Albert Mangwea (Special Thread)

Kampige kwanza bakora kaka yako yule teja alafu ndo uje utushawishi tumpige nakora ngwea!
Rest in peace Ngwea!
 
We unaedai ngwear alikufa kwa madawa ulikua nae? Coz riport hakuna alieiona zaidi ya familia na iliyotoka mwanzo ilikua ya mwanamuziki wa marekani, usihukumu hata ww inaweza ikatokea ukafa juu ya kimada ukim chit mkeo, na huwez jua at the time anakufa alitubu we unajiropokea tu
 

Hiyo ndiyo akili ya watu wengi kusifia upumbavu.
 
Hili suala la ngwair ni kama vile kesi inapokuwa mahakamani haistahili hata kidogo kujadiliwa nje ya mahakama hivyo basi Mungu ndiye jaji wa kila kitu kwa sasa ndie mwenye maamuzi sahihi peke yake.
 
Siwezi sema ngwea aliishi vp kikubwa tunajifunza nn ktk msiba wake, kwa maana ya tunakabiliana vp na changamoto tunapokutana na hali za kukatisha tamaa na mabadiliko ktk maisha, eg kuugua, kufilisika, kuanguka ktk fani, na nk na hiyo ndo point cyo aliishije na ataenda wp? Kama jamii tujiulize tunawasaidia vp watu wakiwa ktk hali ya msongo kutokana na sababu mbalimbali
 
Tumuombee Mangwair apumzike kwa amani. Hisia za upendo mkuu baada ya kifo chake km vile umati wa watu kujitokeza, kusukuma gari iliyobeba mwili, uwakilishi wa serikali nk visiwe sababu ya kupeleka akili zetu likizo. Mangwear ameuawa na matumizi ya mchanganyiko wa pombe na madawa ya kulevya. Kifo chake kimeipa jamii ya watanzania fursa ya kutafakari biashara ya madawa ya kulevya nchini,wauzaji wake ambao tunaambiwa baadhi ni mawaziri, utekelezaji wa sheria zetu, maadili nk. Haya hayawezekani kwa kumfanya Mangwear shujaa-naamini hata yeye angepata second chance angejutia tatizo lake na kuwafunda vijana wenzake. Badala yake tunaona viongozi wa serikali na kidini wakiitupa fursa hii kuasa vijana waliobakia juu ya madhara ya ulevi wa kupindukia na maawa ya kulevya. Haya ni ushahidi wa kukosekana kwa 'moral authority' kwa viongozi hao. JK alisema kuna viongozi wa dini ni wauza unga, na Kangi Lugola (Mb) alisema kuna mawaziri wanauza unga. Matokeo yake jamii imepata 'criminal cult heroes'. Waheshimiwa watuhumiwa wamepokelewa(wamejipokelesha?) majimboni kwa maandamano nk.
 
Mi naamini ktk Biblia na
ndiyo sababu si muongo, mnafiki, waongo, wachawi, wazinzi, wafiraji
hawata ulithi uzima wa milele, ukajitenge nao wafanyao uovu.

ni biblia ipi unayoiamini wewe?mbona leo unamuhukumu marehemu wakati biblia inasema mwenye mamlaka ya kuhukumu ni Mungu na sio binadamu?
Napata kujiridhisha ktk hili,kuwa huko makanisani kwenu mnadanganywa sana,BTW,UNASALI KANISA GANI?NISIJE NIKAWAHUKUMU WOTE WANAOIAMINI BIBLIA!.
 
Asingekuwa na mazuri wa2 wasinge jaa uwanja wa Jamuhuri mpaka kufungwa,wa2 wasinge mpokea barabarani akitokea dsm....
 
Mkuu ndo majina ya wajapani yalivyo, yani full vituko mara Kazakuku Takombili....yaani aibu...

hahaha Baba V, taratibu usijenikumbusha, zamani kulikuwa na shirika la umma tanzania linaitwa TAKOSHILI hahaha.
 
Hii tabia ya kuwa mna msifia mtu anapo kufa tuiache MANGWEA hakuwa mtu mzuri ninaimani watu alio washawishi kuingia kwenyekundi la kutumia madawa ni wengi sana, kama tulikuwa tunampenda kwa kiasi hiki, mbona tulimuacha na hakusaidiwa kama RC?,

Kawaulize clouds maana waliomboleza mwanzo mwisho...ila akiwa hai sikuwahi kusikia nyimbo ya Ngwair ikipigwa clouds miaka ya karibuni zaidi ya kusikia joni....joni...yes papaa...
 

Bwana mdogo, usiishi kwa illusions. Wanamuziki wa Marekani ni watu taahira tu kama ulivyo wewe na wenzako mnaoamini kwenye maisha ya ujana. Wanachoweza kusema ni 'Rest In Piece' kwa sababu wao PEACE hawaijui.

Hata wajipange wanamuziki kwa wingi kama vigae vya kuezekea nyumba, hatma ya roho yako unayo mwenyewe. Itafute kweli na hiyo kweli itakuweka huru. Huyo marehemu kilichomuua ni huo huo utaahira wa kuamini yupo juu. Juu yupo Mungu na hizo anasa ndio janga lenu.

Kuwa mwanamuziki haimaanishi ubadilishe maisha, ukose adabu kwa kutembea makalio nje, ukatoboe masikio mtoto wa kiume halafu utegemee ukifa watakuja wanamuziki wa Marekani na kumwamrisha Mungu akuweke mahali pema peponi....idiot!

Bif, bro, yuko juu, no bif.....typical nonsense!
 

Kwangu mimi, kusoma wasifu wa marehemu sio WADHIFA. Na unaongea hivyo kwa kuwa hunijui hata kidogo. Sina kawaida ya kupepesa macho wala kung'ata maneno.

Hii jamii imeharibika na utandawazi kiasi mmeona kwamba, usipoweka wave kwenye nywele na kuvaa suruali chini ya ------ basi wewe hujawa kijana. Mnasifiana ujinga na kuyaacha yaliyo na tunu kwenu.

Huyu kafa kwa ujinga wake na sio kwa kukosa dawa kiasi tumzungumzie kwa hisia za kumuonea huruma. Wote tutakufa kwani kufa ni ada, lkn kufa kipumbavu ni dhalili ya utu wako mwenyewe.

Mmejazana pale uwanjani kila mmoja anasema Mungu amuweke mahali pema peponi, mnasema kwa kumaanisha au kwa mazoea?

Wakati Mandela anasema mwanae amekufa kwa ukimwi ina maana hakuwa mstaarabu? Ustaarabu na unafiki ni mambo mawili tofauti. Nikifa kesho kwa ulevi, walioko nyuma yangu na waambiwe ili wajifunze kuwa unywaji wa pombe sio 'wadhifa' bali ni upuuzi...FULL STOP; NUKTA
 
unadhani ukiandika maneno makali ya dharau na kebeh ndio utaeleweka, wewe huiwezi kazi ya ushauri japo una hoja za msingi..

Yo are asking me to sweet-talk you? Never!

Tanzania yetu imejaa watu wenye mzaha kwenye mambo ya msingi na umakini kwenye mambo ya kipumbavu. This is the right way to talk to this generation. Hizo hoja za msingi umeziona kwa kuwa zimeambatana na attention tag ya maneno unayoyaona makali.

By the way, pathetic maana yake DHAIFU and that suits you better.

Na usiniombe kumheshimu mtu ambaye hakujiheshimu wala kujipenda. Leo nasema ya huyu mwenye kula midawa, huko mtaani kuna mwingine ni wa kiume lakini anatoboa masikio na kuacha makalio nje majukwaani. Akifa naye huyo, mniombe nimuongelee kwa kumsifia....damn!

Nadharia ya matumizi ya upumbavu kwenye mambo ya msingi ndio imetufikisha hapa. Alipokufa yule mwenzenu mwingine, hakuna aliyefikiria mazingira ya kufa kwake kwamba yalisababishwa na uhalifu wake. Wote mlikimbilia kumlaumu mtoto ambaye ni victim wa ngono wa marehemu....that was not right. Jamii ilipaswa kuelezwa na kuonywa juu ya mambo ya namna ile.

Mimi sio mshauri nasaha wala paroko to sweet-talk you. Ukijiona umepinda kiasi umeanza kujikatia tamaa jikabidhi kwangu, nitakupa maneno makali kiasi kila unapotaka kufanya upumbavu unayakumbuka na unaghairisha ujinga wako na kuwa salama.
 
Mwana Mtoka Pabaya, you are telling it as it is! Sijaandika kwenye fb about ngwear hata siku moja. Nilikutana na rafiki yangu kipenzi miaka 15+ toka tuachane na she was addicted. Alikuwa kafulia pia. Nikamuambia kwanza i aint buying you no alcohol. Ati mume alinifrustrate na mie sikusoma kwa ajili yake! Alijidakia mzungu akasepa. Nikamuambia anakufrustrate umemzaa wewe? Na drugs and alcohol zimesolve matatizo yako?

Tough love ni muhimu sana.
 
Last edited by a moderator:
Na ningemshangaa angekwenda kuzika wahuni akaacha kazi yake ya safari zisizo na mwisho wala maslahi. Tusikengeuke tukawa kama wazungu, kwa akili kama hizi ndio leo tuna Sir Elton John ambaye ni mke wa mtu. Naye akifa, mtataka heshima kwake

Yule asiye na dhambi kabisa na awe wa kwanza kurusha jiwe.
 
Dunia tambala bovu! Wahenga walinena,"Hujafa hujaumbika!" Toka niwe na ufahamu wa kujua nini maana ya kifo na kushiriki misibani, mara nyingi marehemu husifiwa hata kama alikuwa mwizi,mzinzi,mchawi,mlevi n.k! Sifa hizi mara nyingi hutolewa na ndugu au jamaa ambao marehemu alikuwa anashirikiana nao katika mema au mabaya!

Ni vizuri ndugu,jamaa na marafiki wakatoa taarifa za kweli zilizosababisha kifo cha marehemu. Kwa mfano marehemu kafa kwa ukimwi,ulevi,TB,nk, hakuna sababu ya kuficha chanzo cha kifo! Nawapongeza wale wote wanaosema sababu za kweli za vifo vya wapendwa wao ili jamii iweze kujifunza.

Kuna jamaa mmoja yupo Tabata Mawenzi. Siku ya msiba alipokuwa akisoma wasifu wa marehumu dada yake,hakuona aibu kusema dada yake kafa kwa UKIMWI! Aliongea mbele ya mume wa marehemu dada yake na familia yake! Kulikuwa na ukimya mkuu sana!! Yahitaji ujasiri!
 

sijutii kukuomba samahani siku ya tarehe 31/12/2012.........
nilijua hukustahili niliyokwaambia na leo umenithibitishia hapa.
you are the best dude.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…