Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Hakuna kitu hunipa furaha kama niandikapo historia ya mtu kisha akatokea msomaji akaniandikia kuniambia huyo uliyemtaja ni babu au bibi yangu.
Hivi karibuni niliandikiwa na Adam Ahmed kuhusu nyumba aliyolala Mwalimu Nyerere Mikindani safari yake ya kwanza Southern Province mwaka wa 1955 baada ya kutoka UNO.
Aliniandikia na kuniletea picha ya nyumba ile ya ghorofa moja kama ilivyo sasa.
Nyumba hii aliyolala Mwalimu ilikuwa nyumba ya babu yake.
Kiasi cha kama mwezi mmoja niliandika jina la Bi. Amina Kinabo na mjukuu wake Idd Twaha Lema akasoma makala ile.
Bwana Idd kaniandikia na kaniletea picha nyingi za bibi yake Bi. Amina Kinabo wakati wa uhai wake baada ya uhuru akishughulika na harakati za ujenzi wa taifa.
Pamoja na picha kaniletea pia nyaraka za TANU Tawi la Moshi Mjini wakati wa kupigania uhuru.
Angalia barua kutoka maktaba ya Bi. Amina Kinabo kuhusu ziara ya President wa TANJ Julius Nyerere Northern Province mwaka wa 1957.
Siku zote nikisononeka kwa kukosa picha tatu za wanawake shujaa wa Kilimanjaro waliopigania uhuru wa Tanganyika - Bi. Amina Kinabo, Halima Selengia na Mama bint Maalim.
Mzee Yusuf Olotu aliyenifundisha historia ya TANU Moshi mjini anasema TANU Moshi ilijengwa kwa juhudi za akina mama kwa uanachama na kwa fedha zao.
Nilihangaika kupata picha za akina mama hawa bila mafanikio.
Hivi mpaka lini tutaendelea kuipuuza historia ya mashujaa wetu?
Bi. Amina Kinabo
Hivi karibuni niliandikiwa na Adam Ahmed kuhusu nyumba aliyolala Mwalimu Nyerere Mikindani safari yake ya kwanza Southern Province mwaka wa 1955 baada ya kutoka UNO.
Aliniandikia na kuniletea picha ya nyumba ile ya ghorofa moja kama ilivyo sasa.
Nyumba hii aliyolala Mwalimu ilikuwa nyumba ya babu yake.
Kiasi cha kama mwezi mmoja niliandika jina la Bi. Amina Kinabo na mjukuu wake Idd Twaha Lema akasoma makala ile.
Bwana Idd kaniandikia na kaniletea picha nyingi za bibi yake Bi. Amina Kinabo wakati wa uhai wake baada ya uhuru akishughulika na harakati za ujenzi wa taifa.
Pamoja na picha kaniletea pia nyaraka za TANU Tawi la Moshi Mjini wakati wa kupigania uhuru.
Angalia barua kutoka maktaba ya Bi. Amina Kinabo kuhusu ziara ya President wa TANJ Julius Nyerere Northern Province mwaka wa 1957.
Siku zote nikisononeka kwa kukosa picha tatu za wanawake shujaa wa Kilimanjaro waliopigania uhuru wa Tanganyika - Bi. Amina Kinabo, Halima Selengia na Mama bint Maalim.
Mzee Yusuf Olotu aliyenifundisha historia ya TANU Moshi mjini anasema TANU Moshi ilijengwa kwa juhudi za akina mama kwa uanachama na kwa fedha zao.
Nilihangaika kupata picha za akina mama hawa bila mafanikio.
Hivi mpaka lini tutaendelea kuipuuza historia ya mashujaa wetu?
Bi. Amina Kinabo