Alikiba: Unaweza Nichukia, Ukapenda Muziki Wangu

fungi

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2014
Posts
2,539
Reaction score
4,672
Msanii Alikiba amefunguka na kusema kuwa muziki hauna siri na muziki hauna tofauti kati ya mtu na mtu kwani unaweza kuwa una chuki na yeye lakini akiimba muziki mzuri ukapenda kazi yake na kuimba.

Alikiba alizidi kutoa ufafanuzi kuwa kama binadamu inawezekana ukatoa labda humpendi mtu fulani au msanii fulani kutokana na mambo yake lakini inapokuja kwenye muziki inakuwa tofauti maana msanii anapofanya wimbo mzuri, utajikuta tu unaimba wimbo ule kwa kuwa muziki una nguvu na haina mipaka, wala tofauti.

Alikiba alizidi kusema kuwa hata kama unaweza kuwa unamchukia mtu inafika wakati unasahau na kupotezea na maisha ya kawaida yanaendelea na kujikuta ule utofauti wenu umepotea
 

Huyu naona atageuka mhubiri sasa hivi ...maneno meengi!!
 
hahaaaaaaaa naye kaaanza kubwabwaja siku hizi
 
Ni ukweli unaogusa nyoyo nyingi sana kuwa Ali Kiba huenda ndiye msanii anayetengeneza mziki mtamu zaidi Tanzania na Africa Mashariki kwa ujumla....Jamaa ana utamu flani hivi kuanzia sauti na hata melody zake....

Hakuna anayeweza kusikiliza Aje au Nagharamia kisha akabisha hili....

#sinaTeam
 
Kwani nani anamchukia? Kafanya nini?
 
Kwani nani ana mchukia? Kafanya nini?
sidhan kama kasema anachukiwa but nilichoona kazungumzia in general life yan iwe kwa mtu wa kawaida au msanii, unaweza usimpende yeye na maisha yake but ukapenda kazi yake which is very true
 
naked truth
 
kiba wa sasa siyo yule wa sindelela. Amepoteza radha
 
sio kweli coz mtu mwingine anaweza kukuchukia hata sauti yako asitake kuisikia
ulichosema wewe ni probability na alichosema kiba ni proba pia, yaani vyote vina uwezekano wa kutokea kwenye maisha, sasa unaposema sio kweli unakosea coz unamaanisha hiyo scenario haipo, ilibid useme "sio mara zote" (not always the case), japo nadhan hata yeye hajamaanisha mara zote huwa kama hivyo alivyosema
 
Kweli tupu mkuu
 
Mkuu sio Aje tu , ukisikiliza nyimbo za kiba Kama, nakshi nakshi, makmuga , ya karimu mpaka za sasa hiv mwana na cheketua utagundua kiba Ana staili ya peke yake na inafanya mziki wake uwe mtamu zaidi na Nina Imani asilimia kubwa wanaomchukia kiba ukipigwa wimbo wake lazima wainuke au wasipiinuka watatikisa vichwa tu Kama sio kufatisha lyrics ..
 

Mkuu weweuna akili sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…