Aliyekuwa askofu Konde aondolewa wakfu. Fimbo, msalaba na pete yake vyaondolewa wakfu pia. Sasa atabakia kuwa muumini wa kawaida

Aliyekuwa askofu Konde aondolewa wakfu. Fimbo, msalaba na pete yake vyaondolewa wakfu pia. Sasa atabakia kuwa muumini wa kawaida

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Kanisa la KKKT Dayosisi ya Konde leo imetangaza kumwondolea wakfu wa Uaskofu aliyekuwa askofu wa Dayosisi hiyo, Dk. Edward Mwaikali.

Pia imeviondolea wakfu vifaa vya Kiaskofu alivyokuwa anatumia kama pete, msalaba pamoja na fimbo ambavyo alikabidhiwa tarehe 18 Januari 2018 alipowekwa wakfu kuiongoza Dayosisi ya Konde.

Uamuzi huo umefanyika leo Jumapili Juni 5, 2022 wakati wa lbada ya kumweka wakfu mrithi wake, Dk. Geofrey Mwakihaba.

Wamefikia hatua hiyo baada ya Dk. Mwaikali kugoma kuvirejesha ili vitumike kwa mrithi wake kwa mujibu wa taratibu za kanisa hilo.

Dk. Mwaikali aliondolewa madarakani tarehe 22 Machi 2022 na Mkutano Mkuu Maalum wa KKKT Dayosisi hiyo kwa kile kilichoelezwa kushindwa kuiongoza vyema.

Vitu vingine ambavyo amegoma kuvirejesha ni kiti cha uaskofu na mavazi ambavyo navyo vimeondolewa wakfu.

20220605_132917.jpg
 
Mimi sio muumini wa dini kwa sababu mungu hayupo ila dini kama taasisi za kihiyari zina taratibu zake na lazima kama unataka kua muumini ama kiongozi ufuate hizo taratibu.

Huyo askofu alienda kinyume na taratibu za kanisa na kujiona ni mkubwa kuliko kanisa sasa kanisa limemmaliza kabisa.

Ni vyema watu kuheshimu taratibu za taasisi walizokubali kwa hiyari yao kua wanachama ama viongozi.

Nakumbuka miaka ile ya kuibuka kwa makanisa ya kilokole, kiongozi mmoja wa kanisa la kilokole, Kulola aliasi TAG na akaamua kukatalia majengo na makanisa ya TAG. Tukawa tunajiuliza kama umeamua kua mwenyewe kivyako si uachie vitu vya watu, ikawa shida kubwa.

The same ikaja kwa Free Pentecoste church na Pentecoste church of Tanzania, Mlima wa Moto(Juzi nimesikia mchungaji wa mlima wa moto amefichwa tabata na changudoa toka mwezi wa 2, hii ni balaatupu mchungaji kutekeleza kondoo aliopewa awaongoze amejificha kwa malaya anakula utamu tu) na TAG, Father Nkwere na Kanisa Katoliki nk.
 
#HABARI Kanisa la KKKT Dayosisi ya Konde leo imetangaza kumwondolea wakfu wa Uaskofu aliyekuwa askofu wa Dayosisi hiyo, Dk. Edward Mwaikali. Pia imeviondolea wakfu vifaa vya Kiaskofu alivyokuwa anatumia kama pete, msalaba pamoja na fimbo.

#NipasheMwangaWaJamii #NipasheHabari https://t.co/MZMozGtEbjView attachment 2251168
Tumemaliza kazi sisi KKKT

KWA UTARATIBUU Kabisa wa Kanisa letu.

Nakushauri Ndugu Mwaikali omba msamahaa la sivyo mwisho wako sio mzuri
 
#HABARI Kanisa la KKKT Dayosisi ya Konde leo imetangaza kumwondolea wakfu wa Uaskofu aliyekuwa askofu wa Dayosisi hiyo, Dk. Edward Mwaikali. Pia imeviondolea wakfu vifaa vya Kiaskofu alivyokuwa anatumia kama pete, msalaba pamoja na fimbo.

#NipasheMwangaWaJamii #NipasheHabari https://t.co/MZMozGtEbjView attachment 2251168
KKK (T) inachekesha sana hapa duniani.

Maswali wasiyoweza kujibu:

1. Wakfu huwa ni wa binadamu au MUNGU?

2. Kwanini Kanisa lina madeni yasiyolipika kama ya HIPC?

3. Kwanini Maaskofu hawawezi kuhamishwa Dayosisi? (Wako autonomous)

4. Kwanini Watumishi wanakosaga mishahara wakati fulani na mara nyingi?

5. Kwanini Maaskofu wengine wana muda maalum wa kutumika na wengine wanakaa hadi kustaafu kwa Kanisa hilo hilo moja?

6. Kama Kanisa limewekeza kwenye elimu kuanzia shule za awali hadi vyuo vikuu kwanini watoto wa watumishi wanafukuzwa shule kwa kukosa ada? Utumishi wa wazazi wao hautoshi kuwa dhamana ya kusoma bila ada? (kwanini wasipewe scholarship?)

7. Kama Kanisa limewekeza kwenye afya kuanzia afya ya msingi hadi ya umma (Primary to Public Health) kwa maana ya zahanati, vituo vya afya, hospitali, hospitali teule, hospitali za rufaa, hospitali za umahiri (consultant hospitals) kwanini watumishi na familia zao wafe kwa kukosa ela za medical evacuation kwenda ughaibuni? Kwanini wanakuwa ombaomba kwa ndugu, jamaa, marafiki, majirani, waumini ndiyo wawachangie?

8. Kwanini watumishi wanaoondolewa wakfu wakienda wakaanzisha Makanisa yao au Huduma zao wanafanikiwa sana? Wakfu huwa ni wa binadamu au MUNGU? Angalia Mwingira alikuwa Mwinjilisti wa KKKT, angalia Fernandes alikuwa Mchungaji wa Pentecost, angalia Moses Kulola alitimuliwa TAG akaanzisha EAGT, Gamanywa aliondoka Pentecost nk nk.

9. Kwanini asilimia 90 ya watumishi kwenye Makanisa haya ya Kimagharibi wanafanikiwa kiuchumi nje ya mfumo wanaouhubiri? Wakianzisha na kusimama kwenye Makanisa yao au Huduma zao ndipo wanapopata mafanikio makubwa na kuwa Mamilionea. Mwingira aliitangulia KKKT kuanzisha benki, Tv, Kilimo na Ufugaji Katavi, Sacoss, mgodi Arusha nk. Fernandes pia aliitangulia Pentecost kuanzisha Tv, Gamanywa naye aliitangulia Pentecost kuanzisha media..

10. Kwanini watumishi wanaotumika kwenye vituo vya Dayosisi (siyo Dayosisi kwenyewe) baadhi yao wana ugomvi wa sadaka na waumini?

11. Kwanini KKKT, Moravian (version zote mbili) na Anglikana Mchungaji au Askofu anaweza kupigwa na waumini au kufukuzwa?

Hapo juu namba 4, 6, 7, 9 na 10 wahanga wake ni watumishi walio chini kwenye vituo vya Dayosisi, siyo walio makao makuu ya Dayosisi.
 
Mimi sio muumini wa dini kwa sababu mungu hayupo ila dini kama taasisi za kihiyari zina taratibu zake na lazima kama unataka kua muumini ama kiongozi ufuate hizo taratibu.

Huyo askofu alienda kinyume na taratibu za kanisa na kujiona ni mkubwa kuliko kanisa sasa kanisa limemmaliza kabisa.

Ni vyema watu kuheshimu taratibu za taasisi walizokubali kwa hiyari yao kua wanachama ama viongozi.

Nakumbuka miaka ile ya kuibuka kwa makanisa ya kilokole, kiongozi mmoja wa kanisa la kilokole, Kulola aliasi TAG na akaamua kukatalia majengo na makanisa ya TAG. Tukawa tunajiuliza kama umeamua kua mwenyewe kivyako si uachie vitu vya watu, ikawa shida kubwa.

The same ikaja kwa Free Pentecoste church na Pentecoste church of Tanzania.
Mungu hayupo halafu kila saa unafuatilia taasisi zake 🤣
 
natanguliza samahani, naomba mnipe jina la askofu KKKT wa kinyakyusa AMBAYE HAJA-CREATE MIGORORO PALE ALIPO, AU ALIPOKUWA
 
Mungu hayupo halafu kila saa unafuatilia taasisi zake 🤣
Wewe mburula, hizo ni taarifa zinapatikana kwenye public domains. Wengine sisi ni wanasheria tumehusika kwenye cases nyingi ya taasisi mbalimbali zikiwemo za dini hivyo tunajua.

Una akili ndogo sio rahisi kuelewa mambo mengi kwa wakati mmoja.
 
Back
Top Bottom