Alan Lucky yupo vizuri sana na anakimudu sana kile kipindi chake cha SKONGA ni zaidi ya Elim.
EATv mziki mwingine kabisa,ikiondoka Dhahabu wao wanaweka Almasi.
Aliondoka Musa wa Uswazi angalia balaa liliongia kufunika na kusafisha njia Mr.Zembwela,ni nooma.
Yaani mpaka nauliza huyu alikuwa wapi hiki ndio kipindi kinachomfaa.Sasa hivi Zembwela anakiendesha kipindi cha uswazi kwa ubora wa hali ya juu sana na uhalisia husika na unajua kabisa kwamba hiki kiumbe chenyewe kimetokea hukohuko na hakiigizi.
Namtakia kila la Kheir Alan Lucky kama ni kweli anahamia Kenya,najua atamudu vizuri tu,na hii ni fursa kwa vijana wa kitanzania kwamba na sie tuache kulalamika kwamba wakenya wanakuja kuchukua ajira zetu,muhim ni kujituma na kujiamini nakuwa mbunifu,ndio maana yeye ameonekana na kujakuchukuliwa kwa ubora wake.Big Up Brother
Ila naomba uondokea for good ili ukirudi tukupokee tena.