Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,931
- 24,816
Dada yake Mo Dewji alikuwa amekutana na Meddie Kagere, baada ya kusalimiana dada akaanza mtania Meddie.
"Wewe unawaonea dagaa tu kambale huwawezi"
Meddie akacheka kidogo na kuuliza, "Ina maana Yanga na zile team afcon ni dagaa? Basi nitajie team unayotaka niifunge hapa TZ kwa sasa"
Ndiyo dada kusema Azam wana team nzuri na najua mechi yao na Simba itakuwa tough...wapige bao. Ukifanikiwa ntajua wewe kidume nakupa 50,000,000/="
Meddie alicheka sana akasema "angalau ungenambia Ruvu Shooting, hao Lamba Lamba ntawalamba tu, weka mpunga tayari"
Ndiyo kilichotokea. Meddie akawagonga AZAM kimoja.
Akapewa mpunga wake 50,000,000. Hapo ndipo alipoonesha ukomavu wake. Hii pesa angekuwa mtu mwingine asiyejielewa angeenda itumia peke yake.
Lakini Kagere alikumbuka kitu kimoja. Kuwa siku ya mechi hakucheza peke yake. Ule mpira alioufunga hakutoka nao nje ya uwanja akaingia nao ndani akakimbia na hatimaye kufunga. Alifikiria nje ya mawazo ya kuwa yeye ndiyo alifunga lile goal.
Kagere alikumbuka simba ndo ilishinda lile goli ambalo yeye alilimalizia. Hiyo pesa akaitoa kwa team igaiwe kwa kila mchezaji aliyekuwa ndani ya uwanja na nje ya uwanja.
Kwa kitendo hicho unadhani nani atamnyima pasi Kagere? Kama anaona yupo kwenye nafasi ya kufunga kwa nini asipewe pasi ashinde maana hana ujivuni. Anatambua kuwa Simba ni team na Simba si yeye.
Anatambua kuwa ushindi wa Simba unaanzia kwa kipa uwanjani mpaka mshambualiji anatambua pia unaendelea mpaka kwa wachezaji ambao wapo nje ya uwanja kwa mechi hiyo.
Huu ndo ukomavu tunaozungumzia. Mchezaji unapaswa ufikirie kwa mapana, si kwa ubinafsi. Unapaswa usijifikirie wewe, unapaswa ufikirie team nzima. Hiyo ndiyo maana ya ukomavu wa mchezaji.
"Wewe unawaonea dagaa tu kambale huwawezi"
Meddie akacheka kidogo na kuuliza, "Ina maana Yanga na zile team afcon ni dagaa? Basi nitajie team unayotaka niifunge hapa TZ kwa sasa"
Ndiyo dada kusema Azam wana team nzuri na najua mechi yao na Simba itakuwa tough...wapige bao. Ukifanikiwa ntajua wewe kidume nakupa 50,000,000/="
Meddie alicheka sana akasema "angalau ungenambia Ruvu Shooting, hao Lamba Lamba ntawalamba tu, weka mpunga tayari"
Ndiyo kilichotokea. Meddie akawagonga AZAM kimoja.
Akapewa mpunga wake 50,000,000. Hapo ndipo alipoonesha ukomavu wake. Hii pesa angekuwa mtu mwingine asiyejielewa angeenda itumia peke yake.
Lakini Kagere alikumbuka kitu kimoja. Kuwa siku ya mechi hakucheza peke yake. Ule mpira alioufunga hakutoka nao nje ya uwanja akaingia nao ndani akakimbia na hatimaye kufunga. Alifikiria nje ya mawazo ya kuwa yeye ndiyo alifunga lile goal.
Kagere alikumbuka simba ndo ilishinda lile goli ambalo yeye alilimalizia. Hiyo pesa akaitoa kwa team igaiwe kwa kila mchezaji aliyekuwa ndani ya uwanja na nje ya uwanja.
Kwa kitendo hicho unadhani nani atamnyima pasi Kagere? Kama anaona yupo kwenye nafasi ya kufunga kwa nini asipewe pasi ashinde maana hana ujivuni. Anatambua kuwa Simba ni team na Simba si yeye.
Anatambua kuwa ushindi wa Simba unaanzia kwa kipa uwanjani mpaka mshambualiji anatambua pia unaendelea mpaka kwa wachezaji ambao wapo nje ya uwanja kwa mechi hiyo.
Huu ndo ukomavu tunaozungumzia. Mchezaji unapaswa ufikirie kwa mapana, si kwa ubinafsi. Unapaswa usijifikirie wewe, unapaswa ufikirie team nzima. Hiyo ndiyo maana ya ukomavu wa mchezaji.