Aliyepotea Singida abainika kuuawa kwa mganga wa kienyeji

Aliyepotea Singida abainika kuuawa kwa mganga wa kienyeji

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Haya mambo yanahitaji uchunguzi, na subira, huyu naye chadema walisema katekwa na polisi


=====

Jeshi la polisi mkoani Singida linawashikilia watu watatu akiwemo mganga wa kienyeji ambaye hajaweza kufahamika jina lake baada ya kutuhumiwa kumuua kijana samwaja na kumnyofoa baadhi ya viungo na kuufukia mwili wa kijana huyo katika makazi yake.

Tukio hilo limetokea katika kijiji cha makuro kata ya makuro tarafa ya mtinko halmashauri ya singida vijijin mkoan singida baada ya ndugu wa kijana samwaja na wananchi wa kata hiyo kumtafuta kijana huyo aliyepotea toka tarehe 8. 8.2024 wakati akitizama mechi ya ngao ya hisani kati ya Yanga na Simba.

Baadhi ya wananchi walianza kumtilia shaka mganga huyo wa kienyeji aliyehamia katika kijiji hicho hivi karibuni huku akiwa na matukio ya kuchinja mbuzi na ng’ombe za watu katika kijiji hicho licha ya wananchi hao kuripoti matukio hayo kwa viongozi.

Mkuu wa wilaya ya singida godwin gondwe amekiri kutokea kwa tukio hilo huku akielezea hatua ambazo zimechukuliwa na serikali.

Wananchi wa kata hiyo wanaeleza kuwa kuna watu 3 ambao wamepotea katika mazingira ya kutatanishabkatika kata hiyo ambao bado hawajapatikana.
 
Jamii yetu imebobea kwenye ushirikina. Haya makafara mengi yanaashiria tatizo letu kubwa la kuwa mbele mbele kwenye dini wakati ni walozi hatufai
 
Huyo Sangoma apigwe vikali yeye, tunguri hadi mizimu yake.
Mxxxxxiiiiiieeeeew, [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Yaani ni home kabisaa tukio ni kwa jirani😢😢😢😢
Duh kwahiyo huyo mganga ni jirani yako mkuu? Ni kweli alikuwa na hayo matukio ya kuchinja mifugo ya watu bila ruhusa? Na kwanini hawakumchukulia hatua kama hilo lilikuwa linatokea kitambo?
Upo hapo nyumbani na umethibitisha kwa macho yako baada ya mwili kufukuliwa au ni maneno tu ya kiufikishaji habari?
 
Inawezekana akawa sangoma fake hana mizimu wala vinyamfyereee[emoji28]
Hata awe sangoma uchwaraaa, apigwee had maruhani koko yake yabwatukeee.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ddduuuhhh bora sie wala urojo mdebwedo tukishashiba urojo wetu hatuna shida na mtu. Maisha gani hayo kila siku taarifa za watu kuuwana, tena kikatili...ndio kutafuta pesa kwa nguvu zote!!!?
 
Duh kwahiyo huyo mganga ni jirani yako mkuu? Ni kweli alikuwa na hayo matukio ya kuchinja mifugo ya watu bila ruhusa? Na kwanini hawakumchukulia hatua kama hilo lilikuwa linatokea kitambo?
Upo hapo nyumbani na umethibitisha kwa macho yako baada ya mwili kufukuliwa au ni maneno tu ya kiufikishaji habari?
Mimi nipo mkoa mwingine kimakazi ila mahali tukio limetokea ni jirani na home kwetu kabisaa hata familia ya kijana iliodhurika naifahamu na kijana namfahamu ila hayo mengine sijui
 
Huyo Sangoma apigwe vikali yeye, tunguri hadi mizimu yake.
Mxxxxxiiiiiieeeeew, [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
Ulifuatilia hili sakata??...

Walipatikana wengine watatu hapo kwake na wote walifukiwa wakiwa wamekaa... Wametambulika pia.

Pia alikuwa na makazi sehemu nyingine ambapo ilipatikana miili mingine 7 akiwemo askari polisi mmoja aliyepotea mwanzoni mwa mwaka.

Jumla ni miili 10 iliopatikana hadi sasa.

Nilishuhudia mchakato. Inasikitisha
 
Back
Top Bottom