Alphayo Kidata na maajabu ya kuteuliwa, kutenguliwa, kuvuvuliwa na kushtakiwa

Alphayo Kidata na maajabu ya kuteuliwa, kutenguliwa, kuvuvuliwa na kushtakiwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
GF_xQcnX0AAwyWB.jpeg

Huyu ni mojawapo ya Binadamu niliopata kuwafuatilia kidogo, tangu niliposikia jina lake lilitajwa kuwa amepewa dhamana Nchini. Hebu Tazama; 👇🏾👇🏾

DISEMBA 2015
- Aliteuliwa kuwa KAIMU Kamishna Mkuu TRA akitokea nafasi ya Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi aliyoitumikia tangu Agosti 2013.

MACHI 2016
(Takribani Miezi mitatu hivi)
Akathibitishwa rasmi kuwa KAMISHNA MKUU - TRA.

MACHI 23, 2017
(Mwaka Mmoja baadae)
-Akateuliwa kuwa Katibu Mkuu, IKULU.

JANUARI 11, 2018
- Akateuliwa kuwa BALOZI huku akisubiri Uapisho na kupangikiwa kituo cha Kazi.
MEl 20, 2018

-Akaapishwa kuwa BALOZI wa Tanzania Nchini CANADA.

NOVEMBA 8, 2018
- Uteuzi wake Ukatenguliwa, na akaondolewa “HADHI” ya Ubalozi na akarudishwa Nchini.

Siku kadhaa baada ya “kutenguliwa” Ubalozi na kurudishwa Nchini, Novemba 2018 Gazeti Jamhuri liliandika Stori kwamaba anatarajiwa kufikishwa MAHAKAMANI kujibu tuhuma kadhaa (TRA).!

Lakini hakufikishwa Kortini.

SEPTEMBA 2019

- Akateuliwa tena kuwa RAS (Katibu Tawala), Mkoa wa Mtwara.

APRILI 4, 2021
- Mhe. Rais Samia S. Hassan akamteua tena kuwa KAMISHNA Mkuu - TRA.!

JULAI 2, 2024
- Kidata, baada ya kutumikia nafasi hiyo kwa mara ya Pili. Wakati huu akiwa amekaa Ofisini SIKU 1,185 ( Mishara ya takribani Miezi 39 ),sasa anafungasha TRA na kuelekea Ikulu baada ya kuteuliwa kuwa MSHAURI WA RAIS - IKULU.

Andiko la: Stanslaus Lambat
 
Hii nchi ina mifumo ya hovyo sana, yaani watu wale wale tu miaka nenda rudi utafikiri hakuna watz wengine smart kuzidi hao!.
Tazama nafasi za mawaziri, utafikiri wanacheza ile michezo ya watoto wadogo...ukuuti ukuuti, huyu katoka hapa kapelekwa pale...yule katoka kule kasogezwa huku!!.
Nadhani wale vijana wa Kenya Generation Z wasingekubaliana na ungese huu ni hapa Tz tu inawezekana!!.
 
Hii nchi ina mifumo ya hovyo sana, yaani watu wale wale tu miaka nenda rudi utafikiri hakuna watz wengine smart kuzidi hao!.
Tazama nafasi za mawaziri, utafikiri wanacheza ile michezo ya watoto wadogo...ukuuti ukuuti, huyu katoka hapa kapelekwa pale...yule katoka kule kasogezwa huku!!.
Nadhani wale vijana wa Kenya Generation Z wasingekubaliana na ungese huu ni hapa Tz tu inawezekana!!.
Tafuta connection mkuu. Hela kwa wingi, uchawa kwa sana,hewala mzee zizidi na usangoma usikae nao mbali
 
Hii nchi ina mifumo ya hovyo sana, yaani watu wale wale tu miaka nenda rudi utafikiri hakuna watz wengine smart kuzidi hao!.
Tazama nafasi za mawaziri, utafikiri wanacheza ile michezo ya watoto wadogo...ukuuti ukuuti, huyu katoka hapa kapelekwa pale...yule katoka kule kasogezwa huku!!.
Nadhani wale vijana wa Kenya Generation Z wasingekubaliana na ungese huu ni hapa Tz tu inawezekana!!.
Okota okota tu

Ova
 
Nadhani kafikisha 60 yrs huyu afisa kipenyo...angestaafu tu
 
Tafuta connection mkuu. Hela kwa wingi, uchawa kwa sana,hewala mzee zizidi na usangoma usikae nao mbali
Mkuu, binafsi wala sihitaji teuzi yoyote ile...ila kama mwananchi wa kawaida ningependa kuona vipaji vipya vya uongozi vinaibuliwa kwa maendeleo ya nchi yetu.
 
Mkuu, binafsi wala sihitaji teuzi yoyote ile...ila kama mwananchi wa kawaida ningependa kuona vipaji vipya vya uongozi vinaibuliwa kwa maendeleo ya nchi yetu.
Mawazo yako nichanya sana lakini mamlaka zimeamua hivyo na hazitabadilika.
Wazee ndio wanaoatamia mafaili ofisini. Generation Z wakae mbali
 
Hii nchi ina mifumo ya hovyo sana, yaani watu wale wale tu miaka nenda rudi utafikiri hakuna watz wengine smart kuzidi hao!.
Tazama nafasi za mawaziri, utafikiri wanacheza ile michezo ya watoto wadogo...ukuuti ukuuti, huyu katoka hapa kapelekwa pale...yule katoka kule kasogezwa huku!!.
Nadhani wale vijana wa Kenya Generation Z wasingekubaliana na ungese huu ni hapa Tz tu inawezekana!!.
Waambie ukweli Hawa machawa hawaelewi kitu chochote wanaleta! Watu wale wale TU!
 

Huyu ni mojawapo ya Binadamu niliopata kuwafuatilia kidogo, tangu niliposikia jina lake lilitajwa kuwa amepewa dhamana Nchini. Hebu Tazama; [emoji1484][emoji1484]

DISEMBA 2015
- Aliteuliwa kuwa KAIMU Kamishna Mkuu TRA akitokea nafasi ya Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi aliyoitumikia tangu Agosti 2013.

MACHI 2016
(Takribani Miezi mitatu hivi)
Akathibitishwa rasmi kuwa KAMISHNA MKUU - TRA.


(Mwaka Mmoja baadae)
-Akateuliwa kuwa Katibu Mkuu, IKULU.


- Akateuliwa kuwa BALOZI huku akisubiri Uapisho na kupangikiwa kituo cha Kazi.


-Akaapishwa kuwa BALOZI wa Tanzania Nchini CANADA.


- Uteuzi wake Ukatenguliwa, na akaondolewa “HADHI” ya Ubalozi na akarudishwa Nchini.

Siku kadhaa baada ya “kutenguliwa” Ubalozi na kurudishwa Nchini, Novemba 2018 Gazeti Jamhuri liliandika Stori kwamaba anatarajiwa kufikishwa MAHAKAMANI kujibu tuhuma kadhaa (TRA).!

Lakini hakufikishwa Kortini.



- Akateuliwa tena kuwa RAS (Katibu Tawala), Mkoa wa Mtwara.


- Mhe. Rais Samia S. Hassan akamteua tena kuwa KAMISHNA Mkuu - TRA.!

JULAI 2, 2024
- Kidata, baada ya kutumikia nafasi hiyo kwa mara ya Pili. Wakati huu akiwa amekaa Ofisini SIKU 1,185 ( Mishara ya takribani Miezi 39 ),sasa anafungasha TRA na kuelekea Ikulu baada ya kuteuliwa kuwa MSHAURI WA RAIS - IKULU.

Andiko la: Stanslaus Lambat
Kidata na Mataragio ni watu ambao mapengo yao hayazibiki nchi hii

Sent from my TECNO P704a using JamiiForums mobile app
 
Super Intelligence Agent wa bongo huyo gusa unase!
James Bond na Jack Bower hawaoni nje!
😁😁
 
Back
Top Bottom