Aliyefeli hawezi kuwa Mwalimu wako, hatujifunzi kwa waliofeli

Aliyefeli hawezi kuwa Mwalimu wako, hatujifunzi kwa waliofeli

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Mpo salama!

Moja ya kanuni ninayoitumia ni pamoja na kufundishwa na waalimu waliofaulu. Iwe kwenye taaluma, biashara, Siasa, mahusiano, Kiroho, miongoni mwa mambo mengine..

Kamwe usijifunze Kwa Watu waliofeli, mtu aliyefeli asiwe Mwalimu, role model, au mshauri wako. Kikawaida Watu waliofeli hufanikiwa katika mawazo Wakati waliofaulu hufanikiwa katika Matendo yaani Matokeo.

Aliyefaulu anajua kutokufaulu pia. Yaani anajua Pande zote Mbili Kwa sababu kufaulu kunakuja Kwa kufeli au kushindwa mara nyingi.
Wakati aliyefeli anajua kufeli tuu. Hajui kufaulu kukoje. Ameshindwa.

Kabla ya Nuru kulikuwa na Giza. Aliyenuruni hujua yaliyogizani. Lakini aliyegizani hajui yaliyonuruni. Kwa sababu Nuru hufukuza Giza.

Tajiri anaweza kukuambia kuhusu Umaskini Kwa sababu anaujua vizuri kuliko Maskini Mwenyewe. Tajiri anauwezo wa kukueleza utajiri Kwa sababu anauishi. Lakini Maskini hawezi kukueleza utajiri ambao hajawahi kuumiliki, wala hawezi kuuelezea umaskini Kwa namna itakayokufanya uukimbie.

Shuleni waalimu ili wawe waalimu ni lazima wawe walifaulu. Huwezi kuwa Mwalimu bila kuwa umefaulu.
Ikiwa hukufaulu basi utaitwa Mwalimu wa Uongo Kwa sababu unafundisha mambo usiyoyaelewa wala kuyajua.

Wengi husikiliza na kuwafanya Watu walioshindwa kuwa waalimu au washauri wao. Ndio maana hupoteza kujiamini.

Elewa kuwa kushindwa kwako kutategemea uwezo wako Kwa asilimia 50% lakini uwezo wa waalimu wako 50%. Yaani Huko unakojifunzia.

Kabla mtu hujamshauri kuhusu Jambo Fulani jaribu kujiuliza Jambo unalomshauri wewe mwenyewe umelifaulu?
Na Kabla hujaomba ushauri Kwa MTU, jaribu kujiuliza unayemuomba ushauri amefaulu katika Jambo Hilo?

Wanasema huwezi chuma embe kwenye mchungwa. Huwezi chuma ushindi Kwa mtu aliyeshindwa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Maisha hayana kanuni!!
Kuna vitabu vimeandika" how to be rich",kisome Sasa kama utatajirika!!
Nakazia maisha hayana formula
 
Mpo salama!

Moja ya kanuni ninayoitumia ni pamoja na kufundishwa na waalimu waliofaulu. Iwe kwenye taaluma, biashara, Siasa, mahusiano, Kiroho, miongoni mwa mambo mengine..

Kamwe usijifunze Kwa Watu waliofeli, mtu aliyefeli asiwe Mwalimu, role model, au mshauri wako. Kikawaida Watu waliofeli hufanikiwa katika mawazo Wakati waliofaulu hufanikiwa katika Matendo yaani Matokeo.

Aliyefaulu anajua kutokufaulu pia. Yaani anajua Pande zote Mbili Kwa sababu kufaulu kunakuja Kwa kufeli au kushindwa mara nyingi.
Wakati aliyefeli anajua kufeli tuu. Hajui kufaulu kukoje. Ameshindwa.

Kabla ya Nuru kulikuwa na Giza. Aliyenuruni hujua yaliyogizani. Lakini aliyegizani hajui yaliyonuruni. Kwa sababu Nuru hufukuza Giza.

Tajiri anaweza kukuambia kuhusu Umaskini Kwa sababu anaujua vizuri kuliko Maskini Mwenyewe. Tajiri anauwezo wa kukueleza utajiri Kwa sababu anauishi. Lakini Maskini hawezi kukueleza utajiri ambao hajawahi kuumiliki, wala hawezi kuuelezea umaskini Kwa namna itakayokufanya uukimbie.

Shuleni waalimu ili wawe waalimu ni lazima wawe walifaulu. Huwezi kuwa Mwalimu bila kuwa umefaulu.
Ikiwa hukufaulu basi utaitwa Mwalimu wa Uongo Kwa sababu unafundisha mambo usiyoyaelewa wala kuyajua.

Wengi husikiliza na kuwafanya Watu walioshindwa kuwa waalimu au washauri wao. Ndio maana hupoteza kujiamini.

Elewa kuwa kushindwa kwako kutategemea uwezo wako Kwa asilimia 50% lakini uwezo wa waalimu wako 50%. Yaani Huko unakojifunzia.

Kabla mtu hujamshauri kuhusu Jambo Fulani jaribu kujiuliza Jambo unalomshauri wewe mwenyewe umelifaulu?
Na Kabla hujaomba ushauri Kwa MTU, jaribu kujiuliza unayemuomba ushauri amefaulu katika Jambo Hilo?

Wanasema huwezi chuma embe kwenye mchungwa. Huwezi chuma ushindi Kwa mtu aliyeshindwa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kuna watu darasani walikuwa vilaza ila duniani tunawatamani na vidigrii vyetu Yan walifeli!! Hivyo maisha hayana kanuni
 
Mkuu hiyo ni akili ndogo sana unayo oneshwa. Kushinda au kufaulu Kwa jambo kunategemea mazingira mtu aliyomo. Ndiyo maana wanafunzi wanafundishwa sawa darasani na mwalimu mmoja lakini wakipewa mtihani wengine wanafaulu na wengine wanafeli. Hivyo usikatae kupokea ushauri Kwa mtu Kwa dhana kwamba yeye alifeli hicho anacho kushauri. Hivi hujui kuwa Yale maelekezo ambayo kocha wa mpira wa miguu anayowapa wachezaji ili timu ishinde yeye mwenyewe (kocha) akiingia uwanjani kama mchezaji hawezi kuyatekeleza kikamilifu?
 
Mpo salama!

Moja ya kanuni ninayoitumia ni pamoja na kufundishwa na waalimu waliofaulu. Iwe kwenye taaluma, biashara, Siasa, mahusiano, Kiroho, miongoni mwa mambo mengine..

Kamwe usijifunze Kwa Watu waliofeli, mtu aliyefeli asiwe Mwalimu, role model, au mshauri wako. Kikawaida Watu waliofeli hufanikiwa katika mawazo Wakati waliofaulu hufanikiwa katika Matendo yaani Matokeo.

Aliyefaulu anajua kutokufaulu pia. Yaani anajua Pande zote Mbili Kwa sababu kufaulu kunakuja Kwa kufeli au kushindwa mara nyingi.
Wakati aliyefeli anajua kufeli tuu. Hajui kufaulu kukoje. Ameshindwa.

Kabla ya Nuru kulikuwa na Giza. Aliyenuruni hujua yaliyogizani. Lakini aliyegizani hajui yaliyonuruni. Kwa sababu Nuru hufukuza Giza.

Tajiri anaweza kukuambia kuhusu Umaskini Kwa sababu anaujua vizuri kuliko Maskini Mwenyewe. Tajiri anauwezo wa kukueleza utajiri Kwa sababu anauishi. Lakini Maskini hawezi kukueleza utajiri ambao hajawahi kuumiliki, wala hawezi kuuelezea umaskini Kwa namna itakayokufanya uukimbie.

Shuleni waalimu ili wawe waalimu ni lazima wawe walifaulu. Huwezi kuwa Mwalimu bila kuwa umefaulu.
Ikiwa hukufaulu basi utaitwa Mwalimu wa Uongo Kwa sababu unafundisha mambo usiyoyaelewa wala kuyajua.

Wengi husikiliza na kuwafanya Watu walioshindwa kuwa waalimu au washauri wao. Ndio maana hupoteza kujiamini.

Elewa kuwa kushindwa kwako kutategemea uwezo wako Kwa asilimia 50% lakini uwezo wa waalimu wako 50%. Yaani Huko unakojifunzia.

Kabla mtu hujamshauri kuhusu Jambo Fulani jaribu kujiuliza Jambo unalomshauri wewe mwenyewe umelifaulu?
Na Kabla hujaomba ushauri Kwa MTU, jaribu kujiuliza unayemuomba ushauri amefaulu katika Jambo Hilo?

Wanasema huwezi chuma embe kwenye mchungwa. Huwezi chuma ushindi Kwa mtu aliyeshindwa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hivii..!! Kama masikini ana uwezo wa kukuelezea kuhusu umasikini kwa vile anauishi, Huoni kuwa hapo atakufanya ujue namna ya kuukwepa umasikini?? Na ukishaukwepa umasikini, maana yake una utajiri..!! KWA MANTIKI HIYO, HATA MASIKINI TUNAJIFUNZA KWAKE KUUPATA UTAJIRI
 
Kama ni hivyo Drogba asingepaswa kufundishwa na Mourinho au Bekham na wenzake wasingefundishwa na Sir Alex Ferguson... haya maisha yaishi tu kwa kuhakikisha huvunji sheria za Mungu na za jamhuri. Hakuna kanuni ya maisha. Hakuna mjanja au mjinga wa maisha.. sisi wote tunajifunza. Hata siku ya kufa tutajifunza jinsi gani roho inatoka.
 
Watu wa kukaa nao karibu
1. waliofeli na wakajua wapi walifeli,
2. Wapo waliofaulu na wakajua jinsi gani walifaulu

Wasiofaa
1.
walifaulu, wanajua ni vipi walifaulu na hawataki kuonesha njia
2. Waliofeli, wanajua wapi walifeli ila wanataka na wengine wapite hapo wafeli.

wasiolaumiwa
1.
waliofaulu ila hawajui wametoboa vipi
wakuonea huruma
1. Aliefeli na hajui kafeli wapi, just things in mess,
 
Watu wa kukaa nao karibu
1. waliofeli na wakajua wapi walifeli,
2. Wapo waliofaulu na wakajua jinsi gani walifaulu

Wasiofaa
1.
walifaulu, wanajua ni vipi walifaulu na hawataki kuonesha njia
2. Waliofeli, wanajua wapi walifeli ila wanataka na wengine wapite hapo wafeli.

wasiolaumiwa
1.
waliofaulu ila hawajui wametoboa vipi
wakuonea huruma
1. Aliefeli na hajui kafeli wapi, just things in mess,
Sehemu ya hizi hoja zako,zinamwambia mtoa mada kwamba waliofeli wanaweza kuwa walimu wetu,hasa kwa waliofeli na wakajua wapi walifeli
 
mimi nakupinga kwa kiasi fulani.

mambo mengo huwa ni hatua kwa hatua.

unaweza kuona mtu flani kafeli lakini anaweza kukupa maarifa jinsi ya kukwepa kufeli, kukufundisha kidogo alichoambulia, n.k.

Mfano mtu anataka kuwa na biashara kubwa anaweza kwenda kuanza kujifunza kwa wafanyabiashara wa kati waliofeli kuwa wakubwa akafundishwa vya kukwepa ili asipoteze muda sehemu iliyowafelisha
 
Unajifunza haraka kwa waliofeli kuliko kwa waliofaulu. Waliofaulu wengi huwa hawasemi ukweli wote. Hivyo ukiiga bila tahadhari utaingia mkenge.

Lessons learned from failure. Ni kitu inayosaidia kuepuka kurudia kosa ambalo tayari umelifahamu.
 
Kuna mada ukizisoma unaweza Kuta kama umechelewa sana lakini ni vyema ukaishi kwenye chaguzi zako tu it is simple

Maisha yana namna mbili tu.

1.Hofu ya MUNGU, ila usiongozwe na mifumo ya Dini.

2.Imani kwa Mungu.
 
Kuna mada ukizisoma unaweza Kuta kama umechelewa sana lakini ni vyema ukaishi kwenye chaguzi zako tu it is simple

Maisha yana namna mbili tu.

1.Hofu ya MUNGU, ila usiongozwe na mifumo ya Dini.

2.Imani kwa Mungu.
Na kutii sheria za jamhuri maana hizo zitakupeleka jela ukizipuuza.
 
Kuna watu darasani walikuwa vilaza ila duniani tunawatamani na vidigrii vyetu Yan walifeli!! Hivyo maisha hayana kanuni

Kwa hiyo MTU akifaulu mitihani ya shule unadhani ndio kigezo cha kufaulu Maisha?
Au MTU akiwa mzuri kwenye vita unafikiri atakuwa mzuri kwenye mapenzi?
 
Aisee ni kweli kabisa,aliyefeli anahitajika PT akawe mshika bunduki kulinda Bank na kituoni
 
Mpo salama!

Moja ya kanuni ninayoitumia ni pamoja na kufundishwa na waalimu waliofaulu. Iwe kwenye taaluma, biashara, Siasa, mahusiano, Kiroho, miongoni mwa mambo mengine..

Kamwe usijifunze Kwa Watu waliofeli, mtu aliyefeli asiwe Mwalimu, role model, au mshauri wako. Kikawaida Watu waliofeli hufanikiwa katika mawazo Wakati waliofaulu hufanikiwa katika Matendo yaani Matokeo.

Aliyefaulu anajua kutokufaulu pia. Yaani anajua Pande zote Mbili Kwa sababu kufaulu kunakuja Kwa kufeli au kushindwa mara nyingi.
Wakati aliyefeli anajua kufeli tuu. Hajui kufaulu kukoje. Ameshindwa.

Kabla ya Nuru kulikuwa na Giza. Aliyenuruni hujua yaliyogizani. Lakini aliyegizani hajui yaliyonuruni. Kwa sababu Nuru hufukuza Giza.

Tajiri anaweza kukuambia kuhusu Umaskini Kwa sababu anaujua vizuri kuliko Maskini Mwenyewe. Tajiri anauwezo wa kukueleza utajiri Kwa sababu anauishi. Lakini Maskini hawezi kukueleza utajiri ambao hajawahi kuumiliki, wala hawezi kuuelezea umaskini Kwa namna itakayokufanya uukimbie.

Shuleni waalimu ili wawe waalimu ni lazima wawe walifaulu. Huwezi kuwa Mwalimu bila kuwa umefaulu.
Ikiwa hukufaulu basi utaitwa Mwalimu wa Uongo Kwa sababu unafundisha mambo usiyoyaelewa wala kuyajua.

Wengi husikiliza na kuwafanya Watu walioshindwa kuwa waalimu au washauri wao. Ndio maana hupoteza kujiamini.

Elewa kuwa kushindwa kwako kutategemea uwezo wako Kwa asilimia 50% lakini uwezo wa waalimu wako 50%. Yaani Huko unakojifunzia.

Kabla mtu hujamshauri kuhusu Jambo Fulani jaribu kujiuliza Jambo unalomshauri wewe mwenyewe umelifaulu?
Na Kabla hujaomba ushauri Kwa MTU, jaribu kujiuliza unayemuomba ushauri amefaulu katika Jambo Hilo?

Wanasema huwezi chuma embe kwenye mchungwa. Huwezi chuma ushindi Kwa mtu aliyeshindwa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Unakosea Mzee. Mtu hawez kufeli kwenye kila kitu. Na pia hawez kufaulu kwenye kila kitu. Tunategemeana kwa sehem na tunajifunza kila siku popote na kwa yeyote. Otherways uniambie kufaulu ni mpaka ujenge gorofa au kupata pesa kwa upande wako.
 
Back
Top Bottom