Aliyegundua ukoko hivi alikuwa anafikiria nini

Babumawe

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2014
Posts
2,556
Reaction score
2,571
Jamani eeeh kwanza habarini za muda huu
kiukweli tangu nianze kuujua na kuula wali aise hakuna kitu nakikubali kama ukoko, Narudia tena kwa msisitizo hakuna kitu nakikubali kama ukoko sijajua kama nina tatizo au na sitaki kujua.

Yaani tangu nipo mdogo ilikuwa kitu cha mchele kikikaribia kuiva najisogeza jikoni navizia kwanza kile kiukoko cha juujuu kile yani kile ndo kinakuwa introduction nakigonga kile halafu narudi zangu kwenye makochi nasikilizia koko lenyewe lile la chini yaani lile funga kazi. Yani hapo nitazuga zuga nangalia TV ili niwe wamwisho ili nilie kwenye sufuria ili nifanye mchakato wa ukoko.

Halafu ukoko haunaga muda maalumu , mda wowote tu unaweza ukagonga fresh. Usiombe asubuhi sasa uamke na kiporo cha ukoko halafu unafanya kama kukinyunyizia maharage hivi pembeni chai ya rangi tena ukipata chai iliyopikwa na mchaichai yani hapo unaweza ukawa unakula huku unatoa machozi ya furaha.

Sasa jaribuni hii, wali uwe wa nazi halafu chukua ukoko wa juu changanya na koko la chini kisha nyunyuzia chuzi la maharage la nazi halafu njoo na majibu hapa.
 
🀣🀣🀣🀣🀣🀣🀣
 
Alikuwa anamuangalia mzee jengua bahati mbaya akaunguza ubwabwa.
 
Kuna kitu kinaitwa mahaba kiongozi alimarufu (matandu) ukiyatafuna Ni kwarachukwarachu...kongole kwa mgunduzi
 
Wengi watajifanya hawajui hii kitu Ila moyoni mwao wanakubali
Thus why uwa kwangu nawaambia nitachukua mwenyewe msosi msiwe mezani kwenye poti,kumbe nataka nijikwangulie cha chini
 
mi nahisi alipika afu akala kingi
Baadae anakuja kupiga amalizie njaa ikamkaba akaona aonje na ule wa chini
Njaa hiyo mkuuuπŸ˜‚πŸ˜‚
Afu aliegundua sio wakishua
 
🀣🀣 mkuu machozi ya furaha yakoje..?
 
Ukoko siku hizi umekuwa adimu sana sababu watu wanapika wali kwa kutumia rice-cooker
 
kuna ukoko na mahaba...πŸ˜‚πŸ˜‚
Mahaba ni ule ukoko wa juu
sema koko lenyewe kiboko sanaa


Mungu amtunze sana legendi aliyegundua hii kitu
bila kumsahau aliyegundua kiporo cha wali maharage na chai ya rangi... Mungu ambariki huko aliko
 
Ukoko wa ugali na mchuzi wa nyama mtamu Sana

Ukoko wa wali na mchuzi wa maharage unajiona unamiliki dunia na vilivyomo

Ukoko wa wali ukiweka chai ya rangi iliyokolea sukari utapenda kitachotokea unavyokula

Ukoko hoyeeeeee
 
Ukoko wa ugali na mchuzi wa nyama mtamu Sana

Ukoko wa wali na mchuzi wa maharage unajiona unamiliki dunia na vilivyomo

Ukoko wa wali ukiweka chai ya rangi iliyokolea sukari utapenda kitachotokea unavyokula

Ukoko hoyeeeeee
Acha kabisa
 
kuna ukoko na mahaba...[emoji23][emoji23]
Mahaba ni ule ukoko wa juu
sema koko lenyewe kiboko sanaa


Mungu amtunze sana legendi aliyegundua hii kitu
bila kumsahau aliyegundua kiporo cha wali maharage na chai ya rangi... Mungu ambariki huko aliko
Amen
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…