Algeria yapuuzia maombi ya kuongeza uzalishaji wa gesi kufidia gesi ya Urusi

Algeria yapuuzia maombi ya kuongeza uzalishaji wa gesi kufidia gesi ya Urusi

Mtamba wa Panya

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2017
Posts
764
Reaction score
1,892
Taifa la Algeria mpaka sasa limeendelea kuwa "Neutral" na limekataa kuongeza uzalishaji wake wa gesi kwa ajili ya soko la Ulaya kufidia "gepu" lililoachwa na nchi ya Urusi, Vyombo vya habari vya nchi za kiarabu vimeripoti.

A foreign delegation visits on December 14, 2008 the Krechba gas treatment plant, about 1,200 km (746 miles) south of Algiers. The In Salah gas project, a four-year old venture grouping energy majors Sonatrach of Algeria, BP of Britain and Statoil of Norway, is described by its managers as the world's first and largest onshore carbon capture and sequestration scheme. The Organization of Petroleum Exporting Countries (OPEC) is due to meet on December 17, 2008 in the Algerian city of Oran. AFP PHOTO / STR (Photo by STR / AFP) (Photo by STR/AFP via Getty Images)

Miundombinu ya LNG

Msimamo huo wa Algeria umedhihirisha umuhimu wa uhusiano wa kidiplomasia kati ya Algiers na Moscow tokea uhuru wa taifa la Algeria mwaka 1962 pale USSR ilipotangaza kuingia uhusiano wa kidiplomasia kati yake na Algeria.

Wakati huo huo, Algeria ilitambua Taifa la Urusi mwaka 1991 baada ya kuvunjika kwa USSR. USSR ilikuwa miongoni mwa nchi muhimu zilizosaidia Kisiasa na kivita kwenye vita ya ukombozi wa taifa la Algeria na ilikuwa nchi ya kwanza Duniani kutambua serikali iliyoundwa.

Ushirikiano wa kiuchumi baina ya mataifa hayo mawili ulianza tokea miaka ya 1960 pale USSR ilipoipatia Algeria mikopo kwa ajili ya miradi ya maendeleo wakati inatokea kutawaliwa kwa miaka zaidi ya 130.

Kwa usaidizi kutoka USSR, miradi muhimu ya kiuchumi ilianzishwa nchini Algeria ikiwemo viwanda vya steel na chuma, uzalishaji wa Umeme, bomba la gesi pamoja na bwawa la maji.

Mpaka sasa, kampuni ya Taifa ya mafuta ya Algeria, Sonatrach ina ushirikiano wa karibu na kampuni za nishati za Urusi na pia nchi hizi mbili zimesaini mikataba ya ushirikiano kwenye sekta mbali mbali.


Algeria inasambaza na kuuza gesi barani Ulaya kupitia mabomba makubwa matatu.

Akizungumzia ombi la Ulaya kufidia uuzaji wa gesi, CEO wa zamani wa Sonatrach alisema "Kiwango cha gesi kinachosambazwa na Algeria kwa mwaka barani Ulaya ni mita za ujazo billioni 42, wakati Urusi inaweza kusambaza kiwango hiki kwa bomba moja tu ".

"Kiukweli hakuna nchi yoyote inayoweza kuziba gepu la uzalishaji wa nchi ya Urusi kwa sasa, kuna mkakati wa nchi za Ulaya kupunguza utegemezi wa gesi kutoka Urusi kupitia vyanzo mbadala kama Algeria, Qatar na USA" aliongeza kusema.

Pia ikumbukwe kuwa Urusi ndio muuzaji namba moja wa silaha kwa Taifa la Algeria. Kwa miaka ya karibuni, kwa mujibu wa waangalizi, Algeria imenunua silaha kutoka Urusi zenye thamani ya mabillioni ya dola zikiwemo Sukhoi na MiG (ndege), helikopta, vifaru pamoja na submarine.
 
Bongo tuna Gesi nyingi kuliko ya Russia hivi underground movement zinaendelea usiwastue waendelee kususa sisi twala
 
Bongo tuna Gesi nyingi kuliko ya Russia hivi underground movement zinaendelea usiwastue waendelee kususa sisi twala
Gesi ya bongo inatutosha wenyewe tu tuki-export hata Kenya haimalizi miaka 10 itakuwa imekauka lakini Gesi ya Russia inatosha kwa matumizi ya dunia nzima kwa miaka hata 10000 na haiwezi kuisha
 
Bongo tuna Gesi nyingi kuliko ya Russia hivi underground movement zinaendelea usiwastue waendelee kususa sisi twala
Hapana hatuna nyingi kuliko Russia

Hata tungekuwa nayo nyingi Russia ana advantage tayari kuna Pipe which is cheaper..., Sisi kufika huko inabidi iwe converted to Liquid (LNG) Liquefied Natural Gas ambayo inahitaji uwekezaji wa Plant..., kitu ambacho tayar America anacho (LNG) na sasa ni exporter mkubwa worldwide (in short hapa USA ndio anakula).....
 
Sasa kwanini wasije kutuomba sisi Tanzania tuongeze uzalishaji 😂😂😂, anyway, na sisi tufanye haraka ule mradi wetu wa LNG huko mtwara
 
Gesi ya bongo inatutosha wenyewe tu tuki-export hata Kenya haimalizi miaka 10 itakuwa imekauka lakini Gesi ya Russia inatosha kwa matumizi ya dunia nzima kwa miaka hata 10000 na haiwezi kuisha
Kwamba wanaotaka kujenga LNG plant kule Lindi wanapoteza mabilioni ya dola kwa project ya miaka 10?
 
Hapana hatuna nyingi kuliko Russia

Hata tungekuwa nayo nyingi Russia ana advantage tayari kuna Pipe which is cheaper..., Sisi kufika huko inabidi iwe converted to Liquid (LNG) Liquefied Natural Gas ambayo inahitaji uwekezaji wa Plant..., kitu ambacho tayar America anacho (LNG) na sasa ni exporter mkubwa worldwide (in short hapa USA ndio anakula).....
Still mahitaji ya gesi duniani ni makubwa sana. Logistics za gesi zipo expensive and complicated ndo maana supply ni changamoto.

Tanzania tungekuwa na LNG plant, tungekuwa tunaingiza madollari sasa.
 
Hapana hatuna nyingi kuliko Russia

Hata tungekuwa nayo nyingi Russia ana advantage tayari kuna Pipe which is cheaper..., Sisi kufika huko inabidi iwe converted to Liquid (LNG) Liquefied Natural Gas ambayo inahitaji uwekezaji wa Plant..., kitu ambacho tayar America anacho (LNG) na sasa ni exporter mkubwa worldwide (in short hapa USA ndio anakula).....
Still mahitaji ya gesi duniani ni makubwa sana. Logistics za gesi zipo expensive and complicated ndo maana supply ni changamoto.

Tanzania tungekuwa na LNG plant, tungekuwa tunaingiza madollari sasa.
 
Gesi ya bongo inatutosha wenyewe tu tuki-export hata Kenya haimalizi miaka 10 itakuwa imekauka lakini Gesi ya Russia inatosha kwa matumizi ya dunia nzima kwa miaka hata 10000 na haiwezi kuisha
Kuongea kwa facts ni muhimu sana.
 
Back
Top Bottom