Aliyemrudisha Kim Poulsen kuwa kocha wa Taifa Stars amelenga nini?

Aliyemrudisha Kim Poulsen kuwa kocha wa Taifa Stars amelenga nini?

Huyu kocha amenishangaza sana, anafanya mabadiliko ya wachezaji 3 ktk dakika ya 90 kana kwamba timu yake inaongoza wakati imeshafungwa. Yaani anachelewesha muda nakujihukumu mwenyewe. TFF timua huyo kocha.

Vv
Huyu siyo kocha , labda ana kazi nyingine
 
Dah

Tumuombe msamaha Ettiene, tulimkosea sana.

Mara nyingi iwe klabu ama taifa, kocha anaporudi mara ya pili huishia kufanya vibaya. Huyu Kim muda wake ulishapita
 
Naona hapa tumwepigwa tena. Like tunashindwa vipi kujifunza kwa wenzetu ambao sasa wameona bora kuwapa wazawa chance kuliko una hire mgeni alafu bado tunapigwa tuu.
 
Hoja siyo uzawa ila aina ya kocha, Julio alipewa timu ya vijana unakumbuka matokeo yalikuwa vipi?

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
Hoja bado ni pale pale wazawa...tunatakiwa hao wazawa tuwaendeleze na tukawasomeshe. Wapo makocha nchi hii wanaweza endelezwa.

Sasa tunaishia wapa experience makocha wakigeni wakati hatupati chochote.
 
Hoja bado ni pale pale wazawa...tunatakiwa hao wazawa tuwaendeleze na tukawasomeshe. Wapo makocha nchi hii wanaweza endelezwa.

Sasa tunaishia wapa experience makocha wakigeni wakati hatupati chochote.
Wazawa wanatakiwa wajiendeleze wenyewe, wakishasoma wasiwaze kufundisha Simba au yanga, watoke nje ya nchi kutafuta timu za kufundisha tukiona uwezo wao ndio tufikirie kuwapa timu ya Taifa.
Timu ya taifa sio ya majaribio ya kuwapa kazi kwa kigezo cha uzawa bali uwezo ndio kigezo kikuu
 
Wazawa wanatakiwa wajiendeleze wenyewe, wakishasoma wasiwaze kufundisha Simba au yanga, watoke nje ya nchi kutafuta timu za kufundisha tukiona uwezo wao ndio tufikirie kuwapa timu ya Taifa.
Timu ya taifa sio ya majaribio ya kuwapa kazi kwa kigezo cha uzawa bali uwezo ndio kigezo kikuu
Kwanza kujiendeleza wenyewe bila support ya government ni ngumu. Kumbuka licences za uefa can cost up to 30million. Tuwe wakweli makocha wangapi wazawa wanaweza kulipa that amout ukizingatia wakati wao wanacheza pay ilikuwa magumashi?

Kuhusu kufundisha simba na yanga hapo wala hamna tatizo. Ni nadra sana mtu kwenda kufundisha nje ya nchi kama hajaweza fundisha top team kwenye nchi yake. Mfano hai tunao hapa tanzania. Kayuni pekee alienda fundisha kenya akitokea yanga. Leo hii tunamuona mosimane al ahly kwa sababu alifundisha mamelodi ambayo kupitia champions league ndio akaonekana. Chukulia italia pia..ancelotti, conte, capello wote walifundisha timu kubwa nchini kwao ndio wakatoka nje. Hiyo ndio trend kwenye mpira.

Ofcoz timu ya taifa sio ya majaribio. Kwa kupitia mikakati mizuri unakuwa umeshamuandaa kocha wakuja kurithi national team. Huyo kocha wa wapinzani wetu jana amefundisha u20 women national team na ndio kapewa timu ya wakubwa. Ni mchakato mrefu na mipango ya muda mrefu sio kwamba unakurupuka tuu.
 
Naona hapa tumwepigwa tena. Like tunashindwa vipi kujifunza kwa wenzetu ambao sasa wameona bora kuwapa wazawa chance kuliko una hire mgeni alafu bado tunapigwa tuu.
Mzawa yupi anaweza kufundisha timu yetu ya taifa ?

Julio amekuwa kocha wa under 20 na under 23 kwa muda mrefu sana lakini kila mechi anapokea vipigo tu
 
Tanzania tumechoka kuwa kichwa cha mwenda wazimu.
Kila anaejifunza kunyoa basi anajifunzia kwenye kichwa cha mwendawazimu.
 
Back
Top Bottom