Amvizia Binti Aliyekimbia Mabomu

muhosni

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2011
Posts
1,108
Reaction score
152
Ndugu zangu,

kwenye gazeti la Mwananchi la leo ukurasa wa tatu kuna habari yenye kichwa cha habari kama ilivyo hapo juu. Bahati mbaya hawajaipost lakini imeandikwa hivi;

Mwanaume ambaye hakufahamika jina lake katika hali isiyo ya kawaida, juzi usiku alitumia fursa ya milipuko ya mabomu kumshawishi msichana aliyekuwa akihaha kutafuta hifadhi akiwa na mdogo wake mgongoni, wafanye vitendo vya ngono......(inaendelea lakini habari kuu ndiyo hiyo)
 
Du...inaonyesha kalikuwa kabinti kadogo sana...Huyu kuna mahala panapomstahili, apelekwe mara moja!
 
Duh!! Kuna watu wengine wanatumia janga lililotokea kwa ajili ya kurubuni watu, alaaniwe
 

Du!!!! the guy is lunatic
 
pengine katumwa na shehe yahaya afanye hivyo kwa wahanga atakuwa tajiri
 
Hivi ethics za uandishi wa habari hazimtaki mwandishi akikutana na jambo kama hili ampeleke mtuhumiwa polisi pamoja na kuandhika taarifa husika?
 
Huu ni uzandiki kabisa afungwe

Atafungwa na nani sasa, ndiyo maana hapo juu nimehoji responsibility ya mwandhishi wa habari katika cases kama hizi. Anatakiwa atuletee habari tusikitike au anatakiwa amsaidie yule binti kisha atuletee habari?
 
Binadamu tunapenda kutumia matatizo ya wengine kupata manufaa.

Juzi usiku ilikuwa rahisi kumlaghai binti maana watu walikuwa desperate for help.
Nilipotelewa ndugu zangu na katika kuwatafuta ilikuwa unaweza kupakia watu kwenye gari (say U/ndege - Tazara au U/Uhuru) hata wasijiulize unakowapeleka so long as ametoka eneo hatari.
Mbaya ni kwamba wengine hata hawakuwa wamevaa kwa namna ya kujisitiri sana, nadhani ndipo mafirauni kama huyu jamaa wali-take advantage.
Zee la miaka 40 linataka kumla under-age (17yrs), hapa ndipo wanaume huwa tunaonekana kufanya kazi ambazo hata shetani asingethubutu.

The good side of the story ni kwamba jamaa hakufanikiwa maana binti alikuwa mjanja.
 
Hivi ethics za uandishi wa habari hazimtaki mwandishi akikutana na jambo kama hili ampeleke mtuhumiwa polisi pamoja na kuandhika taarifa husika?

Kwa kesi hii jamaa hakufanikiwa maana binti (17) aligoma kupelekwa gesti.
 
Thank God lilishindwa, jaman halina hata utu, bora lingepigwa na bomu . Laudhi sana!
 
Hapa ndipo ninapowazaga akili za wanaume ziko je??
Kwa sababu hata ikitokea vita utasikia wanawake wamebakwa bila hata huruma!!! Yani mi kuna wakati najiulizaga kwa nini Mungu aliumba wanaume kwa jinsi hiyo!! Daaa mi wanaume nawaogopa aisee!!! Ndio sio wanaume wote wenye roho kama hizi, lakini hebu wote vaeni uhusika halafu muone jinsi ambavyo mpo wa ajabu.
Daaa hapa hakuna cha kusema kaka angu, baba angu au sijui nani angu, so long as is a man!!!!!!! Why this?? Mnaongozwa na roho gani?? Ya Mungu au ya Shetani??

Daaaaaaah. Inauma sana aiseeeee!!!!
 
dah! taratibu LD, usije ukavunja skrini kwa hasira.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…