343.
By Matojo M. Cosatta
(the Legal Fitnaologist of Election Law and JF Senior Member).