Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Lupembe mkoani Njombe ambaye kwa sasa ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Njombe Jolam Hongoli amewataka Watanzania kuacha kufikiria kuwa ili uweze kuwa Mbunge unapaswa kujua kusoma na kuandika tu kwa kuwa kazi hiyo ya uwakilishi ni kubwa na inahitaji maarifa.
Hongoli ameeleza hayo wakati akiongea na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mavanga mara baada ya Jumuiya ya Wazazi kufika shuleni hapo na kupanda miti pamoja na kutoa elimu mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kuelekea maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM huku akiwataka wanafunzi kuongeza bidii kwenye masomo kwa kuwa serikali imeendelea kutekeleza Ilani kwa kujenga miundombinu ya kutosha.
"Chama Cha Mapinduzi kinataka watoto wote mfaulu kwasababu mtaweza kujiajiri au kuajiriwa, na kuna wengine wanasema ubunge ni mradi ujue kusoma na kuandika sio kweli, kazi ya mbunge ni kubwa kwa kuwa ni lazima ujue Kiingereza, sheria kidogo mambo ya elimu na mambo mengine kwa hiyo kutunga sheria ni kazi ngumu", amesema Hongoli.
Licha ya mambo mengi yaliyofanywa na Jumuiya katika kuchagiza kilele cha kuzaliwa kwa CCM lakini pia imefanikiwa kuwashika mkono kwa kuwawezesha vitu mbalimbali ikiwemo sukari na sabuni wazee ambao ni waasisi wa chama hicho wanaoishi kata ya Mavanga
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Lupembe mkoani Njombe ambaye kwa sasa ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Njombe Jolam Hongoli amewataka Watanzania kuacha kufikiria kuwa ili uweze kuwa Mbunge unapaswa kujua kusoma na kuandika tu kwa kuwa kazi hiyo ya uwakilishi ni kubwa na inahitaji maarifa.
Hongoli ameeleza hayo wakati akiongea na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mavanga mara baada ya Jumuiya ya Wazazi kufika shuleni hapo na kupanda miti pamoja na kutoa elimu mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kuelekea maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM huku akiwataka wanafunzi kuongeza bidii kwenye masomo kwa kuwa serikali imeendelea kutekeleza Ilani kwa kujenga miundombinu ya kutosha.
"Chama Cha Mapinduzi kinataka watoto wote mfaulu kwasababu mtaweza kujiajiri au kuajiriwa, na kuna wengine wanasema ubunge ni mradi ujue kusoma na kuandika sio kweli, kazi ya mbunge ni kubwa kwa kuwa ni lazima ujue Kiingereza, sheria kidogo mambo ya elimu na mambo mengine kwa hiyo kutunga sheria ni kazi ngumu", amesema Hongoli.
Licha ya mambo mengi yaliyofanywa na Jumuiya katika kuchagiza kilele cha kuzaliwa kwa CCM lakini pia imefanikiwa kuwashika mkono kwa kuwawezesha vitu mbalimbali ikiwemo sukari na sabuni wazee ambao ni waasisi wa chama hicho wanaoishi kata ya Mavanga