MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,675
- 33,583
Wakuu,
Kocha wetu ni dhaifu mno kusoma mchezo na kubadili mbinu. Timu inacheza vile vile hata wapinzani wanapobadili mbinu. Mbaya zaidi kilema kikuu ni kocha kutojua namna ya kutumia viungo wetu. Hivi unamtumia kiungo kama Himid asaidie nini? Yule ni mkabaji tu na hawezi kuchezesha timu.
Badala ya kuingiza mtu wa kutuliza timu au kuongeza kasi ya mashambulizi unaingiza mkabaji tu na kufanya timu ielemewe. Nyoni aliomba sub mapema lakini haikufanyika hadi akalala chini na bado hawakufikiri haraka namna ya kujaza lile gap muhimu.
Amunike anafaa kuwa mkufunzi wa TFF kuendeleza program za soka lakini si mwalimu mzuri kabisa. Hakuna mechi aliyofanya sub za maana na akifanya ni too late damage inakuwa imeshakuwa kubwa na habadiliki haraka kwa kuwasoma wapinzani.
Wachezaji wanapambana wenyewe bila mbinu za ziada. Kwa timu hii hii angepatikana kocha anayewajua vizuri wachezaji wetu na anayeweza kubadilika kutokana na mchezo miujiza ingetokea.
Zambia walichukua hili kombe wakiwa hawana mastaa wa kutisha kulinganisha na wapinzani wao wengi. Technical bench ni msingi muhimu sana kabla hata ya timu yenyewe.
Wachezaji wetu wamepambana kwa uwezo wao wote lakini benchi la ufundi limewaangusha sana. Wasisingizie uzoefu mdogo, akina Okwi wana uzoefu gani? Jana tulihitaji uzoefu gani? Tatizo ni mbinu za kimichezo hatuna.
Kocha wetu ni dhaifu mno kusoma mchezo na kubadili mbinu. Timu inacheza vile vile hata wapinzani wanapobadili mbinu. Mbaya zaidi kilema kikuu ni kocha kutojua namna ya kutumia viungo wetu. Hivi unamtumia kiungo kama Himid asaidie nini? Yule ni mkabaji tu na hawezi kuchezesha timu.
Badala ya kuingiza mtu wa kutuliza timu au kuongeza kasi ya mashambulizi unaingiza mkabaji tu na kufanya timu ielemewe. Nyoni aliomba sub mapema lakini haikufanyika hadi akalala chini na bado hawakufikiri haraka namna ya kujaza lile gap muhimu.
Amunike anafaa kuwa mkufunzi wa TFF kuendeleza program za soka lakini si mwalimu mzuri kabisa. Hakuna mechi aliyofanya sub za maana na akifanya ni too late damage inakuwa imeshakuwa kubwa na habadiliki haraka kwa kuwasoma wapinzani.
Wachezaji wanapambana wenyewe bila mbinu za ziada. Kwa timu hii hii angepatikana kocha anayewajua vizuri wachezaji wetu na anayeweza kubadilika kutokana na mchezo miujiza ingetokea.
Zambia walichukua hili kombe wakiwa hawana mastaa wa kutisha kulinganisha na wapinzani wao wengi. Technical bench ni msingi muhimu sana kabla hata ya timu yenyewe.
Wachezaji wetu wamepambana kwa uwezo wao wote lakini benchi la ufundi limewaangusha sana. Wasisingizie uzoefu mdogo, akina Okwi wana uzoefu gani? Jana tulihitaji uzoefu gani? Tatizo ni mbinu za kimichezo hatuna.