A'more

A'more

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Nausikiliza huu wimbo hapa ofisini na unanipa hamu ya kufanya kazi. Shukrani kwa mwimbaji kuyatendea haki maneno yaliyomo ndani ya wimbo huu. Kaimba vizuri sana. Shukrani pia kwa mtunzi wake-Father G. Huyu bwana katunga nyimbo nyingi sana zilizovuma. Ni wakati sasa kuwaenzi watunzi wa nyimbo badala ya waimbai pekee. Tunzo hazitoshi.

Katika wimbo kuna baadhi maneno matamu kama hivi;
Na ukigusa moyo wangu ni wewe
ulobeba nafsi yangu ni wewe
huna wewe bila mimi, A'more
ulimwengu wote wajue ya kwamba ni wewe
A'more x5

usiumwe usiugue, uwe mzima daima
usisikize ya watu penzi letu kulitupa
na usibadili kipimo cha mapenzi unayonipa

sitokutoza ushuru, nitawale mi ni wako
pesa nyumba nayo gari si mali kitu kwangu
hata niwe jangwani wewe ni maji kwangu
una mapenzi ya kweli yao wote ya bandia....


sasa katika hili pamoja na maneno mazuri kwenye wimbo, ageutunga mwanamke ningefarijika zaidi. hii ni hali ya mwanaume anayeusemea moyo wa mwanamke. kwamba mwanaume anataka mwenza wake awe vipi.

ewe mwanamke;
ni kweli hutonitoza ushuru?
ni kweli pesa nyumba, magari si mali kitu kwako?
ni kweli mapenzi ya wengine ni ya bandia?
ni kweli nimebeba nafsi yako?
ni kweli ulimwengu wote wanatambua ni mimi pekee?

i wish ingekuwa hivi
 
Singles bana...kaaaz kwelikweli!....Kwa mtu kama mimi nishamalizana na mamii mapema asubuhi, muda huu ni kuwajibika na mkoloni!...Taratibu broda, utatulia muda mfupi baadaye!
 
Singles bana...kaaaz kwelikweli!....Kwa mtu kama mimi nishamalizana na mamii mapema asubuhi, muda huu ni kuwajibika na mkoloni!...Taratibu broda, utatulia muda mfupi baadaye!
ah kaka hii postt imebeba jumbe mbili muhimu
1. Ulishamalizana na mamii asubuhi- lucky her (hahahahhah)
2. Umri umekwenda (namaanisha umri wa ndoa) so kijana akikomaa ndoani ataona ni vya kawaida sio?

Mzima lakini?
 
ah kaka hii postt imebeba jumbe mbili muhimu
1. Ulishamalizana na mamii asubuhi- lucky her (hahahahhah)
2. Umri umekwenda (namaanisha umri wa ndoa) so kijana akikomaa ndoani ataona ni vya kawaida sio?

Mzima lakini?

Dadaangu, mi ni mzima, and iam so happy to come to the notion that you are fine!....Pole na kuchoka, but nadhani with any lucky umepata 'massaging'!
 
Singles bana...kaaaz kwelikweli!....Kwa mtu kama mimi nishamalizana na mamii mapema asubuhi, muda huu ni kuwajibika na mkoloni!...Taratibu broda, utatulia muda mfupi baadaye!
mkuu suala hili halina kumalizana. ni suala la kuendeleza pale ulipoachia kila wakati la sivyo wataendeleza wengine
 
Back
Top Bottom