Ally Sykes na viboko vya Wabelgiji 1957

Ally Sykes na viboko vya Wabelgiji 1957

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Haya nimeyatoa katika mswada wa kitabu nilichoandika na Ally Sykes ''Under the Shadow of British Colonialism,'' yapata miaka 20 iliyopita.

Ananihadithia safari yake ya kwenda Accra, Ghana mwaka wa 1957 kuhudhuria sherehe za uhuru wa Ghana chini ya Kwame Nkrumah. Safari hii alifanya kwa barabara kutoka Dar es Salaam hadi Accra.

Safari zake zote kuanzia safari ya kwenda Mozambique (1952) kuona kijiji alichotoka babu yake, Sykes Mbuwane, Rhodesia (1953)alikokua anapita njia kwenda kuhudhuria mkutano wa wapigania uhuru Kusini ya Sahara ulioitishwa na Kenneth David Kaunda, Nyasaland alikopita na Denis Phombeah wakiwa wajumbe wa TAA Ally Sykes alikuwa akisafiri na pasi ya Kireno kama Mzulu.

Katika safari yao hii Ally Sykes na Dennis Phombeah wakisafiri kama wajumbe wa TAA walikamatwa Salisbury, Rhodesia na kufukuzwa. Kufukuzwa kwao ndiyo sababu ya yeye kufika Nyasaland kwao Denis Phombeah wakiwa njiani kurejea Tanganyika.

Ally Sykes anasema alipofika Leopoldville, Belgian Congo alipanga kwenye nyumba ya kulala wageni katika ya mji karibu na soko. Anasema ilikuwa hapo ndipo alipoona kwa jicho lake mwenyewe Wabelgiji wakiwapiga viboko Wakongomani.

Jambo hili lilimuuma sana kwani Wabelgiji kwa kitendo kile walikuwa wamewageuza Waafrika kama wanyama ambao wanaweza wakaswagwa na viboko.

Kutokea hapo Leopoldville akavuka mto na kuingia Congo Brazzaville upande wa pili wa mto. AIly Sykes akaingia Lome, Togo na kutoka hapo akaingia to Accra, Ghana. Safari yote kutoka Dar es Salaam hadi Accra ilimchukua siku 18. Ally Sykes anasema nchi zote hizo alizopita hakuona ushenzi kama ule alioshuhudia Leopoldville wa Mwafrika kucharazwa viboko hadharani watu wakishuhudia.

Picha: Dennis Phombeah na Ally Sykes na Julius Nyerere 1958.
 
ALLY SYKES NA VIBOKO VYA WABELGIJI KWA WAKONGOMANI 1957

Haya nimeyatoa katika mswada wa kitabu nilichoandika na Ally Sykes ''Under the Shadow of British Colonialism,'' yapata miaka 20 iliyopita.

Ananihadithia safari yake ya kwenda Accra, Ghana mwaka wa 1957 kuhudhuria sherehe za uhuru wa Ghana chini ya Kwame Nkrumah.

Safari hii alifanya kwa barabara kutoka Dar es Salaam hadi Accra.

Safari zake zote kuanzia safari ya kwenda Mozambique (1952) kuona kijiji alichotoka babu yake, Sykes Mbuwane, Rhodesia (1953)alikokua anapita njia kwenda kuhudhuria mkutano wa wapigania uhuru Kusini ya Sahara ulioitishwa na Kenneth David Kaunda, Nyasaland alikopita na Denis Phombeah wakiwa wajumbe wa TAA.

Katika safari yao hii walikamatwa Salisbury, Rhodesia na kufukuzwa.

Kufukuzwa kwao ndiyo sababu ya yeye kufika Nyasaland kwao Denis Phombeah wakiwa njiani kurejea Tanganyika.

Ally Sykes wakati ule alikuwa anasafiri na pasi ya Kireno kama Mzulu.

Ally Sykes anasema alipofika Leopoldville, Belgian Congo alipanga kwenye nyumba ya kulala wageni katika ya mji karibu na soko.

Anasema ilikuwa hapo ndipo alipoona kwa jicho lake mwenyewe Wabelgiji wakiwapiga viboko Wakongomani.

Jambo hili lilimuuma sana kwani Wabelgiji kwa kitendo kile walikuwa wamewageuza Waafrika kama wanyama ambao wanaweza wakaswagwa na viboko.

Kutokea hapo Leopoldville akavuka mto na kuingia Congo Brazzaville upande wa pili wa mto.

AIly Sykes akaingia Lome, Togo na kutoka hapo akaingia to Accra, Ghana.

Safari yote kutoka Dar es Salaam hadi Accra ilimchukua siku 18.

Ally Sykes anasema nchi zote hizo alizopita hakuona ushenzi kama ule alioshuhudia Leopoldville wa Mwafrika kucharazwa viboko hadharani watu wakishuhudia.

Picha: Dennis Phombeah na Ally Sykes na Julius Nyerere 1958.


Vipi unyama wa kunyongwa hadharani???
 
Mbona picha haipo?
Picha hizo:
Screenshot_20210104-044431.jpg
Screenshot_20210104-044535.jpg
 
ALLY SYKES NA VIBOKO VYA WABELGIJI KWA WAKONGOMANI 1957

Haya nimeyatoa katika mswada wa kitabu nilichoandika na Ally Sykes ''Under the Shadow of British Colonialism,'' yapata miaka 20 iliyopita.

Ananihadithia safari yake ya kwenda Accra, Ghana mwaka wa 1957 kuhudhuria sherehe za uhuru wa Ghana chini ya Kwame Nkrumah.

Safari hii alifanya kwa barabara kutoka Dar es Salaam hadi Accra.

Safari zake zote kuanzia safari ya kwenda Mozambique (1952) kuona kijiji alichotoka babu yake, Sykes Mbuwane, Rhodesia (1953)alikokua anapita njia kwenda kuhudhuria mkutano wa wapigania uhuru Kusini ya Sahara ulioitishwa na Kenneth David Kaunda, Nyasaland alikopita na Denis Phombeah wakiwa wajumbe wa TAA Ally Sykes alikuwa akisafiri na pasi ya Kireno kama Mzulu.

Katika safari yao hii Ally Sykes na Dennis Phombeah wakisafiri kama wajumbe wa TAA walikamatwa Salisbury, Rhodesia na kufukuzwa.

Kufukuzwa kwao ndiyo sababu ya yeye kufika Nyasaland kwao Denis Phombeah wakiwa njiani kurejea Tanganyika.

Ally Sykes anasema alipofika Leopoldville, Belgian Congo alipanga kwenye nyumba ya kulala wageni katika ya mji karibu na soko.

Anasema ilikuwa hapo ndipo alipoona kwa jicho lake mwenyewe Wabelgiji wakiwapiga viboko Wakongomani.

Jambo hili lilimuuma sana kwani Wabelgiji kwa kitendo kile walikuwa wamewageuza Waafrika kama wanyama ambao wanaweza wakaswagwa na viboko.

Kutokea hapo Leopoldville akavuka mto na kuingia Congo Brazzaville upande wa pili wa mto.

AIly Sykes akaingia Lome, Togo na kutoka hapo akaingia to Accra, Ghana.

Safari yote kutoka Dar es Salaam hadi Accra ilimchukua siku 18.

Ally Sykes anasema nchi zote hizo alizopita hakuona ushenzi kama ule alioshuhudia Leopoldville wa Mwafrika kucharazwa viboko hadharani watu wakishuhudia.

Picha: Dennis Phombeah na Ally Sykes na Julius Nyerere 1958.
Siku hizi watoto wadogo wanatandika wazazi wao bakora mbele ya hadhara,mabinti wanatandika bakora waume zao mbele ya hadhara.Ama kweli mkoloni mweusi ni mkoloni mbaya sana.Sasa naelewa ni kwa nini inafika hatua watu wanakuwa na chuki dhidi ya serikali yao kiasi kikubwa.
 
Mohamed Said mzee wangu, hiyo Safari ya kwenda Ghana walitumia barabara, vipi kwenye hiyo misitu ya Congo, mbona nasikia unaweza kukaa miezi miwili mfululizo ni mvua kubwa sana inanyesha na kuna mito mingi na barabara duni? Vipi hali ilikuwaje hiyo miaka ya 50s ?
 
Buji
Mohamed Said mzee wangu, hiyo Safari ya kwenda Ghana walitumia barabara, vipi kwenye hiyo misitu ya Congo, mbona nasikia unaweza kukaa miezi miwili mfululizo ni mvua kubwa sana inanyesha na kuna mito mingi na barabara duni? Vipi hali ilikuwaje hiyo miaka ya 50s ?
Buji...
Zilikuwako barabara za kupita magari na kulikuwa na treni.
 
Nafikiri hiyo Theory ya wabelgiji ndio wame apply DC wa Arusha na Naibu Waziri
 
Haya mambo ya kuwachapa wananchi viboko ni ishara tosha kuwa nchi badala ya kusonga mbele inarudi nyuma kimaendeleo! Karne hii ya leo watu bado wanapewa corporal punishment?
 
Back
Top Bottom