Aliyeisababishia serekali hasara ya 1.7bil azawadiwa transfer

Aliyeisababishia serekali hasara ya 1.7bil azawadiwa transfer

August

JF-Expert Member
Joined
Jun 18, 2007
Posts
9,327
Reaction score
5,206
12/24/2008
DED aliyesimamishwa Ilala aibukia Shinyanga
Zulfa Mfinanga

ALIYEKUWA mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Ilala, John Lubuva, ambaye alisimamishwa kazi kutokana na kuhusishwa na zoezi la bomoabomoa iliyofanyika Tabata Dampo jijini Dar es Salaam, amehamishiwa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Vijijini.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana na kuthibitishwa na mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Amos Mshandete zinasema kuwa Lubuva ameanza kazi mwezi huu.

Mshandete, aliyesema kuwa hafahamu chochote kuhusu sababu za mabadiliko ya uongozi katika wilaya hiyo, alisema Lubuva amefika wilayani hapo kuchukua nafasi ya Pius Affa.

"Mimi, kama mwenyekiti wa halmashauri hii, ninachofahamu ni kwamba niliitwa na mkurugenzi aliyehamishwa Pius Affa akanieleza kuwa anahamishiwa mkoa Arusha na nafasi yake itachukuliwa na mkurugenzi kutoka Dar es Salaam ambaye ni John Lubuva," alisema Mshandete na kuongeza:

"Zaidi ya kumpokea sijui kingine chochote na maelezo mengine ya ziada yanaweza kutolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi)."

Waziri wa TAMISEMI, Celina Kombani alilithibitishia gazeti hili jana kuwa Lubuva amehamishiwa Shinyanga kuendelea na wadhifa wake ule ule wa mkurugenzi Mtendaji.

Alisema pamoja na matatizo yaliyomkuta jijini Dar es Salaam alipokuwa mkurugenzi wa manispaa ya Ilala, Lubuva bado ana sifa za kuendelea na wadhifa wake kwa kuwa kosa hilo ni la kwanza.

"Taarifa za Lubuva kuhamishiwa Shinyanga ni za kweli tena ukweli mtupu yuko huko na bado ni mkurugenzi mtendaji. Tumefikia hatua hiyo baada ya kufuata taratibu zote za kazi za kumfukuza mtu baada ya kufanya makosa zaidi ya mara tatu," alisema Kombani na kuendelea:

"Kumfukuza mtu ni hatua ya mwisho baada ya kumpa karipio na karipio kali. Hili ni kosa la kwanza kwa John Lubuva hivyo amepewa karipio lakini pia amepewa kuiongoza Shinyanga kwa kuwa wilaya hiyo ni ndogo ikilinganishwa na Ilala."

Alisema uwepo wa Lubuva Shinyanga ni sehemu ya karipio na serikali inaamini kuwa mtendaji huyo atabalika na kuwa bora zaidi.

Februari mwaka huu Lubuva alisimamishwa kazi kutokana na kuhusishwa na ubomoaji haramu wa nyumba za wakazi wa Tabata Dampo akiwa mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Ilala

Kusimamishwa kwa Lubuva kulienda sambamba na serikali kutoa kifuta machozi cha Sh1.7 bilioni kwa wakazi hao ambao nyumba zao zaidi ya 88 zilibomolewa katiak zoezi hilo

Serikali ilikubali kuingia gharama hiyo kutokana na zembe na ukiukwaji wa taratibu na kanuni za notisi kuhusu ubomoaji nyumba unaohusishwa na ufisadi.

Fedha hizo zilitumika kulipa Sh20 milioni kila nyumba iliyobomolewa na kutoa kiwanja bure eneo Buyuni, Wilaya ya Ilala, kwa kila mkazi.

Akisoma Tamko la Serikali jijini Dar es Salaam jana kutokana na matokeo ya Tume Maalumu ya Kuchunguza Ubomoaji wa Nyumba hizo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Stephen Wassira alisema uamuzi huo wa serikali unatokana na kubaini kwamba ubomoaji huo haukuzingatia uamuzi wa Baraza la Ardhi.

Wassira alifafanua kwamba uamuzi wa Baraza la Ardhi ulitaka Halmashauri (Ilala) iangalie taratibu zilizopo katika kuwaondoa wavamizi katika eneo husika.

Wassira alitaja taratibu hizo ambazo zilipaswa kuzingatiwa kwamba ni kufikisha dhamira hiyo ya ubomoaji kwanza katika vikao vya juu vya timu ya menejimenti na vikao vya Baraza la Madiwani.

Wassira aliongeza kuwa taratibu nyingine zilizokiukwa ni wananchi kutoshirikishwa katika azma ya ubomoaji huo, kitu ambacho ni kinyume na misingi na kanuni za utawala bora huku kukiwa na harufu ya rushwa.

"Kulikuwepo kwa viashiria vya vitendo vya rushwa japo haikuweza kuthibitishwa," alisema.

Alisema taratibu zinataka notisi ya ubomoaji wa nyumba za makazi uwe siku 30, lakini katika ubomoaji wa Tabata notisi ilitolewa Febrari 27 na utekelezaji ukaanza Februari 29, yaani siku mbili baadaye.

Alisema uamuzi wa serikali kulipa fidia hiyo, haukuzingatia kama wakazi hao wanaishi kihalali au haramu bali umetokana na kubaini ukiukwaji wa taratibu ambazo zilitokana na maafisa wake kushindwa kuzisimamia.

Waziri Wassira aliweka bayana msimamo wa serikali kwamba, malipo hayo hayahusiani na nyumba ambazo hazijabomolewa kwani wakazi hao hadi sasa wamefungua kesi Mahakama Kuu kupinga kuondolewa katika eneo hilo.
 
Kila jambo linawezekana katika Tanzania yetu.Mtu akiboronga huku anahamishiwa kule.
 
12/24/2008
DED aliyesimamishwa Ilala aibukia Shinyanga
Zulfa Mfinanga

Kombani has made clear kwamba Shinyanga si mahala pa kupelekwa watu wa maana bali wabovu .Watu wa halmashauri ya Shinyanga hawastahili mazuri toka katika Tanzania hii bali mabaya na wamesha wekwa pembeni katika maswal yote kuanzia maendeleo nk .Ni wakati sasa wao kuamua kuwapa wapinzania maana kwa uwazi CCM na Kombani wamesha sema sauti yao .Hii ndiyo Tanzania
 
Kombani has made clear kwamba Shinyanga si mahala pa kupelekwa watu wa maana bali wabovu .Watu wa halmashauri ya Shinyanga hawastahili mazuri toka katika Tanzania hii bali mabaya na wamesha wekwa pembeni katika maswal yote kuanzia maendeleo nk .Ni wakati sasa wao kuamua kuwapa wapinzania maana kwa uwazi CCM na Kombani wamesha sema sauti yao .Hii ndiyo Tanzania


Lunyungu kwa ku spin mambo tu hujambo! tena unasema kwa kujiamini kabisa kwa Kombani has made clear!

Thats the beauty of JF
 
hUU NI MTINDO TULIOUZOELEA. MWENZETU LAZIMA TUMSITIRI.
 
Nasikia Shinyanga hata ndege hupita makalio yao yako juu ili wasiache kumbukumbu yoyote hapo maana kuacha hata kinyesi Shinyanga ni soo kubwa. Na kama huamini basi huo ni mfano wazi.
Hii inanikumbusha jamaa yangu mmoja Mzambia aliyekuwa akisema kuwa hawa Mapadri wa Ulaya, mara nyingi waki-mess up huko kwao Ulaya basi wanapewa adhabu ya kupelekwa Africa, Latina America, nk yaani Mabonde kwinama. Sasa uliza hawa huwa ni watu gani? Mara nyingi ni wale waliokuwa wakiBAKA new comers huko kanisani kwao au kuwa na Nyumba ndogo ingawa watakuwa wanasema wao ni Yesu tu. Sasa ona Kibaka Padri hili likija tuseme Shinyanga, si litaanza kubaka VINGOSHA vyetu AKA vidume vya mbegu? Ningelikuwa natoka Shinyanga ningelihisi kuwa NIMEBAKWA tayari na huyu Mkurugenzi.
Huyu jamaa akileta UFISADI wake huko Shinyanga hasa kwenye machimbo ambako naona tayari anakupigia mahesabu akahamishe watu kwa nguvu, basi WAMCHUNE kipande cha ngonzi na hiyo waiponde dawa ya kufukuza FISADI Shinyanga.
 
Nasikia Shinyanga hata ndege hupita makalio yao yako juu ili wasiache kumbukumbu yoyote hapo maana kuacha hata kinyesi Shinyanga ni soo kubwa. Na kama huamini basi huo ni mfano wazi.
Hii inanikumbusha jamaa yangu mmoja Mzambia aliyekuwa akisema kuwa hawa Mapadri wa Ulaya, mara nyingi waki-mess up huko kwao Ulaya basi wanapewa adhabu ya kupelekwa Africa, Latina America, nk yaani Mabonde kwinama. Sasa uliza hawa huwa ni watu gani? Mara nyingi ni wale waliokuwa wakiBAKA new comers huko kanisani kwao au kuwa na Nyumba ndogo ingawa watakuwa wanasema wao ni Yesu tu. Sasa ona Kibaka Padri hili likija tuseme Shinyanga, si litaanza kubaka VINGOSHA vyetu AKA vidume vya mbegu? Ningelikuwa natoka Shinyanga ningelihisi kuwa NIMEBAKWA tayari na huyu Mkurugenzi.
Huyu jamaa akileta UFISADI wake huko Shinyanga hasa kwenye machimbo ambako naona tayari anakupigia mahesabu akahamishe watu kwa nguvu, basi WAMCHUNE kipande cha ngonzi na hiyo waiponde dawa ya kufukuza FISADI Shinyanga.

Kidogo kidogo tunatoka kweny mada.

Simo!
 
Jambo hili kwa nchi yetu inawezekana sana tu. Bado tunalindani. Manake aingii akilini kwamba karipio ni kubadilishiwa wilaya lakini cheo kubaki pale pale.
Labda ni mkakati wao wa kumuandaa kwa kuwaondoa watu wengine kwenye makazi yao ili kupisha wanyonyaji wa dhahabu zetu za shinyanga
 
Nasikia Shinyanga hata ndege hupita makalio yao yako juu ili wasiache kumbukumbu yoyote hapo maana kuacha hata kinyesi Shinyanga ni soo kubwa. Na kama huamini basi huo ni mfano wazi.
Hii inanikumbusha jamaa yangu mmoja Mzambia aliyekuwa akisema kuwa hawa Mapadri wa Ulaya, mara nyingi waki-mess up huko kwao Ulaya basi wanapewa adhabu ya kupelekwa Africa, Latina America, nk yaani Mabonde kwinama. Sasa uliza hawa huwa ni watu gani? Mara nyingi ni wale waliokuwa wakiBAKA new comers huko kanisani kwao au kuwa na Nyumba ndogo ingawa watakuwa wanasema wao ni Yesu tu. Sasa ona Kibaka Padri hili likija tuseme Shinyanga, si litaanza kubaka VINGOSHA vyetu AKA vidume vya mbegu? Ningelikuwa natoka Shinyanga ningelihisi kuwa NIMEBAKWA tayari na huyu Mkurugenzi.
Huyu jamaa akileta UFISADI wake huko Shinyanga hasa kwenye machimbo ambako naona tayari anakupigia mahesabu akahamishe watu kwa nguvu, basi WAMCHUNE kipande cha ngonzi na hiyo waiponde dawa ya kufukuza FISADI Shinyanga.


Achana na myth za ajabu ajabu ndugu yangu.Una uthibitisho gani wa hiyo kauli ya jamaa yako kuwa mapadri wanaopelekwa afrika na latin america ni wabakaji au wametenda maovu kwenye nchi zao?
JF inasomwa na watu wa rika tofauti na uelewa tofauti,hivyo tufanye utafiti wa hoja zetu kwanza kabla ya kupost vinginevyo tukiendekeza hadithi za kwenye vijiwe vya kahawa tutakuwa tunapotosha watu hapa!
 
Huyo mama ameniacha hoi na hizo hatua kabla ya kumfuta mtu kazi.Yani mtu akiiba mamilioni anapewa karipio,safari ya pili akila mabilioni wanampa karipio kali,akiiba mara ya tatu ndiyo watamfuta kazi!
bongo kweli tambarare!!!
 
Achana na myth za ajabu ajabu ndugu yangu.Una uthibitisho gani wa hiyo kauli ya jamaa yako kuwa mapadri wanaopelekwa afrika na latin america ni wabakaji au wametenda maovu kwenye nchi zao?
JF inasomwa na watu wa rika tofauti na uelewa tofauti,hivyo tufanye utafiti wa hoja zetu kwanza kabla ya kupost vinginevyo tukiendekeza hadithi za kwenye vijiwe vya kahawa tutakuwa tunapotosha watu hapa!

Mtarajiwa,
Nimewahi kuyasikia haya maneno kutoka kwa Father mmoja ambaye alipokosana na boss wake wakamlima Ukraine ndani kabisa huko vijijini kama adhabu. Hii inatokea sana tu. Wengi wenye makosa kama haya hufichwa na baadaye kimya kimya kupelekwa mbali sana kutoka Ulaya kama adhabu na kuwaweka mbali na maeneo waliyofanyia hayo makosa.
Ila sidhani unafikiri nilivyosema kuwa wanapelekwa basi ina maana ni wote. Hiyo si kweli. Wapo wazuri na wabaya. Ila siyo siri kuwa sehemu wanazokwenda zinategemea sana unamfahamu nani kule juu au umefanya kitu gani kwa watu wa juu au sehemu unayoishi.
Pia juu ya maovu yanayofanywa na Mapadri kweni ni siri? Mbona Australia, USA, nk ilibidi Vatican wakubali walipe fidia kwa ajili ya ubakaji vitoto vya kiume uliofanywa na Mapadre? Unafikiri wakitoka huko hupelekwa wapi? Third world au First world? Mtarajiwa dunia hii hamna siri tena.
BBC NEWS | Americas | Timeline: US Church sex scandal

Ila kama alivyosema Masatu, issue hapa ni Shinyanga, hivyo tuache hii habari ife na turude kwa Mkurugenzi wetu waliyemhamishia Shinyanga ili nako aibe na wamkaripie zaidi na abakize mara ya mwisho ambazo ataiba ili ajiwekee Kiinua Mgongo chake kabla ya KUFUKUZWA kazi.
 
Ila kama alivyosema Masatu, issue hapa ni Shinyanga, hivyo tuache hii habari ife na turude kwa Mkurugenzi wetu waliyemhamishia Shinyanga ili nako aibe na wamkaripie zaidi na abakize mara ya mwisho ambazo ataiba ili ajiwekee Kiinua Mgongo chake kabla ya KUFUKUZWA kazi.

Swadakta!!!!
Si mnamkumbuka yule mama CHUWA aliyekuwa OCD Kilosa mwanzoni mwa 2000 baada ya kushindwa kudhibiti mauaji/mapigano kati ya wakulima na wafugaji wilayani Kilosa alisimamishwa kazi like Lubuva.(sijui yuko wapi sasahivi).
Baadae akaibukia Ilala akiwa OCD pale msimbazi.Mnakumbuka kilichotokea pale msimbazi police????kama sijasahau milioni 24 ziliibiwa bila ofisi kuvunjwa, halafu sikumbuki ile kesi iliishia wapi.Kwahiyo hata huyu Lubuva nae tutegemee aendeshe operesheni ya kuwabomolea shemeji zangu pale shinyanga ili kuwapisha wakwapuaji a.k.a wawekezaji ili apewe karipio kali!!!

Nimegundua kuwa hii ndiyo staili ya uongozi wa JK, mtu anavurunda lakini sharti apewe karipio mara ya kwanza, akiharibu tena anapewa karipio kali na akiharibu mara ya tatu ndipo anafukuzwa.Naamini sasa kuwa ndio maana serikali imeamua kuyapuuza mapendekezo ya Bunge kuhusu ufisadi wa richmond ili kukidhi utaratibu wao wa makaripio matatu!!!!!
 
Let us be fair on this! kwani Lubuva alikuwa na kosa gani? If you will tell me he was wrong kwa kuvuunja nyumba za watu waliovamia kiwanja cha mtu bila idhini basi Serikali nayo ikiri kuwa ilifanya kosa kuvunja nyumba za wananchi wa Ubungo along Morogoro road n awahusika wawajibike. Lubuva alikuwa mwafirika wa siasa za Serikali kujikomba kwa wananchi wa tabata. Ndo maana baadaye wakaambiwa wasiendelee kuishi pale waende kinyerezi kwenye viwanja vipya. Kwangu Lubuva hana kosa la kustahili kufukuzwa kazi lakini kutokana na ajali hiyo angepelekwa wizarani siyo Halmashauri tena kwani sasa atakosa ujasiri katika maamuzi.
 
sasa aliposimamishwa kazi huyo Lubuva si kulikuwa na maana alikuwa anachunguzwa? sasa imekuwaje amerudishwa kimya kimya? ameenda jimbo la mbunge gani? au na mbunge naye amemkubali huyu jamaa?
 
sasa aliposimamishwa kazi huyo Lubuva si kulikuwa na maana alikuwa anachunguzwa? sasa imekuwaje amerudishwa kimya kimya? ameenda jimbo la mbunge gani? au na mbunge naye amemkubali huyu jamaa?

sasa si inamaana uchunguzi umekamilika na imeonekana hana kosa?
 
sasa si inamaana uchunguzi umekamilika na imeonekana hana kosa?

Bwana Nziku,

uchunguzi wapi umefanyika? zaidi ya kuita vyombo vya habari kwa jazba na kutangaza kwamba Lubuva amesimamishwa kazi. wanajua kwamba hakuna kilichofanyika ndo maana wamemteua kimya kimya. Hivi Tanzania hatuna FOIA? I mean 'Freedom of Information Act". I am sure kuna madudu mengi huwa yanafanyika katika tume na chunguzi nyingi za serikali.

Ukifatilia kesi ya watu wa tabata dampo, huyo Lubuva kuweza kurudi kwenye public office ilikuwa ni kazi kweli kweli. Wakati wa Nyerere walikuwa wanaachishwa kazi kwa manufaa ya umma, awamu nyingine unapigwa pande la ulaji sehemu nyingine.
 
Mtarajiwa,
Nimewahi kuyasikia haya maneno kutoka kwa Father mmoja ambaye alipokosana na boss wake wakamlima Ukraine ndani kabisa huko vijijini kama adhabu. Hii inatokea sana tu. Wengi wenye makosa kama haya hufichwa na baadaye kimya kimya kupelekwa mbali sana kutoka Ulaya kama adhabu na kuwaweka mbali na maeneo waliyofanyia hayo makosa.
Ila sidhani unafikiri nilivyosema kuwa wanapelekwa basi ina maana ni wote. Hiyo si kweli. Wapo wazuri na wabaya. Ila siyo siri kuwa sehemu wanazokwenda zinategemea sana unamfahamu nani kule juu au umefanya kitu gani kwa watu wa juu au sehemu unayoishi.
Pia juu ya maovu yanayofanywa na Mapadri kweni ni siri? Mbona Australia, USA, nk ilibidi Vatican wakubali walipe fidia kwa ajili ya ubakaji vitoto vya kiume uliofanywa na Mapadre? Unafikiri wakitoka huko hupelekwa wapi? Third world au First world? Mtarajiwa dunia hii hamna siri tena.
BBC NEWS | Americas | Timeline: US Church sex scandal

Ila kama alivyosema Masatu, issue hapa ni Shinyanga, hivyo tuache hii habari ife na turude kwa Mkurugenzi wetu waliyemhamishia Shinyanga ili nako aibe na wamkaripie zaidi na abakize mara ya mwisho ambazo ataiba ili ajiwekee Kiinua Mgongo chake kabla ya KUFUKUZWA kazi.


Tuwekane sawa kabla hatujaendelea na mada iliyopo.
Ulisema umesikia kwa jamaa yako mzambia.Sasa unasema uliwahi kusikia kutoka kwa father mmoja.anyway,huyo father alipelekwa ukraine(ulaya) na siyo afrika na latin america kama ulivyodai mwanzoni tena baada ya kukosana na boss wake na si kwa kubaka kama ulivyodai mwanzoni.
Umeweka link.Nilidhani ingeelezea hiyo mikasa ya mapadri wabakaji wa ulaya kupelekwa afrika na latin america kama ulivyodai badala yake imeelezea maovu yanayofanywa na mapadri wa marekani na si ulaya kama ulivyodai,tena hakuna popote waliposema hao mapadri baada ya hayo maovu walihamishiwa africa na latin america.
Halafu kama mapadri wanaofanya maovu ulaya huwa wanapelekwa afrika na latin america na mapadri wanaobaka afrika na latin america huwa wanapelekwa wapi?
Madai yako hayana ukweli wowote ni hadithi tu za mitaani.Kwa kawaida mapadri wa ulaya huwa wanapelekwa Africa to help with a shortage of pastoral experience and teaching in theological colleges.
West sasa wana uhaba wa mapadri na vatican ina mpango wa kuimport mapadri kutoka afrika,kwahiyo utaona hapo kuwa afrika haina shortage ya mapadri na hivyo kuwafanya watupiwe mapadri waovu kutoka ulaya.
 
SIKONGE,
Lugha yako imekuwa kali sana, huyu Lubuva nafikiri wanaojua vizuri ile issue ya Tabata dampo watakuwa wanasema Mungu amejibu maombi na kuwa haki siku zote itasimama na kuwa Mungu humtetea mtu aliyeonewa. Ninafahamu vizuri sana kuwa huyu bwana alionewa na alitolewa kafara na jamaa wawili (mmoja toka serikalini na mwnigine toka Chama tawala? kwa sababubinafsi tu. Ni kwamba haw jamaa walikuwa wamtafuta huyu bwana siku nyingi wakaitumia hii issue kuhalalisha jambo lao.

Namtetea Lubuva kwa issue hii tu ya tabata dampo, kama ana mambo mengine mimi sijui.
Japo umeshushwa cheo ( from manispaa to that level) lakini naamini Bwana amekupigania.

Chapa kazi, kichwa Lubuva, uwezo wako tunauhitaji, Shinyanga mmelamba dume
 
SIKONGE,
Lugha yako imekuwa kali sana, huyu Lubuva nafikiri wanaojua vizuri ile issue ya Tabata dampo watakuwa wanasema Mungu amejibu maombi na kuwa haki siku zote itasimama na kuwa Mungu humtetea mtu aliyeonewa. Ninafahamu vizuri sana kuwa huyu bwana alionewa na alitolewa kafara na jamaa wawili (mmoja toka serikalini na mwnigine toka Chama tawala? kwa sababubinafsi tu. Ni kwamba haw jamaa walikuwa wamtafuta huyu bwana siku nyingi wakaitumia hii issue kuhalalisha jambo lao.
Namtetea Lubuva kwa issue hii tu ya tabata dampo, kama ana mambo mengine mimi sijui.
Japo umeshushwa cheo ( from manispaa to that level) lakini naamini Bwana amekupigania.

Chapa kazi, kichwa Lubuva, uwezo wako tunauhitaji, Shinyanga mmelamba dume

Hivi bongo ukionewa huna pa kujitetea we unakubali tu matokeo??

Namshauri kama ni uonevu kweli avifate vyombo husika ili asafishe jina lake kwani damage iliyo tokea ni kubwa sana, hata huko aliko pelekwa shinyanga kwa technologia hii ya habari watamuona hafai kabisa na huenda akakosa ushirikiano na hivyo kushindwa kutimiza majukumu yake.
 
Back
Top Bottom