Pre GE2025 Amos Makalla: Hoja ya Rais Mwinyi kuongezewa miaka ya Urais haipo

Pre GE2025 Amos Makalla: Hoja ya Rais Mwinyi kuongezewa miaka ya Urais haipo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (#CCM), Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla amesema hoja ya kuongeza muda wa Urais kwa Rais wa #Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi kutoka Miaka Mitano hadi Saba, haipo.

Akihojiwa na Clouds FM, Makalla amesema “Hilo jambo halipo, halijafika Halmashauri Kuu, CCM inaendeshwa na vikao, kikao cha Kamati Maalum Zanzibar halijafika.”

Awali, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa alinukuliwa akisema CCM Zanzibar imeona Serikali kuingia katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ni hasara na matumizi mabaya ya Fedha ndio maana wameona wawasilishe pendekezo la kuongeza muda wa kukaa madarakani."

Pia soma Kuelekea 2025 - CCM Zanzibar wapendekeza Rais Mwinyi atawale kwa miaka 7, wasema kufanya uchaguzi 2025 ni hasara na matumizi mabaya ya fedha za umma
 
  • Thanks
Reactions: Ame
^Hilo jambo halipo, halijafika Halmashauri Kuu^

RPC Mwanza: Hilo jambo kuhusu ulawiti wa RC Simiyu halijanifikia.

Tuliosomea Qba tumeelewa kwamba jambo lenyewe lingali njiani kuelekea Halmashauri Kuu.
 
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (#CCM), Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla amesema hoja ya kuongeza muda wa Urais kwa Rais wa #Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi kutoka Miaka Mitano hadi Saba, haipo.

Akihojiwa na Clouds FM, Makalla amesema “Hilo jambo halipo, halijafika Halmashauri Kuu, CCM inaendeshwa na vikao, kikao cha Kamati Maalum Zanzibar halijafika.”

Awali, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa alinukuliwa akisema CCM Zanzibar imeona Serikali kuingia katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ni hasara na matumizi mabaya ya Fedha ndio maana wameona wawasilishe pendekezo la kuongeza muda wa kukaa madarakani."

Zanzibar wana Katiba yao. Walipoitunga hawakupata baraka toka Bara ..... hivyo wanaweza kuibadilisha na kuongeaza term limit bila CCM.
 
Nilikuwa namsikiliza Leo Asbuhi Clouds Fm


Nadhani Masoud Kipanya, atakuwa na majawabu mazurii kuhusu viongozi wa Taasisi/mashirika na Taifa/nchi tulionao.

Thinking capacity,
Critical thinking,
Analytical minds,
Problem solv"" ".
 
Nilikuwa namsikiliza Leo Asbuhi Clouds Fm


Nadhani Masoud Kipanya, atakuwa na majawabu mazurii kuhusu viongozi wa Taasisi/mashirika na Taifa/nchi tulionao.

Thinking capacity,
Critical thinking,
Analytical minds,
Problem solv"" ".
 
Back
Top Bottom