Ambaye ana uzoefu na biashara za Dar-Zanzibar

Extrovert

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2016
Posts
70,785
Reaction score
186,690
Niko katika mchakato wa kuangalia fursa za kibiashara maeneo tofauti tofauti ila nimefikia muda wa tathmini ya biashara Zenji.

Nina hamu ya kujua biashara ambazo zinashamiri za kutoka Dar kwenda Zanzibar hasa za vyakula. Naomba ushirikiano wenu ili niweze kupata tathmini halisi ya mambo ya changamoto, gharama na kodi ikibidi kwa wazoefu.

Biashara nayolenga mojawapo ni ya kusafirisha mayai ya jumla. Kutoka Dar to Zenji. Karibuni.
 
Kule vitu vya electronics tungekusaidia masuala ya vyakula ni ngumu kidogo
 
Mkuu, mimi sina uzoefu na biashara za zenji ila kama uko serious karibu pm nikwambie nini unaweza kufanya haswa kuanzia mwezi wa sita, utakuja kushuhudia hapa..
 
Nataka nifanye biashara ya mayai mkula! Sema naona kwa Dar soko lipo saturated sana. Mayai ya jumla yale. Nikawaza what if naweza kuyavusha maji incase Zanzibar bado soko sio tight
Usiingie kichwa kichwa, ficha mtaji wako then nenda Zanzibar kazunguke madukani waambie wewe ni mfanyabiashara wa mayai umefulia unataka kufunga biashara unayauza kama anahitaji umuuzie.

Hapo utapata details zote za muuzaji na soko la mayai lilipo

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Eeh uchoyo wa mafanikio ndio asili yetu. Humu raia wanasema mayai zanzibar mengi ila kuna mwana anayavusha toka bara huku. Ndio business yake.
Mkuu Zanzibar nauli Tsh 60,000 kata maji ukajionee mwenyewe.

Hivi karibuni nilikuwa Handeni, nilikuta kuna wazanzibar wengi tu wanakuja kununua mbuzi minadani. Wanabeba kwenye mafuso mpaka Tanga mjini then wanapandisha boti kwenda Zanzibar.
 
Zanzibar mchele wa bara hauna issue.


Kuna mchele kutoka Asia Bei chee
Basmati rice..

Sio kweli sana mkuu. Ule ni kwaajiri ya mapishi ya biriani. Ila unapotaka kupika pilau au wali wa kawaida then mchele mzuri ni huu wetu wa bara especially ile mbegu ya Mchele wa mbeya au shinyanga huwa inadatisha sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…