Alichokitaka Manara kwa TFF amefanikiwa

pwilo

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2015
Posts
10,913
Reaction score
13,876
Kwa wapenzi na wadau wote wa soka habari za wakati huu nawasalimu kwa jina la tozo na makato yaendelee.

twende kwenye mada:–

Manara ni mtu mmoja mbinafsi sana anayeendekeza chuki na visasi kwa mashabiki wa team pinzani au kwa viongozi ambao yeye ana tofauti nao ili aonekane yeye ndo yupo sahihi au anaonewa hata kipindi yupo simba aliwapiga marufuku mashabiki wa yanga wasiingie taifa kwenye mechi za simba ila leo wamesahau na wanamuunga mkono kila kitu anachosema.

Baada ya Manara kupewa adhabu na TFF alitaka kuwaaminisha watu kwamba amepewa adhabu ili kuidhoofisha yanga unajiuliza yeye sio mchezaji wala hayuko katika nafasi za uongozi wa juu sasa kwa nini aseme yanga inataka kudhoofishwa kupitia yeye wakati kipindi yupo simba wananchi walikuwa wanafanya mambo yao wenyewe bila yeye.

Amefanikiwa kueneza chuki kwa mashabiki wa yanga ili waichukue TFF na kweli amefanikiwa kwenye hilo hata akipewa adhabu yeye binafsi ataihusisha na yanga hata kama kweli kuna makosa na kila mtu anaona amefanya kama alivyoenda kwenye yanga day wakati anajua kabisa ana adhabu sijui kiburi anatoa wapi yule mtu inawezekana ikawa kweli TFF na yanga wana tofauti ila anachokifanya yeye ni kuongeza tatizo ili TFF ionekane ina makosa kitu ambacho sio sahihi.

Juzi kwenye dirisha la usajili wakati linakaribia kufungwa team ya wanawake ya yanga princess ilikuwa miongoni mwa team ambazo zilikuwa hazija sajili majina ya wachezaji wao na wakakumbushwa kufanya hvyo hapo walikuwa wametega likitokea la kutokea wajifiche kwenye kivuli cha kuonewa na TFF kwa hilo Manara amefanikiwa.

Wachezaji wa yanga wakigeni wanaonekana kwa idadi wamezidi 12 je ni kweli walipeleka jina mapema la mchezaji wanaetaka kumuacha na kumuongeza au hawakuwa na uhakiki wa dili kukamilika na walipogundua wameshindwa wakaamua wajifiche kwenye kivuli cha kuonewa na TFF unajiuliza kwani wao TFF wanafaidika na nini kisinda akisajiliwa au asiposajiliwa kwenye system tatizo la mashabiki wa yanga wanabeba taarifa kama ilivyo kutoka kwa Manara iwe ya propaganda au ya kweli kwa hilo amefanikiwa.

Juzi wamepewa adhabu na TFF ila badala waangalie tatizo la adhabu waliyopewa wakajificha kwenye rafu ya inonga na kuonewa na TFF kitu ambacho Manara ndo anakitaka na ndo kinampa furaha na kwa hilo kweli wamefanikiwa kuwagombanisha na TFF.

Haya mnamuacha nani kati ya wachezaji 13 mnaotaka tifua tifua wawasajili wote kwenye mfumo ili muweze kuwatimia.

NB: Manara alifungiwa kujihusisha na mpira maisha ila karia ndo alimtoa kwenye kifungo hicho kwa hyo kufungiwa hajaanza kufungiwa akiwa yanga ieleweke hvyo ili twende sawa.
 
Kwa wale mambwiga mnaomtetea Haji oneni uchokozi huu kwa Mwakinyo,akijibiwa sawa na wazimu wake mnasema anaonewa kwa vile ni zeruzeru. Jee Haji anayokinga ya kutukana watu bila kujibiwa kwa huo uzeruzeru wake? Matusi yote kwa Mwakinyo ni kwa vile tu Mwakinyo ni mshabiki wa Simba.
 

Attachments

  • VID-20220905-WA0001.mp4
    2.7 MB
Mbona mnatumia nguvu nyingi kujitetea? Kulikoni!!
 
Alafu hapa mara kaongea yupo mtungi kwelikweli,maana sauti imekuwa ya kipombe pombe
 
Sheria na kanuni za TFF zinasema kusajili wachezaji wa kigeni mwisho 12.haya tuambieni mngemtoa Nani hapo?
Mbona ninyi hamtumii akili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…