chiembe
JF-Expert Member
- May 16, 2015
- 16,859
- 28,112
Haya mambo yanahitaji uchunguzi, na subira, huyu naye chadema walisema katekwa na polisi
=====
Jeshi la polisi mkoani Singida linawashikilia watu watatu akiwemo mganga wa kienyeji ambaye hajaweza kufahamika jina lake baada ya kutuhumiwa kumuua kijana samwaja na kumnyofoa baadhi ya viungo na kuufukia mwili wa kijana huyo katika makazi yake.
Tukio hilo limetokea katika kijiji cha makuro kata ya makuro tarafa ya mtinko halmashauri ya singida vijijin mkoan singida baada ya ndugu wa kijana samwaja na wananchi wa kata hiyo kumtafuta kijana huyo aliyepotea toka tarehe 8. 8.2024 wakati akitizama mechi ya ngao ya hisani kati ya Yanga na Simba.
Baadhi ya wananchi walianza kumtilia shaka mganga huyo wa kienyeji aliyehamia katika kijiji hicho hivi karibuni huku akiwa na matukio ya kuchinja mbuzi na ng’ombe za watu katika kijiji hicho licha ya wananchi hao kuripoti matukio hayo kwa viongozi.
Mkuu wa wilaya ya singida godwin gondwe amekiri kutokea kwa tukio hilo huku akielezea hatua ambazo zimechukuliwa na serikali.
Wananchi wa kata hiyo wanaeleza kuwa kuna watu 3 ambao wamepotea katika mazingira ya kutatanishabkatika kata hiyo ambao bado hawajapatikana.
=====
Jeshi la polisi mkoani Singida linawashikilia watu watatu akiwemo mganga wa kienyeji ambaye hajaweza kufahamika jina lake baada ya kutuhumiwa kumuua kijana samwaja na kumnyofoa baadhi ya viungo na kuufukia mwili wa kijana huyo katika makazi yake.
Tukio hilo limetokea katika kijiji cha makuro kata ya makuro tarafa ya mtinko halmashauri ya singida vijijin mkoan singida baada ya ndugu wa kijana samwaja na wananchi wa kata hiyo kumtafuta kijana huyo aliyepotea toka tarehe 8. 8.2024 wakati akitizama mechi ya ngao ya hisani kati ya Yanga na Simba.
Baadhi ya wananchi walianza kumtilia shaka mganga huyo wa kienyeji aliyehamia katika kijiji hicho hivi karibuni huku akiwa na matukio ya kuchinja mbuzi na ng’ombe za watu katika kijiji hicho licha ya wananchi hao kuripoti matukio hayo kwa viongozi.
Mkuu wa wilaya ya singida godwin gondwe amekiri kutokea kwa tukio hilo huku akielezea hatua ambazo zimechukuliwa na serikali.
Wananchi wa kata hiyo wanaeleza kuwa kuna watu 3 ambao wamepotea katika mazingira ya kutatanishabkatika kata hiyo ambao bado hawajapatikana.