Amini usiamini! Nimeokota Tsh milioni 6

kikaniki

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2014
Posts
508
Reaction score
968
Ilikuwa hivi:

Jirani na ninapoishi kuna eneo limetengwa na Manispaa kwa ajili ya kuhifadhi takataka kwa muda kabla gari la Manispaa halijaja kubeba taka hizo.

Wakazi wengi wa mtaa wetu huona uvivu kwenda kumwaga taka ktk chemba hiyo iliyotengwa, badala yake husubiri usiku mwingi kuja kumwaga taka zao jirani kabisa na nyumba yangu.

Asubuhi ilipofika, nikaamka na kukuta furushi la taka jirani na kwangu.

Nikaghadhibika sana

Nikaamua kulibeba furushi hilo na kulipeleka dampo (chemba). Wakati nalikokota, furushi lile likanaswa na kipande cha mti, likapasuka na uchafu ukasambaa.

Hamadi!!!!

Nilichokiona, sikuamini. Nilipigwa butwaa. Baada ya akili kuwa Sawa, nikainama na kuokota na kukimbilia nyumbani, tena chumbani kwangu.

Nimezihesabu. Zipo Tsh 6,000,000 (milioni 6).
 

!
!
Hata ungekuta bilioni, bado tutatupa tu nyumbani kwako na hatutakuzolea teh teh teh
 
no shit?
 
subiri PM nyingi za wadada wa humu wakikuomba urafiki
 
jana housegirl wangu alikosea akachukua furushi langu nililohifadhia pesa zangu tsh milioni sita na kulitupa jalalani badala ya furushi la takataka,,, nina hakika ni pesa zangu naomba nirudishie mkuu usijali nitakupa genji...
 
Reactions: bdo
Hali ilivyokuwa ngumu kipindi hiki hata kuokota sarafu ni nadra!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…