Ali Kiba ahujumiwa tuzo za Afrimma. siri yafichuka

AdvocateFi

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
11,492
Reaction score
5,047
Habari wakuu!
Ule msemo kuwa mziki umetawaliwa na kila aina ya ghilba, fitna ,figisu na kila aina ya uchafu sasa umetimia.

Itakumbukwa mwaka jana msanii wa Bongoflava Alikiba aliandika ujumbe kwenye page yake instagram kuwa "kuna watu wanajaribu kupoteza pesa zao kwa kuhonga waandaji wa tuzo ili kumshusha Kiba kimziki",

Kauli hiyo ilipingwa vikali na mahasimu wake kimziki ikiwemo genge la WCB. Lakini kwa wenye akili tuliamua kuchukulia suala hilo for profit na kuanza kutafutia ukweli juu ya hilo.

Ni mwezi August 2016 ambapo waandaaji wa tuzo za Afrimma walitoa majina ya wasanii waliochaguliwa kushiriki huku Diamond na Alikiba wakiwa ni watanzania waliokuwa wapo katika category ya "Best east Africa male",

Kama tulivyoshuhudia juzi matokeo yake yamegubikwa na ukungu mzito hasa ukizingatia Msanii alikiba ndiye aliyekuwa anaongoza kwa kura kwa zaidi ya robo na kuwapiga gap washiriki wenzake wote katika category hiyo. Mshindi aliyetangazwa si halali na hilo limebainika baada ya miongoni mwa vijana wazalendo wa IT waliokuwa wakiendesha zoezi hilo kufichua siri hiyo kupitia mtandao wa perscope.

Swali la kujiuliza, hawa wanaonunua tuzo wanapata faida gani? Maana kama graph ya msanii wao kimziki inashuka je njia sahihi ni kufanya fitna za namna hii?

Mhusika mkubwa wa hujuma hizi ni ni promoter mtanzania anayeishi USA anayejulikana kwa jina la DMK ambaye yeye na Alikiba ni mwaka sasa wamekuwa na mgogoro wa kimaslahi baada ya Alikiba kukataa kutumika kama rubber stamp kwa kupiga show zenye maslahi madogo,

kwahiyo hii inasadikiwa kuwa ni sababu ya promoter huyo kumuhujumu Alikiba, hivyo msitarajie hata siku moja mkamsikia Alikiba akiwa ameshinda kwenye tuzo zozote zilizopo chini ya promoter Dmk, tuzo kama Afrimma USA, AEUSA.

[HASHTAG]#JusticeForKiba[/HASHTAG] [HASHTAG]#SolidarityForever[/HASHTAG]
 
Vote for Olamide...
[HASHTAG]#Mtvema[/HASHTAG]
*sitaki shari
 
Nataka Mimiload ushahidi wa unonesha idadi ya kura za washiriki wote, lakini nashindwa, yeyeto anaueweza kunisaidia anielekeze namna ya kuapload images.
 
Mbona vijana wa kiba kila kukicha mnatokwa na mapovu nawaomba xna mjitadhimini upya kuliko kila kukicha mnaleta vicngizio kibao ,naomba niwaombe kitu kimoja kuwa ujinga huo mnaojifunza kwa kujilalamisha kwa kila kitu hakiwafikishi kokote ila mwisho wa cku mtafutika kama 20per cent
 
Kila siku huwa nasema mashabiki wa Kiba mnampoteza msanii wenu, kila akifeli mnajitahid kutafta sababu mara uchawi, mara figisu. sasa hivi kiba ni msanii bora east africa!! Kwa lipi alilofanya!!?.
* kiba kama msanii aache kulalamika afanye kaz na ajue yeye si mwanamuziki bora siyo east afrika tuu bali hata tukisema Kigoma peke yake Kiba si bora
 
Kila siku huwa nasema mashabiki wa Kiba mnampoteza msanii wenu, sasa hivi kiba ni msanii bora east africa!! Kwa lipi alilofanya!!?.
* kiba kama msanii aache kulalamika afanye kaz na ajue yeye si mwanamuziki bora east afrika

Kama hautambui ubora wa kiba, pole yako ila boss wako anautambua.
 
Team kiba [HASHTAG]#team[/HASHTAG] kulia lia#team lawama#team kutojiamini!
Hahaha hv mtaacha lini? We Shardcole acha kumtafuta mchawi
Mnanyota ya lawama nyie mmezaliwa kiangazi mkiongozw na kibabuuuun

Tulia mkuu maana hueleweki.
 

Tofautisha lawama na ukweli
 
Nataka Mimiload ushahidi wa unonesha idadi ya kura za washiriki wote, lakini nashindwa, yeyeto anaueweza kunisaidia anielekeze namna ya kuapload images.
Shardcole heshima yako Mkuu
Naomba nitofautine mawazo na wewe na naomba usikwazike tafadhali..

1. Lazima utambue kuwa AFRIMMA ni tuzo zenye hadhi kubwa na kamwe usanii wakitoto hivyo hauwezi kufanyika kiasi kwamba ati unaweza tu kuingia periscope na kujua kwamba wamecheat.. Ukitaka kujua ukubwa wa hizo tuzo angalia orodha ya Sponsors pia angalia jinsi wenzetu wa Afrika Magharibi wanavyoziheshimu!! Huo usanii wa kitoto hivyo ni impossible kufanyika

2. Tuzo za AFRIMMA na AEUSA haziko chini ya DMK kama unavyodai.! DMK ni promota wa matamasha tu na ukaribu wake na Diamond ni kwamba kama haufahamu yeye ndiye meneja wa diamond kwa USA. Lakini hana uwezo na wala sio anayemiliki tuzo za AFRIMMA na AEUSA.. Hii kafanye research tena

3. Kiba ni msanii mzuri ila ana inferiority complex! Nilichogundua ni kuwa akiwekwa category moja na diamond kwenye tuzo yoyote huwa ahamasishi watu wampigie kura coz anaamini diamond atachukua alafu ataonekana alikuwa anaitaka tuzo alafu ameikosa so suluhisho anaonaga bora asihamasishe kabisa.. Mfano tuzo hizi alikaa kimya lakini angalia jinsi anavyo hamasisha apigiwe kura MTV Ema coz kule yuko peke yake diamond hayupo!!
Kiba anatakiwa aanze kujiamini

4. Kiba pamoja na mashabiki na menejimenti yake wanatakiwa wakue kiakili na kimikakati! Waache utoto wa kutupia wengine lawama pale wanapofeli kimikakati na kushindwa kufikia malengo.. Wakiendeleza huu utoto baada ya mwaka mmoja watajikuta mtaani watu wanabishana kiba na harmonize nani mkali?? Hata Rayvany hadhi yake atajikuta iko juu kuliko yeye..
Mwanaume ukishindwa kufikia malengo unakaa chini unajitathimini sio kutupia wengine lawama.!!

Steve Jobs aliwahi kuwaambia wafanyakazi wa Apple kuwa wanatakiwa waache mawazo mgando kuwa ili Apple ifanikiwe inabidi Microsoft wafeli! Hayo ni mawazo finyu coz Apple inaweza kufanikiwa hata Microsoft nayo ikiwa inafanikiwa..
The same nawaasa team kiba, waache kufikiria kuwa ili kiba awe juu ati inabidi WCB washuke! Mimi nasema hapana, kiba anaweza akafanikiwa hata WCB ikiendelea kuwa juu.. Pia achukue WCB kama mfano kwake jinsi wenzake wanavyopanga mikakati na kuitekeleza! Hiyo ndio positive mentality
 
Hahujumiwa na nani aisee.. Kuna watu hawana roho nzuri hila Mungu hanawaona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…