"Kama alifunga kufuli katikati ya nyeti zake"
"Utepe mwekundu mpaka kwenye nguo zake za ndani"
Huu wimbo una mistari ambayo inafikirisha sana. Napenda sifa za jamaa ila baadae FA anaulizia "kama alikufa kwa ngoma jiuliza alijali nini?
Hakuonekana na binti hakuwahi kuiasi dini.
Mfuasi mzuri wa maadili (lakini alikufa kwa ngoma).
Aliwarudisha waliopotea akawapa tiba mbadala.
Na adui mkubwa wa zinaa (lakini alikufa kwa ngoma).
Najaribu kumjengea picha mshikaji alie kalala ndani ya futi sita.
Namkumbuka mtaani alipokuwa anakatisha.
Na mara kadhaa maskani na washkaji ungemkuta.
Usingedhani ana ngoma machoni alivyokuwa mwema.
Mzuri, mtanashati aliyewaza kabla ya kusema.
Ibilisi wa njaa za mwili daima alimchezea mbali.
Tungi, vicheche, mineli hakuonekana kujali.
Tazama maisha yake hutaliona kosa lake
Kama aliyefunga kufuli kati kati ya nyeti zake.