Pre GE2025 Makalla Jimbo la Kigamboni mmezidi kujipitisha, msipojirekebisha tutawaengua

Pre GE2025 Makalla Jimbo la Kigamboni mmezidi kujipitisha, msipojirekebisha tutawaengua

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Minyukano ya makada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), inayoendelea kupigania Jimbo la Kigamboni imeuibua uongozi wa Chama hicho unaodai haufurahishwi na vitendo hivyo huku ukiahidi kuwashughulikia iwapo hawata jirekebisha.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Chanzo cha vurugu hizo kushamiri katika eneo hilo ni baada ya aliyekuwa Mbunge wake Dk Faustine Ndugulie na aliyekuwa Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, kufariki dunia usiku wa kuamkia Novemba 27, 2024 nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu.

 
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla amewakosoa baadhi ya Wanachama wa CCM wanaoonesha nia ya kuwania Jimbo la Kigamboni lililokuwa likiongozwa na marehemu Faustine Engelbert Ndugulile kinyume cha utaratibu.
 
Back
Top Bottom