Aliyekwepa foleni kuaga mwili wa Malkia Elizabeth II kufikishwa mahakamani kesho

Aliyekwepa foleni kuaga mwili wa Malkia Elizabeth II kufikishwa mahakamani kesho

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Mwanaume mmoja ameshtakiwa kwa kukwepa kupanga mstari wakati waombolezaji wakipita kwenye jeneza kuaga mwili wa Malkia Elizabeth II.

Mwanaume huyo ambaye anatoka Tower Hamlets mashariki mwa London, Muhammad Khan anadaiwa kupita nje ya foleni Ijumaa Septemba 16, 2022 na alikamatwa siku hiyo hiyo.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vy kimataifa, urushaji wa matangazo ya moja kwa moja ya maombolezo kutoka katika Ukumbi wa Westminster yalikatwa wakati tukio lilipotokea.

Taarifa kutoka kwa Polisi imesema kuwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 28 alishitakiwa jana Jumamosi na atafikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Westminster kesho Jumatatu.

Kijana huyo amekuwa mtu wa pili kushtakiwa kwa kutenda kosa akiwa kwenye foleni ya kuuaga mwili wa Malkia II.

Mwanaume mwingine mwenye umri wa miaka 19 alishtakiwa baada ya kudaiwa kuvua nguo na kujaribu kuwanyanyasa kingono waombolezaji wa kike walipokuwa wakisubiri kwenye foleni katika bustani ya Victoria Tower Jumatano.

Kijana huyo Adio Adeshine alishtakiwa kwa makosa mawili ya unyanyasaji wa kijinsia na makosa mawili ya kukiuka amri ya kuzuia madhara ya kingono.

Mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabeth II yatafanyika kesho Jumatatu Westminster Abbey, London, kabla ya mwili wake kulazwa kwenye kasri la Windsor.

Kiongozi huyo wa kimila alifariki Alhamisi, Septemba 8, 2022 akiwa na miaka 96 huku akishikilia rekodi ya kuliongoza Taifa hilo kwa muda wa miongo saba.

Elizabeth alianza kuliongoza taifa hilo akiwa na miaka 25 tu mwaka 1952.

Mwananchi
 
Sasa sijui natizama mpira ndiyo nimeshindwa kuielewa hii taarifa?!

Nitarudi baadaye.
 
He must punished accordingly... Wenzako wamepanga folen we una skip ili uwe mbele uache waliokutangulia!.
... huko ni kukosa ustaarabu kwa hali ya juu. Ni mhindi au mpakistan kwa mujibu wa jina lake wana vitabia vya aina hiyo.
 
Uyo shetan hawajamzika tu aisee
Unakalia
IMG_20220831_134836.jpg
 
... huko ni kukosa ustaarabu kwa hali ya juu. Ni mhindi au mpakistan kwa mujibu wa jina lake wana vitabia vya aina hiyo.
Teh teh teh..kapeleka Usela wa Mumbai ama Tripoli kwenye Nchi za watu wanaohusudu ustaarabu.
Huko mtu anakuta mtu yupo kwenye ATM MACHINE na wewe umesimama jirani tu na hiyo ATM ni lazima akusalimie then akuulize:,ni foleni?.
Hawezi fika tu na kujipachika.
Kuna watu katika hiyo folen wamekaa masaa 19 bila kulifikia Jeneza la Elizabeth ila yeye na ujuaji wake anataka atumie dakika 20 kulifikia Jeneza.
 
Mwanaume mmoja ameshtakiwa kwa kukwepa kupanga mstari wakati waombolezaji wakipita kwenye jeneza kuaga mwili wa Malkia Elizabeth II.

Mwanaume huyo ambaye anatoka Tower Hamlets mashariki mwa London, Muhammad Khan anadaiwa kupita nje ya foleni Ijumaa Septemba 16, 2022 na alikamatwa siku hiyo hiyo.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vy kimataifa, urushaji wa matangazo ya moja kwa moja ya maombolezo kutoka katika Ukumbi wa Westminster yalikatwa wakati tukio lilipotokea.

Taarifa kutoka kwa Polisi imesema kuwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 28 alishitakiwa jana Jumamosi na atafikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Westminster kesho Jumatatu.

Kijana huyo amekuwa mtu wa pili kushtakiwa kwa kutenda kosa akiwa kwenye foleni ya kuuaga mwili wa Malkia II.

Mwanaume mwingine mwenye umri wa miaka 19 alishtakiwa baada ya kudaiwa kuvua nguo na kujaribu kuwanyanyasa kingono waombolezaji wa kike walipokuwa wakisubiri kwenye foleni katika bustani ya Victoria Tower Jumatano.

Kijana huyo Adio Adeshine alishtakiwa kwa makosa mawili ya unyanyasaji wa kijinsia na makosa mawili ya kukiuka amri ya kuzuia madhara ya kingono.

Mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabeth II yatafanyika kesho Jumatatu Westminster Abbey, London, kabla ya mwili wake kulazwa kwenye kasri la Windsor.

Kiongozi huyo wa kimila alifariki Alhamisi, Septemba 8, 2022 akiwa na miaka 96 huku akishikilia rekodi ya kuliongoza Taifa hilo kwa muda wa miongo saba.

Elizabeth alianza kuliongoza taifa hilo akiwa na miaka 25 tu mwaka 1952.

Mwananchi
Jina limemponza
 
Mkuu,
Ndio hapo Sasa unanzakujiuliza hawa na demokrasia wanayoihubiri kila siku hasa kwetu Africa mbona wao hawendani nayo kimatendo,,[emoji16]
Demokrasia maana yake nini? Ni kwenda msibani u nakuta wenzako wame panga foleni halafu wewe unaji ona bora kuliko wao na kuamua kuwa pita nje ya mstari na upongezwe? Haiwezekan haujalewa

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom