Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya zoezi la uchukuaji fomu za kugombea uongozi wa Serikali za mitaa kuanza, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ametangaza kuwa uongozi wa sasa umefikia ukomo leo tarehe 19 Oktoba 2024.
Wananchi wenye nia ya kugombea wamepewa muda wa kujiandaa kwani fomu zitaanza kutolewa rasmi kuanzia tarehe 26 Oktoba 2024.
Aidha, Chalamila amewakumbusha wananchi ambao bado hawajajiandikisha kwenye daftari la mkazi, kuwa muda unaoyoyoma na imebaki siku moja pekee kufikia mwisho wa zoezi hilo.
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya zoezi la uchukuaji fomu za kugombea uongozi wa Serikali za mitaa kuanza, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ametangaza kuwa uongozi wa sasa umefikia ukomo leo tarehe 19 Oktoba 2024.
Sasa mbona wengine hawakuwa namihuri tangu mwanzoni mwa mwaka huu,nilienda kijijini kwetu mwez March nikahitaji huduma ya mhuri ajabu mwenyekiti akaniambia mtendaji ameshakusanya mihuri yote kwaiyo ishu yoyote inayohitaji mhuri shart uende kwamtendaji
Sasa mbona wengine hawakuwa namihuri tangu mwanzoni mwa mwaka huu,nilienda kijijini kwetu mwez March nikahitaji huduma ya mhuri ajabu mwenyekiti akaniambia mtendaji ameshakusanya mihuri yote kwaiyo ishu yoyote inayohitaji mhuri shart uende kwamtendaji