Ally Mayai Salvatory Edward Sekilojo Chambua Salam zenu kutoka Denmark

Maghayo

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2014
Posts
20,307
Reaction score
47,210
Ebwana wanaJF Mzuka!

Leo hapa Copenhagen mchana nilikuwa najinyoosha kidogo nikakutana na waafrika wenzangu wanne. Nikamuomba mmoja anipige picha kwenye simu yangu. Baada ya kunipiga tukaanza story nikawauliza wametoka wapi? Wakaniambia Ghana. Nao wakaniuliza mimi wa wapi? Nikawaambia Tanzania.

Dah kutamka tu Tanzania kuna mmoja mkimya alikaa pemben kusikia tu mimi mtanzania alinisogelea faster. Akaniambia miaka ya nyuma alikuwa mchezaji mpira na alikutana na Yanga akiichezea Costa do Sol ya msumbiji.

Alisema baada ya mechi alijenga urafiki na wachezaji wa Yanga hadi wakamkaribisha Dar. Walisafiri kwa basi kutoka msumbiji Malawi mbeya hadi Dar.

Anawakumbuka Ali Mayai, Salvatory Edward, Sekilojo Chambua, Bakari Malima, Lunyamila wazir mahadh anasema 'the young boy little bit fat'. Ila anamsifia sana Ali Mayai kwa ukarimu wa kipeke. Anakumbuka Ali Mayai alimuambia mayai ni 'egg'. Anakumbuka hadi mitaa ya Dar kwa majina.

Ila cha kuhuzunisha jamaa alinyimwa hifadh ya ukimbiz Ujeruman. Akaja Denmark na yupo Denmark wiki mbili tu tayar wamereject application yake. Wamempa wiki moja kuappeal. Lakin possibility ya kurudishwa Ujeruman ziko juu sana. Je want Yanga wa miaka iyo mnakumbuka rafiki yenu kutoka Ghana aliyekuwa anaichezea Costa do Sol Msumbiji CHARLES ASANTE? Salaam zenu. Nikamuambia Sekilojo yupo Facebook nawengine Akaniambia hatumii mitandao ya Jamii.

Ila ingekuwa eti wachezaji wa simba ndio walijenga naye urafiki ningemkatisha maongez nakusepa (natania)

God bless YANGA.
 
inapendeza sana
 
Nampenda ally mayai kwa jinsi anavyokuwa yuko peace kupokezana na mwenzake wakichambua mambo ya soka! sio mtu unaongea sana as if wengine wako hapo kwa bahati mbaya tu!
Na ally anajua sana aisee nasi mnafiki kuzizungumzia Simba na Yanga japo ni mtoto wetu wa jangwani nadhani usomi umechangia kuwa na weledi wa halI ya juu
 
Hahahah Tunaendekeza ushabiki kila sehemu ya maisha yetu duuh...
 
Hahhaha mkuu kumbe we ni yanga moto chinii bati juu!!unaona sasa africa ilivyo moja ndio maana leo niko nkana hapo kitwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…