Aliyeisababishia serekali hasara ya 1.7bil azawadiwa transfer

August

JF-Expert Member
Joined
Jun 18, 2007
Posts
9,327
Reaction score
5,206
12/24/2008
DED aliyesimamishwa Ilala aibukia Shinyanga
Zulfa Mfinanga

 
Kila jambo linawezekana katika Tanzania yetu.Mtu akiboronga huku anahamishiwa kule.
 
12/24/2008
DED aliyesimamishwa Ilala aibukia Shinyanga
Zulfa Mfinanga

Kombani has made clear kwamba Shinyanga si mahala pa kupelekwa watu wa maana bali wabovu .Watu wa halmashauri ya Shinyanga hawastahili mazuri toka katika Tanzania hii bali mabaya na wamesha wekwa pembeni katika maswal yote kuanzia maendeleo nk .Ni wakati sasa wao kuamua kuwapa wapinzania maana kwa uwazi CCM na Kombani wamesha sema sauti yao .Hii ndiyo Tanzania
 


Lunyungu kwa ku spin mambo tu hujambo! tena unasema kwa kujiamini kabisa kwa Kombani has made clear!

Thats the beauty of JF
 
hUU NI MTINDO TULIOUZOELEA. MWENZETU LAZIMA TUMSITIRI.
 
Nasikia Shinyanga hata ndege hupita makalio yao yako juu ili wasiache kumbukumbu yoyote hapo maana kuacha hata kinyesi Shinyanga ni soo kubwa. Na kama huamini basi huo ni mfano wazi.
Hii inanikumbusha jamaa yangu mmoja Mzambia aliyekuwa akisema kuwa hawa Mapadri wa Ulaya, mara nyingi waki-mess up huko kwao Ulaya basi wanapewa adhabu ya kupelekwa Africa, Latina America, nk yaani Mabonde kwinama. Sasa uliza hawa huwa ni watu gani? Mara nyingi ni wale waliokuwa wakiBAKA new comers huko kanisani kwao au kuwa na Nyumba ndogo ingawa watakuwa wanasema wao ni Yesu tu. Sasa ona Kibaka Padri hili likija tuseme Shinyanga, si litaanza kubaka VINGOSHA vyetu AKA vidume vya mbegu? Ningelikuwa natoka Shinyanga ningelihisi kuwa NIMEBAKWA tayari na huyu Mkurugenzi.
Huyu jamaa akileta UFISADI wake huko Shinyanga hasa kwenye machimbo ambako naona tayari anakupigia mahesabu akahamishe watu kwa nguvu, basi WAMCHUNE kipande cha ngonzi na hiyo waiponde dawa ya kufukuza FISADI Shinyanga.
 

Kidogo kidogo tunatoka kweny mada.

Simo!
 
Jambo hili kwa nchi yetu inawezekana sana tu. Bado tunalindani. Manake aingii akilini kwamba karipio ni kubadilishiwa wilaya lakini cheo kubaki pale pale.
Labda ni mkakati wao wa kumuandaa kwa kuwaondoa watu wengine kwenye makazi yao ili kupisha wanyonyaji wa dhahabu zetu za shinyanga
 


Achana na myth za ajabu ajabu ndugu yangu.Una uthibitisho gani wa hiyo kauli ya jamaa yako kuwa mapadri wanaopelekwa afrika na latin america ni wabakaji au wametenda maovu kwenye nchi zao?
JF inasomwa na watu wa rika tofauti na uelewa tofauti,hivyo tufanye utafiti wa hoja zetu kwanza kabla ya kupost vinginevyo tukiendekeza hadithi za kwenye vijiwe vya kahawa tutakuwa tunapotosha watu hapa!
 
Huyo mama ameniacha hoi na hizo hatua kabla ya kumfuta mtu kazi.Yani mtu akiiba mamilioni anapewa karipio,safari ya pili akila mabilioni wanampa karipio kali,akiiba mara ya tatu ndiyo watamfuta kazi!
bongo kweli tambarare!!!
 

Mtarajiwa,
Nimewahi kuyasikia haya maneno kutoka kwa Father mmoja ambaye alipokosana na boss wake wakamlima Ukraine ndani kabisa huko vijijini kama adhabu. Hii inatokea sana tu. Wengi wenye makosa kama haya hufichwa na baadaye kimya kimya kupelekwa mbali sana kutoka Ulaya kama adhabu na kuwaweka mbali na maeneo waliyofanyia hayo makosa.
Ila sidhani unafikiri nilivyosema kuwa wanapelekwa basi ina maana ni wote. Hiyo si kweli. Wapo wazuri na wabaya. Ila siyo siri kuwa sehemu wanazokwenda zinategemea sana unamfahamu nani kule juu au umefanya kitu gani kwa watu wa juu au sehemu unayoishi.
Pia juu ya maovu yanayofanywa na Mapadri kweni ni siri? Mbona Australia, USA, nk ilibidi Vatican wakubali walipe fidia kwa ajili ya ubakaji vitoto vya kiume uliofanywa na Mapadre? Unafikiri wakitoka huko hupelekwa wapi? Third world au First world? Mtarajiwa dunia hii hamna siri tena.
BBC NEWS | Americas | Timeline: US Church sex scandal

Ila kama alivyosema Masatu, issue hapa ni Shinyanga, hivyo tuache hii habari ife na turude kwa Mkurugenzi wetu waliyemhamishia Shinyanga ili nako aibe na wamkaripie zaidi na abakize mara ya mwisho ambazo ataiba ili ajiwekee Kiinua Mgongo chake kabla ya KUFUKUZWA kazi.
 

Swadakta!!!!
Si mnamkumbuka yule mama CHUWA aliyekuwa OCD Kilosa mwanzoni mwa 2000 baada ya kushindwa kudhibiti mauaji/mapigano kati ya wakulima na wafugaji wilayani Kilosa alisimamishwa kazi like Lubuva.(sijui yuko wapi sasahivi).
Baadae akaibukia Ilala akiwa OCD pale msimbazi.Mnakumbuka kilichotokea pale msimbazi police????kama sijasahau milioni 24 ziliibiwa bila ofisi kuvunjwa, halafu sikumbuki ile kesi iliishia wapi.Kwahiyo hata huyu Lubuva nae tutegemee aendeshe operesheni ya kuwabomolea shemeji zangu pale shinyanga ili kuwapisha wakwapuaji a.k.a wawekezaji ili apewe karipio kali!!!

Nimegundua kuwa hii ndiyo staili ya uongozi wa JK, mtu anavurunda lakini sharti apewe karipio mara ya kwanza, akiharibu tena anapewa karipio kali na akiharibu mara ya tatu ndipo anafukuzwa.Naamini sasa kuwa ndio maana serikali imeamua kuyapuuza mapendekezo ya Bunge kuhusu ufisadi wa richmond ili kukidhi utaratibu wao wa makaripio matatu!!!!!
 
Let us be fair on this! kwani Lubuva alikuwa na kosa gani? If you will tell me he was wrong kwa kuvuunja nyumba za watu waliovamia kiwanja cha mtu bila idhini basi Serikali nayo ikiri kuwa ilifanya kosa kuvunja nyumba za wananchi wa Ubungo along Morogoro road n awahusika wawajibike. Lubuva alikuwa mwafirika wa siasa za Serikali kujikomba kwa wananchi wa tabata. Ndo maana baadaye wakaambiwa wasiendelee kuishi pale waende kinyerezi kwenye viwanja vipya. Kwangu Lubuva hana kosa la kustahili kufukuzwa kazi lakini kutokana na ajali hiyo angepelekwa wizarani siyo Halmashauri tena kwani sasa atakosa ujasiri katika maamuzi.
 
sasa aliposimamishwa kazi huyo Lubuva si kulikuwa na maana alikuwa anachunguzwa? sasa imekuwaje amerudishwa kimya kimya? ameenda jimbo la mbunge gani? au na mbunge naye amemkubali huyu jamaa?
 
sasa aliposimamishwa kazi huyo Lubuva si kulikuwa na maana alikuwa anachunguzwa? sasa imekuwaje amerudishwa kimya kimya? ameenda jimbo la mbunge gani? au na mbunge naye amemkubali huyu jamaa?

sasa si inamaana uchunguzi umekamilika na imeonekana hana kosa?
 
sasa si inamaana uchunguzi umekamilika na imeonekana hana kosa?

Bwana Nziku,

uchunguzi wapi umefanyika? zaidi ya kuita vyombo vya habari kwa jazba na kutangaza kwamba Lubuva amesimamishwa kazi. wanajua kwamba hakuna kilichofanyika ndo maana wamemteua kimya kimya. Hivi Tanzania hatuna FOIA? I mean 'Freedom of Information Act". I am sure kuna madudu mengi huwa yanafanyika katika tume na chunguzi nyingi za serikali.

Ukifatilia kesi ya watu wa tabata dampo, huyo Lubuva kuweza kurudi kwenye public office ilikuwa ni kazi kweli kweli. Wakati wa Nyerere walikuwa wanaachishwa kazi kwa manufaa ya umma, awamu nyingine unapigwa pande la ulaji sehemu nyingine.
 


Tuwekane sawa kabla hatujaendelea na mada iliyopo.
Ulisema umesikia kwa jamaa yako mzambia.Sasa unasema uliwahi kusikia kutoka kwa father mmoja.anyway,huyo father alipelekwa ukraine(ulaya) na siyo afrika na latin america kama ulivyodai mwanzoni tena baada ya kukosana na boss wake na si kwa kubaka kama ulivyodai mwanzoni.
Umeweka link.Nilidhani ingeelezea hiyo mikasa ya mapadri wabakaji wa ulaya kupelekwa afrika na latin america kama ulivyodai badala yake imeelezea maovu yanayofanywa na mapadri wa marekani na si ulaya kama ulivyodai,tena hakuna popote waliposema hao mapadri baada ya hayo maovu walihamishiwa africa na latin america.
Halafu kama mapadri wanaofanya maovu ulaya huwa wanapelekwa afrika na latin america na mapadri wanaobaka afrika na latin america huwa wanapelekwa wapi?
Madai yako hayana ukweli wowote ni hadithi tu za mitaani.Kwa kawaida mapadri wa ulaya huwa wanapelekwa Africa to help with a shortage of pastoral experience and teaching in theological colleges.
West sasa wana uhaba wa mapadri na vatican ina mpango wa kuimport mapadri kutoka afrika,kwahiyo utaona hapo kuwa afrika haina shortage ya mapadri na hivyo kuwafanya watupiwe mapadri waovu kutoka ulaya.
 
SIKONGE,
Lugha yako imekuwa kali sana, huyu Lubuva nafikiri wanaojua vizuri ile issue ya Tabata dampo watakuwa wanasema Mungu amejibu maombi na kuwa haki siku zote itasimama na kuwa Mungu humtetea mtu aliyeonewa. Ninafahamu vizuri sana kuwa huyu bwana alionewa na alitolewa kafara na jamaa wawili (mmoja toka serikalini na mwnigine toka Chama tawala? kwa sababubinafsi tu. Ni kwamba haw jamaa walikuwa wamtafuta huyu bwana siku nyingi wakaitumia hii issue kuhalalisha jambo lao.

Namtetea Lubuva kwa issue hii tu ya tabata dampo, kama ana mambo mengine mimi sijui.
Japo umeshushwa cheo ( from manispaa to that level) lakini naamini Bwana amekupigania.

Chapa kazi, kichwa Lubuva, uwezo wako tunauhitaji, Shinyanga mmelamba dume
 

Hivi bongo ukionewa huna pa kujitetea we unakubali tu matokeo??

Namshauri kama ni uonevu kweli avifate vyombo husika ili asafishe jina lake kwani damage iliyo tokea ni kubwa sana, hata huko aliko pelekwa shinyanga kwa technologia hii ya habari watamuona hafai kabisa na huenda akakosa ushirikiano na hivyo kushindwa kutimiza majukumu yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…