Huyu jamaa kama angekuwa serious zaidi na kazi yake angepiga hela sana,kwani kufanya kazi na Diamond kumempa umaarufu mkubwa sana na naona anashindwa kuutumia , siku hizi ameamua kuchamba kwa kutumia insta hii si tabia ya kiume.Ujue sisi wanaume huwaga hatuna vinyongo hata tukiwa na beef zetu lakini zinachukuaga muda mfupi na huisha,sasa kwa kulijua hilo kama alikuwa na neno lake basi angewafikishia watu wengine wa karibu na Diamond huo ndio ushikaji ,mimi mwenyewe hata nigombane vipi na marafiki zangu ,hata kama akikosea siwezi kumkosoa mbele ya kadamnasi ,hata kama kaniblock nitatafuta watu wa karibu nitaongea nao wamfikishie ujumbe basi.Sasa yeye analeta habari za wadada wa Bongo Movies.Hebu kifesi fanya kazi yako ,haya maswala ya Diamond na familia yake achana nayo .