Ally Hapi ajitetea kama mbogo aliyejeruhiwa

Ally Hapi ajitetea kama mbogo aliyejeruhiwa

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594

Baada ya mh Rais Samia kupiga indiketa ya kuutumbua uongozi wa mkoa wa Mara, leo Ally Hapi katumia jukwaa vizuri kujitetea.

Pamoja na ukweli kuwa Ally Hapi angeweza kuyatatua yote aliyomwomba Rais , lakini wachunguzi wa mambo wanafikiri Ally Hapi bado hajawiva kiuongozi.

Wakurugenzi ndani ya mkoa ndani ya wilaya wanaomsaidia DED bado wako ndani ya mamlaka ya kusimamiwa na kuchukuliwa hatua na Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa kushindwa kuwasimamia watendaji na hata wateule wa Rais mkoani kwake ni kushindwa kazi.
 
Mwanaharakati huru Cyprian Nyamagambire Musiba hajapewa nafasi y kuongea?

Si kwao huko?

Hawa ndio walisema wastaafu wanawashwa washwa .

Msimdanganye dogo wamamsubiria vizuri tu atakamatika.
 
Kasema mkoa wa Mara unanuka rushwa anasahau kuwa yeye mwenyewe ndiye Mkuu wa mkoa!
 
Huyu dogo ashukuru alipoamka leo. Ila siku yake ipo pumbavu sana yani anarusha bomu kwa watendaji ambao wapo chini ya mamlaka yake then anawatetea DEDs kipuuzi.

Huwezi kuniambia kwamba wakuu wa idara ndio wanakwamisha miradi ingali yeye ndio boss wao wa mkoa, where was he to act upon and against their negligence?

Pia huwezi kusema mkurugenzi wa Halmashauri anadanganywa ina maana hafai kuwa kiongozi huyo wa kufukuza na anasema kabisa eti analia, how??? And why Alie wakati yeye ana power ya kuwaripoti pccb Kama wamekula rushwa?

Hivi mtu akikudanganya unalia au unampeleka PCCB akajibu mashtaka?

Hao wameiba wote Ila kaamua kuangusha jumba bovu kwa wakuu wa idara akijua wakurugenzi ni team Samia akiwasemea nae survival yake ni ndogo so ameona heri awaangushie jumba bovu watu ambao hawapo kwenye mamlaka ya Rais. Yeye ndio aondoke mjinga sana huyu .

Hata Rais sijui amekubali vipi Yale maelezo ya RC Kirahisi namna Ile wakati taarifa anayo na alikuwa na maamuzi tayari!!!! Sijui kapigwa juju??

Angeanza na huyu na hao wakurugenzi then awape maagizo hao watakaoteuliwa wakaangalie Kama kweli wao pia ni wa kufukuzwa . Hiyo ingekuwa maamuzi sahihi.

Anyway ndio tunavyoenda.
 
Mwanaharakati huru Cyprian Nyamagambire Musiba hajapewa nafasi y kuongea?

Si kwao huko?

Hawa ndio walisema wastaafu wanawashwa washwa .

Msimdanganye dogo wamamsubiria vizuri tu atakamatika.
Hakuna anasikiliza kichaa kama yule this regime alisikilizwa na kichaa mwenzie, kwani umemuona makonda pale au polepole?
 
Huyu dogo ashukuru alipoamka leo. Ila siku yake ipo pumbavu sana yani anarusha bomu kwa watendaji ambao wapo chini ya mamlaka yake then anawatetea DEDs kipuuzi...
Ndiyo faida ya kuteua vijana wa CCM kwenye kazi za utendaji kama DED, MD, TD, RAS, DAS. Pia kazi za kisiasa kama za DC na RC. Hawajui hata majukumu na mipaka yao ya madaraka
 
Happi amejichanganya zaidi kwa huo utetezi wake dhaifu ameonesha alivyo dhaifu asieweza kuihudumia nafasi yake ya mkuu wa mkoa wa Mara, anatakiwa kuwapisha wengine.
 
Nchi inaliwa mno. Siyo mkoa wa Mara pekee, bali nchi nzima inaliwa kipuuzi sana na wajanja. Kuanzia kwenye majiji, miji, na hata vijijini huko, upigaji umeshika kasi. Pesa zinaingia na kupigwa kimya kimya huku shughuli za maendeleo zikiachwa bila kufanyika.

Kwakweli mama anatakiwa ajipange sana kupambana na hawa wezi na wapigaji. Mifumo ya nchi inampa Rais wigo mpana wa kufanya chochote atakacho. Asipoyatumia mamlaka hayo, lawama zote ni kwake.

Mama asipoangalia atajikuta anaondolewa madarakani hata kwa maandamano. Sisi wanyonge ndiyo tunapita barabara za mashimo, tunakosa huduma za maji, tunanunua mahitaji bei ghali, na kuumizwa kwa njia nyingine nyingi kila siku.
 
Back
Top Bottom