Alpha Dry Cleaner-Mlimani City!

Alpha Dry Cleaner-Mlimani City!

Tusker Bariiiidi

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2007
Posts
5,551
Reaction score
2,153
Nikiwa mteja wa muda mrefu wa Alpha Dry cleaner,nilifurahia sana kitendo cha kwao kutuletea/kutusogezea huduma karibu kwa kufungua duka /Outlet mpya Mlimani City Mall na kama mnavyofahamu karibu huduma zote zinazopatikana hapo karibu asilimia 97 zinafunguliwa siku zote saba za wiki mfano ni benki za NBC,NMB,CRDB,TWIGA na EXIM pia maduka ya kampuni za simu kama ZAIN,TIGO na VODACOM yanatoa huduma zake siku zote iwe sikukuu au wikiendi lakini mimi nimesikitishwa na kitendo chao Alpha Dry Cleaner kufungua duka lao mfano kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 12 jioni kwa siku za wiki na jumamosi saa 3 asubuhi mpaka saa 9 mchana!! na kufungwa siku za Jumapili na siku za sikukuu!!! sasa mimi sijaelewa umuhimu wa wao kuleta duka hilo hapo Mlimani city na kujaza eneo ambalo lingeweza kuongeza ufanisi wa kupatikana huduma nyingine ambazo zinamfanya mteja azifuate katikati ya jiji. Tafadhali uongozi wa Alpha Dry Cleaner uliangalie hilo... NAWASILISHA!!
 
Tusker,
nakuunga mkono. Lakini yaelekea hawa jamaa wa Alpha hawana hata access ya kusoma JF vinginevyo wangelishughulikia hili katika wakati huu wa competition. Nafikiri tufuatilie email yao tuwajulishe kwanza kuwa kuna mtandao maridhawa wa JF, na pili juu ya kuboresha huduma zao haswa katika suala hilo la muda ambao wako wazi.
 
Nimeshapotelewa na SUTI yangu hapo - they just lack seriousness! It seems wale wafanyakazi wa front-desk ni wadogo zake mweye Alpha!
 
alpha dry cleaners na alpha internet za lowasa, inaonekana zinakaribia kufilisika au kukosa seriosness kama ilivyoandkikwa hapo juu, hata ile internet ya mjini ppf tower buree kabisa
 
Alpha Dry Cleaner kufungua duka lao mfano kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 12 jioni kwa siku za wiki na jumamosi saa 3 asubuhi mpaka saa 9 mchana!! na kufungwa siku za Jumapili na siku za sikukuu!!!

Kwa kuwa ni mteja wao ulitakiwa kuwafikishia hili wao wenyewe, ingekuwa bora zaidi. Lakini kwa vyovyote kulileta hapa hata kama hawaingii JF umewasaidia, kwa wale waliokuwa hawajui kuna dry cleaner Mlimani City sasa wanajua.
 
alpha dry cleaners na alpha internet za lowasa, inaonekana zinakaribia kufilisika au kukosa seriosness kama ilivyoandkikwa hapo juu, hata ile internet ya mjini ppf tower buree kabisa
...Mh!! Hata huu ujasilia mali wa kufua nguo nao Ex-PM naye yumo???? I don't believe my legs!!!
 
Yaani sifadi bwana kawekeza kila idara hata zile ambazo sio size yake rancho zote za taifa zake , dili la richmond lake sijui nini chake
 
alpha dry cleaners na alpha internet za lowasa, inaonekana zinakaribia kufilisika au kukosa seriosness kama ilivyoandkikwa hapo juu, hata ile internet ya mjini ppf tower buree kabisa
...Mh!! Hata huu ujasilia mali wa kufua nguo nao Ex-PM naye yumo???? I don't believe my legs!!!
 
...nadhani hiyo biashara alikuwa nayo kabla hata ya U-pm.
 
Kwa kuwa ni mteja wao ulitakiwa kuwafikishia hili wao wenyewe, ingekuwa bora zaidi. Lakini kwa vyovyote kulileta hapa hata kama hawaingii JF umewasaidia, kwa wale waliokuwa hawajui kuna dry cleaner Mlimani City sasa wanajua.

Nimejitahidi sana kuwaambia lakini nadhani wananiambia watawaambia wahusika...Ila inaonyesha hata wao wanafurahia sana kutoka mapema... Mwenye number ya Mama Lowassa pleaseeeee...
 
Tusker Baridiiii!
Ulichokisema kuhusu hiyo dry cleaner ni kweli kabisa,full matatizo halafu watu wanafanya biashara kama hawataki yaani mteja ndo unalazimisha. Pia kwa kukosea nguo za wateja wao hawajambo kabisa.
Mwaka jana nilienda hapo na nguo zangu nyingi tu kufua, wakati wa kuchukua wakanizidishia suti 5 zote hebu fikiria na ustaarabu nilionao nikakanyaga milonjo yangu kuwarudishia jamani mmenizidishia nguo. Upande wangu nilikuwa na nguo nyingi hivyo wakati wa kuchukua sikuziangalia vizuri pale pale japo hamna nguo iliyopotea.
Sehemu waliopo pale ni nzuri kweli kibiashara na hawana mpinzani kwa pale badala ya kuchangamkia wateja wanabaki kuuza sura maana ni vibinti tu vyote vilikuwa,nahisi mpaka sasa. Labda uishie internet au wakufanyie massage kwenye hivyo vyumba vya internet!
 
Tusker Baridiiii!!!! ....inaonekana wewe ni very loyal customer, mpaka unatafuta namba ya mmiliki? kwa nini usiende kwa service provider mwingine kama wanakuzingua?
 
Wanasema wanatoa na huduma za internet but whenever I go there wanasema huduma hakuna. Mh. Waziri mkuu mstaafu ana biashara gani ya siri pale? isijekuwa dry cleaner na internet service ni geresha tu! Au ndo ofisi mpya za DOWANS?
 
Mtu anaviwanda viwili holland mnamwambia mambo ya Alpha.. anawazuga yule..
 
Mimi nilidhani labda kile chumba chenye internet cafe alipewa nyongeza hakilipii aisee, hamna biashara yoyote haki!
 
Mtu ana viwanda viwili holland mnamwambia mambo ya Alpha.. anawazuga yule..

Duuuuu !!!!! Kusikia hivyo miguu yangu yote imelegea!!! Je viwanda hivi aliviangika katika fomu ya maadili ya viongozi????
 
Wajameni,

Sasa mumezidisha... hii peleka kwa mwenye biashara na kama inakukera nenda kwa service provider mwingine.
 
Jamani mnafahamu kuwa kwa waafrika imejengeka dhana, ali muradi una mapesa mengi na unaweza kuiingiza kwenye biashara za kila aina basi wewe ni mjasiriamali! Whether unapata faida, unatoa huduma nzuri ama unakidhi haja ya soko.
Matokeo yake watu wanafungua mashule wakati hawana hata idea ya education service delivery or standards, watu wanaanzisha hospitali vichochoroni hawana idea ya standards watu wanafungua night clubs kwenye sehemu za makazi ya watu . Ukiuliza nini? wana pesa!
Do you wonder service delivery is so low? and our cities are the worst planned in SSA!

Since we are on the topic of businesses opening up, I would like to draw your attention to a new outlet recently opened on Haile Selassie an extension of another one at Mikocheni one of the first malls to be etsablished in Dar. Hilo duka jamani linauza vitu aghali ajabu! sometimes three times higher! sasa najiuliza ni kwa sababu liko masaki au kwa sababu anatake advantage ya euphoria ya watu kusogezewa huduma karibu au ndio ile kawaida yetu ya kuibiwa wabongo? Halafu anadiriki hata kupokea foreign exchange for purchases. Yaani nchi inachezewa hii kama haina wenyewe!!

Hebu TRA tembeleeni huko jamaa walipe kodi basi anagalao ebo!
 
Tusker Baridiiii!
Ulichokisema kuhusu hiyo dry cleaner ni kweli kabisa,full matatizo halafu watu wanafanya biashara kama hawataki yaani mteja ndo unalazimisha. Pia kwa kukosea nguo za wateja wao hawajambo kabisa.
Mwaka jana nilienda hapo na nguo zangu nyingi tu kufua, wakati wa kuchukua wakanizidishia suti 5 zote hebu fikiria na ustaarabu nilionao nikakanyaga milonjo yangu kuwarudishia jamani mmenizidishia nguo. Upande wangu nilikuwa na nguo nyingi hivyo wakati wa kuchukua sikuziangalia vizuri pale pale japo hamna nguo iliyopotea.
Sehemu waliopo pale ni nzuri kweli kibiashara na hawana mpinzani kwa pale badala ya kuchangamkia wateja wanabaki kuuza sura maana ni vibinti tu vyote vilikuwa,nahisi mpaka sasa. Labda uishie internet au wakufanyie massage kwenye hivyo vyumba vya internet!
naenda kesho......
 
Back
Top Bottom