Aliyemrudisha Kim Poulsen kuwa kocha wa Taifa Stars amelenga nini?

Wabongo huwa mnataka shortcut sana yan unataka upande mche asubuhi afu jion uvune kitu ambacho ni kigumu ndo maana wengi mnaishia kuwa wezi na mafisadi.
Sasa untaka kupima mafanikio ya kocha kwa mechi mbili kweli?
 
Simba haiwezi kuinvest kwa mtu ambaye akishakuwa na vyeti vizuri muda wowote anawaacha, unaweza kukuta simba wanamsomesha akirudi anateuliwa kocha wa taifa au anapata timu inayomlipa vizuri zaidi ya Simba.
Hayo mambo ya kusomesha ilikuwa enzi za ujamaa sanasana tff watafute scholarship kwenye balozi mbalimbali.
Tatizo jingine makocha wengi walikimbia shule
 
Kiukweli bado sijaelewa kabisa kisa cha Kim Poulsen kupewa kazi ya kufundisha Timu ya Taifa, Aliyempa kazi hiyo ni nani na alilenga nini?
Hawa makocha tutakuwa tunawafukuza kila siku, tatizo lipo kwenye mentality ya wachezaji wetu, wapo too soft, hawafundishiki, wameridhika na usimba na uyanga, huwezi linganisha na wachezaji wa west africa na north. Alafu pia wanaomzunguka kocha mkuu, wanamhujum, kocha mgen kwa vyovyote atakuwa anasikiliza ushauri wa wenyeji kumpa characteristics za wachezaji.
 
Wewe mbona unakuwa na mtazamo hasi...kwani matola atashindwa kulipa fadhila...come on he is not that stupid. Wee msomeshe na mlipe vile anavyostahili kulipwa kama head coach just like wat owner wa mamelodi alivyofanya kwa mosimane. Hakika na kwambia atajituma na atafanya kazi.

Hilo la shule kwa coaches wetu kweli lipo lakini am sure kuwa ways in which tunaweza kupata educated coaches. Ata sasa wapo ambao wana education ni kuhakikisha tunawaendeleza hao na ku motivate wengine waingie kwenye hii profession.
 
Inawezekana na mtazamo hasi lakini wewe upeo wako ni mdogo mimi naongea reality wewe unalazimisha vitu ambavyo havipo kibadeni na Boniface na marehemu Joe Bendera walisoma ujerumani wakati huo bado mfumo wetu ni wa kijamaa, wanaotakiwa kuwa na program ya kusomesha makocha ni ttf lakini wao wamekuwa wakitoa kozi fupifupi sasa hivi tuko Ulimwengu wa kibepari kama Matola kaamua awe kocha ndio career ya maisha yake aende kusoma akisubiri Simba wamsomeshe ataendelea kuwa kocha msaidizi na ataweza kukabidhiwa timu
 
Tff wanajitahidi kutoa kozi zakuwaendeleza makocha hilo lazima tukubali. Hizo kozi wether ndani ya nchi au nje ya nchi lazima zilipiwe. Ndio kama kocha ambaye ndio profession yako unatakiwa mstari wa mbele kujiendeleza ila kuna sehemu club au government lazima wakushike mkono.
 
Taifa Stars imegeuzwa Mikia FC wachezaji wa benchi wa Simba wanaanza. Ajabu na kweli. Nyoni, Kenedy, Yassin. Matola huyo mamaaake na kocha bwege tu.
 
Kuna makocha wenye vipaji vikubwa na elimu, mfano Mwambusi na Mkwasa, wana lesen A, hawa taifa lingewaendeleza waongeze skills waendane na wakati, alafu tuwape timu ya Taifa.
 
Kiukweli bado sijaelewa kabisa kisa cha Kim Poulsen kupewa kazi ya kufundisha Timu ya Taifa, Aliyempa kazi hiyo ni nani na alilenga nini?
Kumlaum Kim Poulsen ni kumuonea tu, ukiangalia kikosi chetu wachezaji wa kulipwa tunaowategemea, wapo out of form, Samatta umri ushamtupa, Msuva kwenye derby ya Morocco aliingia na kutolewa, hamna alichokuwa anafanya, sasa ona Guinea, almost timu nzima wapo unyamwezin na wanaanza kwenye timu zao.[emoji42]
 
Huyo Msuva ndiyo alitoa pasi kwa adui bayo move ilienda hadi goli
 
Kuna makocha wenye vipaji vikubwa na elimu, mfano Mwambusi na Mkwasa, wana lesen A, hawa taifa lingewaendeleza waongeze skills waendane na wakati, alafu tuwape timu ya Taifa.
Mkwasa alishasababisha tukapigwa 7 kwa buyu na Algeria
 
Mkwasa alishasababisha tukapigwa 7 kwa buyu na Algeria
Kupigwa 7 haizuii ukweli kwamba ni miongoni mwa makocha bora, hata Wenger aliwah pigwa 8 na Man Utd, miongoni mwa makocha wasomi wachache tulionao, Mwambusi, Mkwasa, Koroso, huyu koroso alikuwa anafundisha timu ya vijana Botswana na ni mshauri mkubwa wa project za soccer kule.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…